Nijuzeni kuhusu "Jambazi" Kasusura

Deo Corleone

JF-Expert Member
Jun 29, 2011
16,927
13,011
Wakuu mtusaidie sisi vijana wa 90s .

Huyu jamaa alihusishwa na mabilioni, sijui alikwapua benki au vipi?

Nilikuwa nasikia sikia tu story zake .

Pasco Na wengine ,mtujuze profile ya huyu jamaa Na alichofanya.
=======

3070502-png.241874

Mkuu Deo Corleone,

Ilikuwa Tar 2 Mwezi wa Nane mwaka 2001(2 August 2001) siku ya Alhamis, Justine Kasusura akiwa na wenzake watatu wafanyakazi wa Knight Support walikuwa uwanja wa ndege JKNIA wakichukua USD 2mils zilizokuwa zinatoka Marekani na kupelekwa tawi la Citibank(DSM). Ndipo Pepo la wizi lilimuingia Kasusura na kuwaweka wenzake chini ya ulinzi na kupiga hizo fedha.

Kasusura is still serving 30 years behind bars for armed robbery and theft.

Kuweka kumbukumbu sawa,alikua ni mtumishi wa Knight Support Tanzania LTD makao makuu pale Victoria (Dar es salaam),idara ya usafirishaji wa mali na pesa. Siku ya tukio Baba yangu mzazi ndiye aliyekuwa dereva wakiwa na kasusura kwenda airport kupokea pesa hizo.
Ulikua ni mchoro wa muda mrefu kati ya Kasusura,mke wa mkurugenzi wa Knight Support na akina urassa. Baada ya kupokea pesa na kutoka nje ya eneo tu,ndipo kasusura akatoa silaha na kumuwekea Mzee wangu kichwani apaki gari pembeni... zikafika gari za akina urassa wakachukua pesa zote na kutokomea. Mzee wangu akaenda kutoa taarifa kituoni,akachukuliwa na kuwekwa ndani kusaidia upelelezi. Kesi iliendelea akiwa gerezani keko,hadi kasusura alipokamatwa ndipo akaachiwa huru.

Ramani ya wizi: Siku ya tukio escotter wa zamu alijifanya anaumwa,ndipo Mke wa Mkurugenzi akaagiza Kasusura aje ashike zamu,akakabidhiwa silaha...ndipo mchezo ulivyokuwa.

Kesi yake ilikuwa na jambo moja kuu nalo ni jinsi alivyoteswa akiwa mikononi mwa polisi.Na ni Abdalla Zombe aliyeifanya shughuli hiyo.
Nikikumbuka maelezo na nikiskia Abdallah Zombe,naichukia dunia!!!!!!!
I wish kama ningepata fursa ya kufuatilia maisha binafsi ya Zombe.
 
Nilisikia akiwa askari wa KK alitorosha madola uwanja wa ndege badala ya kuyapeleka benki husika, akapanda nayo gari nyingine akazifanya zake na wenzake, akawa anatafutwa weee mwisho akajakukamatwa Mbeya akiwa hana kitu tena. Mwenye ufahamu vizuri atarekebisha.
 
Nilisikia akiwa askari wa KK alitorosha madola uwanja wa ndege badala ya kuyapeleka benki husika, akapanda nayo gari nyingine akazifanya zake na wenzake, akawa anatafutwa weee mwisho akajakukamatwa Mbeya akiwa hana kitu tena. Mwenye ufahamu vizuri atarekebisha.

Ahsante kwa info
 
Yes ni kweli alitorosha kama 1bn hivi na ushee.Alikamatwa Mbeya katika hotel iliyojulikana kwa jina la Three In One eneo la Soweto.
 
Huyo jamaa siyo noma bali ni mjinga. Waliofaidi hela yake ni akina Urassa ambao baba yao alikuwa mwanajeshi na ana baa pale whisho wa lami Gongo la Mboto. Yeye mjinga tu, ila wachagga akili kichwani katika mambo ya wizi.
 
Huyo jamaa siyo noma bali ni mjinga. Waliofaidi hela yake ni akina Urassa ambao baba yao alikuwa mwanajeshi na ana baa pale whisho wa lami Gongo la Mboto. Yeye mjinga tu, ila wachagga akili kichwani katika mambo ya wizi.

Ungeongezea nyama, hapo
 
Kasusura bwana alipata umaarufu ghafla. Baada ya kuchukua mzigo alizunguka karibu mikoa yote, kote huko alikopita alimwaga pesa kwa maafsa usalama. sijui yeye binafsi alifaidika vipi
 
Huyo jamaa siyo noma bali ni mjinga. Waliofaidi hela yake ni akina Urassa ambao baba yao alikuwa mwanajeshi na ana baa pale whisho wa lami Gongo la Mboto. Yeye mjinga tu, ila wachagga akili kichwani katika mambo ya wizi.

Duuuuu kweli akili ni nywele ww una fikir kwamba wizi ni akili au dhambi...?
 
Alihukumiwa kifungo cha kati ya miaka 3 na 5 nafikiri alishamaliza

Hilo la kumfananisha na Bujibuji umenivunja mbavu Mamndenyi

Mkuu mshana jr huyu Justine Kasusura alihukumiwa kwenda jela miaka 30 na kuchapwa viboko 12.. Alikata rufaa lakini rufaa yake ikatupiliwa mbali.. Jamaa aliondoka na dola taslim milioni 2.. Nakumbuka baadae kwa kuwa zile hela zilikuwa na serial no zinazofuatana Polisi wakawa wanafuatilia kwenye maduka ya kuuza pesa za kigeni..

Hilo la Mamndenyi kumpiga dongo Bujibuji mie silisemei maana amekuwa kama mjane siku hizi lol..
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom