Nifanye nini ili nipate ajira?

Nifanye nini ili nipate ajira?

Mzunde

Senior Member
Joined
Aug 30, 2016
Posts
141
Reaction score
104
Jamani naandika kwa uchungu sana, mwenzenu nina miaka saba sasa tangu nimemaliza chuo sijawahi bahatika kupata ajira popotee.

Nilisoma BBA baada yakuona mambo magumu nikaenda driving nasasa nina hadi cheti cha NIT cha proffesional driving lakini bado sioni mwanga.

Naomba ushauri mzuri nifanyaje ili niweze kupata ajira?
 
jamani naandika kwa uchungu sana,,mwenzenu ninamiaka saba sasa tangu nimemaliza chuo sijawahi bahatika kupata ajira popotee,,nilisoma BBA baada yakuona mambo magumu nikaenda driving nasasa nina hadi cheti cha NIT cha proffesional driving lakini bado sioni mwanga,,naomba ushauri mzuri nifanyaje ili niweze kupata ajira?
AJIRA ni za WATOTO na NFUGU za "WALA NCHI"
Wewe na Mimi AJIRA yetu ni KUJIAJIRI au KILIMO
 
Kiukwel leo ndo siku ambayo nashangaa sana umesoma bba alafu unalalamika ajira wakati asilimia 90 mnafundishwa kujiajili
 
Kazi za udereva serikalini zimejaa wewe unakosaje?
Yawezekana kwenye kujisajili ajira portal umejichanganya.
Sekretarieti ya ajira bila shaka umeweka BBA then ukaweka na cheti cha udereva na leseni juu.
Inabidi alifanyie hili kazi, kama kajisajili Ajira portal akatoe hiyo qualification ya BBA na aweke ya udereva pekee.
 
Jamani naandika kwa uchungu sana, mwenzenu nina miaka saba sasa tangu nimemaliza chuo sijawahi bahatika kupata ajira popotee...
Pesa uliyotumia kusoma NIT ungeanzisha biashara sasa hivi ungekuwa mbali.. Nakushauri badili mtazamo wako sasa kuhusu ajira unaweza kujiajiri pia
 
Mkuu kwaniji usijikite kwenye udereva tu. Miaka saba bila ramani ni mingi sana mkuu.

Bora uwe hata dereva wa deiwaka kupata chochote huku ukiset mipango yako
 
Kazi za udereva serikalini zimejaa wewe unakosaje?

Yawezekana kwenye kujisajili ajira portal umejichanganya.

Sekretarieti ya ajira bila shaka umeweka BBA then ukaweka na cheti cha udereva na leseni juu.
hapana mkuu nimeweka udereva tuu
 
Nipo Dar es salaam naweza kufanya kazi yoyote ambayo ipo ndani yahizo proffesional mbili nilizonazo mkuu
Nilijua utajibu hivi. Ndo maana hupati kazi. Hakunaga kazi yeyeto.

Tatizo la vijana wengi wanaomaliza vyuo vikuu, wanamaliza wakati hawwajui ni kina nani.

Mimi ningependa kuwaasa kama ivyuatavyo. By the time unaingia mwaka wa mwisho orodhesha kazi zote ambazo mtu aliye soma kazi yako anaweza kufanya. Fanya utafiti kidogo kujua ni titlez zipi ziko mtaani. Kwa mfano makazini hakuna computer scientist...ila vyuo watu wanasoma Computer science. Mtu aliyesoma computer science anaweza kuwa systems analyst, systems administrator, Database administrator etc.
So angalia kwa masomo yako unaweza kuwa nani.

Ukisha orodhesha tick kazi moja au mbili ambazo unazioenda na unadhani unaweza kuzimudu.

Mwaka wa tatu tumia muda wako kusoma na kujisomea fani uliochagua. Kwa mfano kama umechagua systems analyst angalia roles za systems analyst ni nini. Jikite huko ili uwe mbobezi na kama programme yenu ina final years project chagua final year project ambayo itakujengea ujuzi na uelewa katika fani uliyo ichagua.

Na hata unapomaliza shule endelea kujiendeleza kati fani uliyo chagua ili uwe nondo.
Unapoenda mahali kutafuta kazi usiende kutafuta kazi yoyote. Sema mimi ni sales person natafuta kazi ya sales...au mimi ni mtu wa marketing au mimi ni sytstems analyst etc.

Unapoenda mahali na kusema natafuta kazi yoyote hakuna mtu atakupa kazi. Kwa sababu utaonekana mbabaishaji.

Kampuni. zinataka mtu anayejua kazi siyo mtu atakayefundishwa kufanya kazi.
 
Jamani naandika kwa uchungu sana, mwenzenu nina miaka saba sasa tangu nimemaliza chuo sijawahi bahatika kupata ajira popotee.

Nilisoma BBA baada yakuona mambo magumu nikaenda driving nasasa nina hadi cheti cha NIT cha proffesional driving lakini bado sioni mwanga.

Naomba ushauri mzuri nifanyaje ili niweze kupata ajira?
Pole sana ndugu. Huwa naona kazi nyingi-nyingi kwenye groups, channels na platforms mbalimbali zinazohusisha ajira (Telegram, LinkedIn, nk). Nikiona inayofaa, nitajitahidi niiweke hapa.
 
Back
Top Bottom