Kasomi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 11,036
- 20,337
Jopo la wataalam wa umoja wa mataifa limezitaka mamlaka nchini Nigeria kumuachilia huru mwanamume mmoja aliyekamatwa mwaka mmoja uliopita siku kama ya leo .
Mubarak Bala alikamatwa baada ya malalamishi kufikishwa katika kituo cha polisi katika jimbo la kaskazini mashariki la Kano kudai kwamba alikuwa amemfanyia kejeli mtume Mohammed kupitia ujumbe aliyoweka kwenye Facebook .
" Kukamatwa na kuzuiliwa kwa Bw. Bala sio tu ukiukaji wa haki zake za kimsingi lakini pia kunaathiri uhuru wa kimsingi nchini Nigeria'.Jopo hilo la umoja wa mataifa limesema kupitia taarifa .
Watalam hao wamesema wamefadhaishwa kwamba mamlaka za Nigeria hazikutii agizo la mahakama kuu disemba tarehe 21 mwaka jana la kumuachilia Bw. Bala
Mahakama ilikuwa imeagiza kwamba aachiliwe kwa dhamana na alipwe fidia ya ($650, £460) kwa sababu haki zake zilikiukwa
Kikao cha mahakama kilitarajiwa kufanyika tarehe 20 mwezi huu lakini hakikufanyika kwa sababu wafanyikazi wa idara ya mahakama wamegoma. Watalaam hao wa umoja wa mataifa wameitaka serikali kuhakikisha kwamba maamuzi ya mahakama yanaheshimiwa
Bwana Bala sio wa kwanza kujipata pabaya katika mkono wa sharia kuhusiana na imani kwani mwaka jana mwanamuziki Yahaya Sharif-Aminu, mwenye umri wa miaka 22 alihukumiwa kifungo cha kunyongwa kwa kulifanyia mzaha jina la mtume Mohammed .
Mahakama ya juu ya sheria ilimpata na kosa hilo katika jimbo la Kano baada ya wimbo mmoja aliyotunga kusambazwa kupitia Whatsapp mwezi machi mwaka huo .
Bwana Sharif-Aminu hakukana mashtaka hayo na alipewa fursa ya kukata rufaa dhidi ya hukumu aliyopewa .
Majimbo mengine kaskazini mwa Nigeria ambako kuna idadi kubwa ya waislamu yanatumia sheria za kawaida na zile za kiislamu -sharia .
Ni hukumu moja tu ya kifo iliyotolewa na mahakama ya Nigeria ya sharia ilitekelezwa tangu sheria hizo zirejeshwe nchini humo mwaka wa 1999.
Mubarak Bala alikamatwa baada ya malalamishi kufikishwa katika kituo cha polisi katika jimbo la kaskazini mashariki la Kano kudai kwamba alikuwa amemfanyia kejeli mtume Mohammed kupitia ujumbe aliyoweka kwenye Facebook .
" Kukamatwa na kuzuiliwa kwa Bw. Bala sio tu ukiukaji wa haki zake za kimsingi lakini pia kunaathiri uhuru wa kimsingi nchini Nigeria'.Jopo hilo la umoja wa mataifa limesema kupitia taarifa .
Watalam hao wamesema wamefadhaishwa kwamba mamlaka za Nigeria hazikutii agizo la mahakama kuu disemba tarehe 21 mwaka jana la kumuachilia Bw. Bala
Mahakama ilikuwa imeagiza kwamba aachiliwe kwa dhamana na alipwe fidia ya ($650, £460) kwa sababu haki zake zilikiukwa
Kikao cha mahakama kilitarajiwa kufanyika tarehe 20 mwezi huu lakini hakikufanyika kwa sababu wafanyikazi wa idara ya mahakama wamegoma. Watalaam hao wa umoja wa mataifa wameitaka serikali kuhakikisha kwamba maamuzi ya mahakama yanaheshimiwa
Bwana Bala sio wa kwanza kujipata pabaya katika mkono wa sharia kuhusiana na imani kwani mwaka jana mwanamuziki Yahaya Sharif-Aminu, mwenye umri wa miaka 22 alihukumiwa kifungo cha kunyongwa kwa kulifanyia mzaha jina la mtume Mohammed .
Mahakama ya juu ya sheria ilimpata na kosa hilo katika jimbo la Kano baada ya wimbo mmoja aliyotunga kusambazwa kupitia Whatsapp mwezi machi mwaka huo .
Bwana Sharif-Aminu hakukana mashtaka hayo na alipewa fursa ya kukata rufaa dhidi ya hukumu aliyopewa .
Majimbo mengine kaskazini mwa Nigeria ambako kuna idadi kubwa ya waislamu yanatumia sheria za kawaida na zile za kiislamu -sharia .
Ni hukumu moja tu ya kifo iliyotolewa na mahakama ya Nigeria ya sharia ilitekelezwa tangu sheria hizo zirejeshwe nchini humo mwaka wa 1999.