NGULI
JF-Expert Member
- Mar 31, 2008
- 4,803
- 637
Ndg zangu wana JF na watanzania kwa ujumla. Na mika mingi tangu nimalize elimu ya juu hapa TZ nikabahatika kupata kazi. Kazi yangu ni inahusika na kutoa huduma kwa wateja sasa kabla hata sijaomba wala kuonyesha dalili za kuitaka rushwa wateja wamekuwa wakiniwekea katikati ya forms zao kiasi cha fedha kila mara nacho kifanya kwa vile kuna number zao za simu nawapigia na wakija nazirudisha zile fedha. Kwa sasa nakaribia kushindwa uvumilivu kwa vile kodi za nyumba ziko juu sana sana, nimekopa bank ili nijenge nimepata milioni 3 na nusu viwanja hatua 20x20 ni mil 5 je nitajenga kweli? Na shirika halina hata mpango wa kuongeza mishahara.
Wakati mwingine nashawishika Kula rushwa ila namwona kama Dr. Slaa ananiambia endelea tu watanzania wanakuona. Naona naharibu imani yangu na Mungu wangu.kwa sasa sahani ya chakula cha mchana imefikia TZS 3500-5000 na 3500 kwa maeneo ya ofisi yetu ni kwa mama ntilie. Wenzangu mnafanyaje mkipambana na hali kama hizi??
Cha kushangaza wenzangu niliotoka nao chuo wenye kipato almost sawa wana majumba makubwa Boko na Mbweni. Maisha sio mchezo.
Wakati mwingine nashawishika Kula rushwa ila namwona kama Dr. Slaa ananiambia endelea tu watanzania wanakuona. Naona naharibu imani yangu na Mungu wangu.kwa sasa sahani ya chakula cha mchana imefikia TZS 3500-5000 na 3500 kwa maeneo ya ofisi yetu ni kwa mama ntilie. Wenzangu mnafanyaje mkipambana na hali kama hizi??
Cha kushangaza wenzangu niliotoka nao chuo wenye kipato almost sawa wana majumba makubwa Boko na Mbweni. Maisha sio mchezo.