Nifanyeje?

Nifanyeje?

Mtoto mkubwa anasoma Diploma in Accountancy (namsomesha kwa kinguvunguvu maana ndugu zangu wote hawapendi). Huyu yupo chuoni. Wa pili amemaliza VETA (naye nililipa karo mpaka dadazangu wengine wamentenga), huyu ndio tatizo. He is 19 now. Wengine wawili wapo Sekondari Form 3 kitindamimba yupo Std 6. Huyo wa VETA ana walioko Sekondari wamekuwa mwiba sana kwa mama yangu. Lakini niwafanyeje??

pole sana..mimi naona itisha kikao na wawepo hao watoto wote na uwaeleze ubaya wa matendo yao,uwape muda wa mwezi mmoja wa kubadilika na ukiona mwezi umeisha lakin bado hakuna mabadiliko waachie nyumba ww mchukue mama uishi nae.Huyo mkubwa wa diploma anaweza kuangalia wenzie,msaada uliotoa unatosha wasijekumdhuru mama yako pia na wema wako ukageuka mwiba kwa ndugu zako wa tumbo moja maisha yote.
 
we jamaa unamkosea sana mama yako ila ww hujujui bado, yaan umeniudhi sana
kumpa mzigo mama wa watu kisa nini? Kama vp c ukae nao hao ndugu zako.....muache mama apumue banah!!!!!!!!!!!
 
ndg yangu dunia hii tenda wema nenda zako.So fukuza hao mb.wa. lasivyo watamuua mamayo kwa mawazo!..ww ni mwanaume waweza mchukua kabsa mamayo ukaish nae 4the rest of her life.Ni hayo2 mkuu
 
Unampa mama mateso asiyostahili,mchukue ukae naye.
Naamini Mna ndugu kwa baba na hao watoto wana ndugu wa mama yao,kaeni kikao cha familia kabidhi hao watoto waambie utalipa ADA shule ila watakula nini familia iamue. Wakimaliza shule unanawa mikono.
 
huyo wa veta fukuzilia mbali mwambie aende akatafute maisha yake huyo wa sec mtafutie boarding hapo abaki wa std six. mama yako ameshateseka sana wakati bb yk alipomwacha embu mpe uhuru amalizie uzee wake kwa amani jamani. huo wema wako ni mzuri lkn uwe na mipaka wangekuwa na adabu kweli watawasumbua maisha yenu yote. inaonekana wamelelewa kwa chuki.baki na huyo mdogo tu
 
Pole sana kk ila cha msingi mtoe kwanza mama yako kwenye nyumba umuhudumie prke yake hao watoto piga chini coz ndo walikuwa chanzo cha matatizo yako c mzee ana watoto wa nje ambao walituletea shida sana enzi hizo kiukweli hatuwatambui c tunaendelea na maisha yetu
 
unatakiwa kufanya maamuzi magumu sana ujue kila la kheri na mungu akutangulie
 
kaka pole sana tena sana maaana naisi hata mambo flani ayaendi vyema. Ni ivi jaribu kwenda kwa mama uongeee na wadogo zako ujue mama nae hatakiwi hapate tabu kwakuwa ashakuwa mtu mzima sana sasa ongea na wadogo zako na mama nakuomba utumie ujasiri sasa wakumtoa pale nyumbani ao huduma zao zitaendelea kama kawaida sema wasije wakuza na iyo nyumba ilo ndio langu
 
Wapeleke kwa mashangazi zao yaan upande wa baba yako, yaan wewe mvumilivu hongera kwa hilo, mm nisingoweza jaman nani kama mama sembuse hao intruder mpfyuuuuu
 
mkuu kwanza pole sana na misukosuko hiyo,cham msingi ni kwamba ndugu ni ndugu tu haijalishi ametoka katika tumbo gani,naamini paka wamekuwa na uwezo wa kutukana basi ni wamekuwa na wanjua nn wanafanya kwaiyo sasa wewe ukiwa mkubwa unawajibu wa kuwaita na kukaa nao friendly kama ndugu wakati huo huo kama rafiki jaribu kuwaeleza namna unavyoumia na jinsi wanavyofanya na waambie tu ukweli haupendezwi na hiyo hali so unawataka kubadiklika na wanapaswa kumuheshimu mama kama mama yao mzazi,fanya hivyo ukiona hawataki jirekebisha basi hilo ni gunia la misumali watafute ustaarabu mwingine.vilevile kumbuka kwamba ur mama ata the age of 70 ni miaka mingi sana na akili inakuwa kama mtoto so tatizo linaweza kuanzaia hapo pia so na unawajibu pia wa kuwaambia hilo hao madogo.all the best
 
We jamaa una Moyo wa Ajabu sana aise hongera sana na Mungu akujalie sana,

Mi kwa Akili zangu navyo zijua na namna navyo mkubali B mkubwa, Kitambo ningesha korofishana na hao Vijana.
 
Ahsante dadaangu lakini nimeshaongea nao sana lakin naona hawabadiriki ndo maana nimekuja hapa na ushauri nitakaoupata hapa nautekeleza kuanzia kesho.

Ss unasubiri nn km Umeshaona hawavadiriki?
 
Heshima kwenu wadau,

Mwaka 1990 marehemu baba yangu aliamua kuoa mke wa pili. Miaka mitatu baadaye (1993) yule mke wa pili akafanikiwa kumhamisha kimapenzi baba yangu, akaamua kuondoka kabisa pale nyumbani. Mimi na wadogo zangu tumeishi maisha ya kutokumwona baba akitoa huduma yoyote kwetu toka wakati huo hadi kifo kilipomfika yeye na mkewe huyo wa pili mwaka 2011 kwa kukatwakatwa na majambazi kwa madai kwamba ni wachawi. Wameacha watoto watano. Mimi ndiye kijana pekee wa kiume mkubwa na ambaye ndiye pekee mwenye elimu ya Chuo Kikuu na uwezo kidogo kifedha. Mama yetu mzazi bado yupo hai. Toka 2011 ndugu zangu walitamani sana tuwatelekeze wale watoto wa yule mama wa kambo. Mimi nilikopa roho ya simba, nikaingilia kati. Nilimjengea nyumba mama yetu mzazi (70 yrs) na hao watoto walioachwa. Wanaishi pamoja japo kwa taabu sana. Kwenye uzao wa mama yetu mzazi sote ni watu wazima. Hakuna hata mmoja anayeishi karibu na mzazi wetu huyo. Tumemwekea mfanyakazi wa ndani kumsaidia huku hao watoto wote bado wanasoma.

Leo kinachonisukuma kuja kuomba msaada wa mawazo hapa ni: kila siku hao watoto wamekuwa wasumbufu kwa mama yetu. Wanamtukana, wanamsema vibaya na hata kumsingizia kuwa ndiye aliwaua wazazi wao. Kila msichana ninayempeleka pale, wanamtukana hadi anatoroka. Hivi ninavyoongea mama yangu anaishi bila msaidizi. Ninaumia kuona mama anapata shida. Ninaumia kuwaza kumwondoa pale mama maana tunaua mji wa urithi na watoto watakosa msaada. Ndugu zangu hawanielewi japo wananiheshimu kama mtoto wa kiume. Wnashauri niwatelekeze wale watoto kwa kumwondoa mama yetu. Nipo njia panda. Naomba ushauri wenu wadau.

wapangir mbali na mama aisee...wanashida ao
 
Back
Top Bottom