Inaonekana ulipopata mualiko wa kwenda US hukumshirikisha ipasavyo mkeo, maamuzi yalikua ni yako tu pengine ni kwa ajili ya kitete cha safari, tatizo lako si kwamba lilianza baada ya wewe kufika US bali tatizo lilianza hata kabla hujaianza safari yako.
Kuna jambo unajaribu kulificha hapa, kua muwazi usaidiwe, kitendo cha mkeo kukwambia kua 'Nimekukataa ili nikuonyeshe kua Marekani sio kitu mbele yangu" kina ashiria kua uliithamini safari yako zaidi kuliko mkeo,sasa umesharudi na akili imekurudi.