Anna Mosha
JF-Expert Member
- Aug 18, 2014
- 209
- 61
Halafu Dongola si nakudai!!!! kumbe una pesa nyingi hivyo ila deni kulipa hutaki
tumia tu hiyo hela sijaona ubaya wake naona amekupa kwa wema. Alikuwa anakupenda na pengne anakukumbuka still maana aliye nae hakuwa chaguo lake. Amekupa kama appreciation yake kwako
Wewe tumia pesa hiyo ikusaidie huyo achana naye kama uitaki hiyo pesa.Nenda jukwaa la biashara kadonate kwa watu wanaohitaji mitaji na hawana pesa.
Huyo si wako tena hiyo ametoa kama zawadi tu kwako
Mwanaume/Mwanamke akiugusa moyo wako kwa namna ambayo haujawahi kuguswa na mtu mwingine hapa duniani ukitaka kumtafuta katika dunia hii ya leo utampata tu. Hizo pesa umeambiwa ni zawadi kwa kumbukumbu yako kwake hujaiba au kumdhulumu yoyote, mshukuru kwa msaada wake kisha ufanye yale uyatakayo kwenye maisha yako kwa kutumia hizo pesa.
Inaumiza sana kupendana na mtu kiasi hicho halafu Wazazi/ndugu ndio wanakuwa chanzo cha kuvunja penzi lenu, baadhi hugoma na kuendelea na penzi lao na hili huweza kuzua tafrani kubwa sana katika familia ya mke au mume na wapendanao pia.
Pesa hazina tatizo, tumia tu, kama anataka kuwasiluana na wewe atafanya hivyo hata kama utazirudisha hizo pesa....
labda tu kama hizo pesa zinahatarisha mahusiano yako mapya.... Vinginevyo zitumie tu.
Wewe acha ujinga chukua mzigo huo...amekupa kama fidia ya kukupotezea muda wako....nahis jamaa alikuwa anakupenda saaaan ndo maan ameamua akufanyie kitu hicho na ameona alikupotezea muda ktk uhusiano wenu hvyo amekuoa hyo hela kama ukumbusho wake ktk uhusiano wenu
hahahahahaha naona wafata nyao za miss chagga
Mwanaume/Mwanamke akiugusa moyo wako kwa namna ambayo haujawahi kuguswa na mtu mwingine hapa duniani ukitaka kumtafuta katika dunia hii ya leo utampata tu. Hizo pesa umeambiwa ni zawadi kwa kumbukumbu yako kwake hujaiba au kumdhulumu yoyote, mshukuru kwa msaada wake kisha ufanye yale uyatakayo kwenye maisha yako kwa kutumia hizo pesa.
Inaumiza sana kupendana na mtu kiasi hicho halafu Wazazi/ndugu ndio wanakuwa chanzo cha kuvunja penzi lenu, baadhi hugoma na kuendelea na penzi lao na hili huweza kuzua tafrani kubwa sana katika familia ya mke au mume na wapendanao pia.
Ni mwaka na miezi 2 imepita sasa tangia niachane na ex huyu kiukweli tulipendana sana tuliachana coz wazazi wake walimchaguli mke wa kumuoa coz aliwaheshimu sana wazazi wake hakutaka kupingana nao alifanya vile walivyotaka na huo ndo ulikuwa mwisho we2 kiukweli alitoka kwenye familia yenye uwezo na alikuwa mfanya biashara tofauti na mimi familia yangu ya kawaida 2.
Baada ya yeye kuoa nilikata kabisa mawasiliano naye lakini jana asubuhi nilipokea sms kutoka kwake aliandika hivi(wewe ni mwanake wa pekee kwangu kamwe sitokuja kukusahau pokea pesa izo nimekuingiazia kwenye account yako kiasi cha sh.milioni 4 naomba nikupatia zawadi hiyo kama kumbukumbu yako kwangu tarehe 13 mimi na mke wangu tunaamia Italy kwa heri na kubaki salama) nimebaki njia panda nifanye nini naogopa kuzitumia hizi pesa nimemshilikisha mama yangu kanishauri nizirudishe nahitaji mawazo yenu nifanye nini nimrudishie pesa zake coz now kiuchumi najiweza na sihitaji kabisa mawasiliano naye na naogopa pesa hizi isije ikawa chanzo cha mimi na yeye kuwasiliana.
hhahahh akulipe
Sina mume wala mchumba asante kwa ushauli
Ni mwaka na miezi 2 imepita sasa tangia niachane na ex huyu kiukweli tulipendana sana tuliachana coz wazazi wake walimchaguli mke wa kumuoa coz aliwaheshimu sana wazazi wake hakutaka kupingana nao alifanya vile walivyotaka na huo ndo ulikuwa mwisho we2 kiukweli alitoka kwenye familia yenye uwezo na alikuwa mfanya biashara tofauti na mimi familia yangu ya kawaida 2.
Baada ya yeye kuoa nilikata kabisa mawasiliano naye lakini jana asubuhi nilipokea sms kutoka kwake aliandika hivi(wewe ni mwanake wa pekee kwangu kamwe sitokuja kukusahau pokea pesa izo nimekuingiazia kwenye account yako kiasi cha sh.milioni 4 naomba nikupatia zawadi hiyo kama kumbukumbu yako kwangu tarehe 13 mimi na mke wangu tunaamia Italy kwa heri na kubaki salama) nimebaki njia panda nifanye nini naogopa kuzitumia hizi pesa nimemshilikisha mama yangu kanishauri nizirudishe nahitaji mawazo yenu nifanye nini nimrudishie pesa zake coz now kiuchumi najiweza na sihitaji kabisa mawasiliano naye na naogopa pesa hizi isije ikawa chanzo cha mimi na yeye kuwasiliana.