Nifanye nini kutimiza malengo yangu

Nifanye nini kutimiza malengo yangu

King snr

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2015
Posts
1,165
Reaction score
1,474
Siku zote napenda kuwa lab.technician na ndio malengo yangu maana naipenda toka moyoni sasa tatizo linakuja katika kutimiza malengo yangu
Nimemaliza kidato cha nne (credit 1.9) sikuchaguliwa kidato cha tano nikachaguliwa special diploma udom(chem&math) sikuwaza kuja kuwa mwalimu na bado siamini kama nitakuwa mwalimu niliwashawishi wazazi niende advance private wakasema hawana uwezo nikawashawishi chuo cha afya pia hawana uwezo wanaona ni bora niende special diploma sasa hapa ndo ninapoona ugumu katika kufanikisha malengo yangu
Naombeni msaada wenu wa mawazo inawezekana kubadilisha kozi nikifika chuoni?
Nifanye nini ili niweze kutimiza malengo yangu?
napenda sana lab.technician
 
Dogo stop dreaming and walk your butt up!maisha sio rahisi kiasi icho,umepata nafasi ya kusoma chuo BURE..bado tena unataka ushauri wa nini?mimi sijui hii BRN imewaribu ninyi watoto kwa kiasi hicho..badala ya kushukuru mungu kwa nafasi hiyo unafikilia kitu kisichowezekana,NENDA KASOME MAMBO MENGINE UTAKUTANA NAYO MBELENI..ACHA UTOTO
 
nenda kasome, ili hali unavyoenda kusoma umesema ni chem&math, bado una uwezo wa kutimiza ndoto zako za kuwa lab tech baada ya kumaliza masomo yako ya uwalimu... malengo yako wala hayajafa ila ni wewe tu una wasi wasi
 
Nafasi ya kutimiza malengo yako ulikuwa nayo nzuri sana mwanzoni,like ungepata GPA ya kueleweka njia ingekuwa straight

Now nenda kasome(kuna wengine hata hiyo nafasi hawajaipata),,ukishakuwa mwalimu unaweza kwenda kujiendeleza na kusoma hiyo fani ya ndoto zako
 
Dogo stop dreaming and walk your butt up!maisha sio rahisi kiasi icho,umepata nafasi ya kusoma chuo BURE..bado tena unataka ushauri wa nini?mimi sijui hii BRN imewaribu ninyi watoto kwa kiasi hicho..badala ya kushukuru mungu kwa nafasi hiyo unafikilia kitu kisichowezekana,NENDA KASOME MAMBO MENGINE UTAKUTANA NAYO MBELENI..ACHA UTOTO

nashukuru kwa ushauri wako mkuu kama hakuna njia nyingine ya kutimiza malengo yangu sina jinsi itabidi nikubaliane na hali halisi
 
nenda kasome, ili hali unavyoenda kusoma umesema ni chem&math, bado una uwezo wa kutimiza ndoto zako za kuwa lab tech baada ya kumaliza masomo yako ya uwalimu... malengo yako wala hayajafa ila ni wewe tu una wasi wasi

nashukuru mkuu so inawezekana kusoma ualimu af nisiende kufundisha nikaenda lab.tech?
 
Nafasi ya kutimiza malengo yako ulikuwa nayo nzuri sana mwanzoni,like ungepata GPA ya kueleweka njia ingekuwa straight

Now nenda kasome(kuna wengine hata hiyo nafasi hawajaipata),,ukishakuwa mwalimu unaweza kwenda kujiendeleza na kusoma hiyo fani ya ndoto zako

nashkuru kwa ushauri wako mkuu kama itawezekana hivyo unavyosema nitaenda kujiendeleza maana wengine huwa wanakataliwa
 
Pole sana mdogo wangu I can feel what u ar trying to say... Unajua umaskini umechelewesha kama sio kukatisha ndoto za vijana wengi sana.... Mm nakushauri ukasome tu hiyo special diploma ya education kwa vile unapata full support kutoka bodi.... Kuhusu suala la kuhama course hiyo sahau kabisa na hata kama ukihama tatzo linakuja pale pale ufadhili So nenda tu Kasome ukishamaliza unapiga Kaz miaka kadhaa kisha utafufua ndoto za lab tec.... Unajua kuna watu wengine ili kuzifikia ndoto zao lazima wakutane na changamoto mbali mbali na ww ni mmojawapo so yakupasa uzikabili ili usonge mbele na ndo maisha yalivyo mkuu.... Ww hutokuwa wa kwanza wala wa mwisho kuna wengi tu washakutana na changamoto za aina yako na pengine kubwa kuliko zako na leo hii wako sehem wanafurahia kuzifikia ndoto zao japo safari ilikuwa na vikwazo vingi.... SO Always Never Give Up Regardless How Long U Gonna Take To Achieve Ur Dreams As Long As U Ave It In Ur Mind.
. All The Best.
 
mkuu inapita kama miezi mingapi baada ya kuwa mwalim nikitaka kujiendeleza?

