Nigeria: Arudisha cheti chuoni na kudai arudishiwe ada yake

sifi leo

JF-Expert Member
Mar 30, 2012
5,013
8,369
Hiii ni kweli kama umemaliza degree na huoni umuhimu wake we warudishie cheti wakupe ada uliyolipa ili uanzishe biashara.


===
Oludare Alaba; ni mhitimu wa Chuo Kikuu cha Teknolojia cha LAUTECH cha nchini Nigeria akihitimu katika Kitivo cha Kilimo ambaye amezua mjadala mitandaoni baada ya kusambaa kwa video yake akizua kasheshe katika sehemu ya mapokezi ya chuo hicho.

Oludare alikuwa akirudisha cheti chake cha digrii katika chuo hicho ili arejeshewe pesa zote alizozitumia kama ada ya masomo yake.

Katika video hiyo, Oludare anaonekana akilalamika kwamba masomo aliyoyapata katika chuo hicho hayajamfaidi kivyovyote na ndiyo maana alitaka kurejeshewa ada yake.

Video hiyo imepokelewa kwa hisia tofauti huku baadhi wakitumia misemo kumshauri kwamba mtu huwezi ukaila keki yako na bado ukataka kuwa nayo mkononi.

Baada ya video hiyo kusambaa, watu mbalimbali walimfikia na wengine kutaka kujua ni kwa nini aliamua kuchukua uamuzi kama huo wa kuzua kioja katika chuo chake cha awali.
 
Hiii ni kweli kama umemaliza degree na huoni umuhimu wake we warudishie cheti wakupe ada uliyolipa ili uanzishe biashara.

View attachment 2769291
===
Oludare Alaba; ni mhitimu wa Chuo Kikuu cha Teknolojia cha LAUTECH cha nchini Nigeria akihitimu katika Kitivo cha Kilimo ambaye amezua mjadala mitandaoni baada ya kusambaa kwa video yake akizua kasheshe katika sehemu ya mapokezi ya chuo hicho.

Oludare alikuwa akirudisha cheti chake cha digrii katika chuo hicho ili arejeshewe pesa zote alizozitumia kama ada ya masomo yake.

Katika video hiyo, Oludare anaonekana akilalamika kwamba masomo aliyoyapata katika chuo hicho hayajamfaidi kivyovyote na ndiyo maana alitaka kurejeshewa ada yake.

Video hiyo imepokelewa kwa hisia tofauti huku baadhi wakitumia misemo kumshauri kwamba mtu huwezi ukaila keki yako na bado ukataka kuwa nayo mkononi.

Baada ya video hiyo kusambaa, watu mbalimbali walimfikia na wengine kutaka kujua ni kwa nini aliamua kuchukua uamuzi kama huo wa kuzua kioja katika chuo chake cha awali.
Kwakeli turudishe tu
Tumepoteza muda na Hela
 
Ni sawa huyo jamaa kukosa kazi maana hana akili, kwa hiyo thaman ya Elimu ya ni cheti na sio content?
 
Hali ni ngumu. Hakuna uwiano sawa kati ya Elimu na engagement ya vijana kwenye shughuli za kujipatia kipato.

Tuanze kufundishana shughuli badala ya kazi,
Tatizo intentions yao ya mwanzo ni kuajiriwa. Hili ndo mbaya kuliko lolote.... wengi hawasomi kupata maarifa kuendesha professional walizosomea au kuendeleza kitu.

Kwa kesi hizi zikipimwa kwa kigezo Cha ajira mfumo wa elimu itakuwa haifai totally mana unapunguza watu kila ukienda juu. So, utawaumiza watu akili tu.

Wengi wetu tumekuwa tukijaji kwa Nini umesoma lakini haijakusaidia elimu yako tukiwa na maana moja tu. Maana ya kuajiriwa, lakin ukimuuliza kwa Nini umesoma na hubadilishi kitu kwenye taaluma yako unauliza competency level.

K
 
Back
Top Bottom