Ki utaratibu ukae kazn miak mi3 lkn kama umeanda mazngira mapema hata baada ya mwaka 1 unachomoka.
Lkn jipange kujiendeleza alone unabak na salary yako tu
 
Unajua umaskini umechelewesha kama sio kukatisha ndoto za vijana wengi sana.... Mm nakushauri ukasome tu hiyo special diploma ya education kwa vile unapata full support kutoka bodi.... Kuhusu suala la kuhama course hiyo sahau kabisa na hata kama ukihama tatzo linakuja pale pale ufadhili So nenda tu Kasome ukishamaliza unapiga Kaz miaka kadhaa kisha utafufua ndoto za lab tec.... Unajua kuna watu wengine ili kuzifikia ndoto zao lazima wakutane na changamoto mbali mbali na ww ni mmojawapo so yakupasa uzikabili ili usonge mbele na ndo maisha yalivyo mkuu.... Ww hutokuwa wa kwanza wala wa mwisho kuna wengi tu washakutana na changamoto za aina yako na pengine kubwa kuliko zako na leo hii wako sehem wanafurahia kuzifikia ndoto zao japo safari ilikuwa na vikwazo vingi.... SO Always Never Give Up Regardless How Long U Gonna Take To Achieve Ur Dreams As Long As U Ave It In Ur Mind.
. All The Best.

nashkuru sana mkuu kwa kunitia moyo
 
Ki utaratibu ukae kazn miak mi3 lkn kama umeanda mazngira mapema hata baada ya mwaka 1 unachomoka.
Lkn jipange kujiendeleza alone unabak na salary yako tu

wakati najiendeleza mshahara nakuwa naendelea kupokea?
 
Dogo stop dreaming and walk your butt up!maisha sio rahisi kiasi icho,umepata nafasi ya kusoma chuo BURE..bado tena unataka ushauri wa nini?mimi sijui hii BRN imewaribu ninyi watoto kwa kiasi hicho..badala ya kushukuru mungu kwa nafasi hiyo unafikilia kitu kisichowezekana,NENDA KASOME MAMBO MENGINE UTAKUTANA NAYO MBELENI..ACHA UTOTO

hiyo ndio akili kubwa uliyonayo, pumba.v.u kabisa, kama ulishindwa ww usimkatishe mtu tamaa heri ungekaa kimya uweke akiba ya maarifa.
 
hiyo ndio akili kubwa uliyonayo, pumba.v.u kabisa, kama ulishindwa ww usimkatishe mtu tamaa heri ungekaa kimya uweke akiba ya maarifa.

Kama umeweza kunitukana mimi unaweza hata kutukana baba yako aliyekuzaa,soma comment yangu vizuri elewa concept yangu hata wewe itakusaidia katika maisha yako..nimekusamehe bure
 
Kama umeweza kunitukana mimi unaweza hata kutukana baba yako aliyekuzaa,soma comment yangu vizuri elewa concept yangu hata wewe itakusaidia katika maisha yako..nimekusamehe bure

samehe saba Mara 70
 
kaka, kama hamna namna kabisa nenda tu kasome halafu utarudi

nakupa mfano wa broo wangu alipenda sana kusoma kilimo hakua na uwezo hapo mwanzoni akachaguliwa ualimu akasoma 3yrs akamaliza akaajiriwa kajikusanya zaidi ya 5yrs kapata pesa akaacha akaenda mwanza pale kuna chuo cha mifugo kasoma diploma 3yrs kamaliza kaajiriwa arusha kapiga 1yr saiv anachukua dgree anaingia 2yr

note; age is just a number, kikubwa uzima ndo wakuomba kwa MUNGU
 
dogo ushauri wangu nenda shule ya alpha gems ipo moro ada ni laki hv shule ni nzuri sana. komaa na wazazi wakupeleke hawashindw hiyo laki 9.
achana na hiyo special diploma nenda kwanza shule ukasome.
 
Back
Top Bottom