Tamatheo
JF-Expert Member
- May 28, 2012
- 3,298
- 1,562
Sitaki kutoa pongezi kwa maamuzi ya kutafuta mtoto nje ya ndoa ila kwa mbali naona tatizo kwa mkeo.....Kama ulivyosema mkeo anakataa kwenda kupata vipimo vya afya yake ni wazi anajua chanzo cha tatizo lake na kwa kuwa aliidhamiria ndoa kuliko matokeo ya ndoa ni wazi hata ungemfunga mikono na miguu kamwe asingekubali kwenda hospitali...Matokeo ya ukatili wake ni sababu ya kutokuwa na uwezo wa kupata mtoto kwani naamini yeye na hata familia yake inajua mchezo mzima. Angalizo..siku utakapo mwambia una mtoto out of ndoa atalipokea hili jambo kwa furaha ila amini usiamini wanawake wenye tatizo hili hawakawii kutoa uhai wa m2. Nakushauri ubadilishe staili ya kuishi nae, kwanza usiulize tena kuhusu kwenda hospitali ila jifanye kauzu, pili jitahidi kumpa nafasi ya upendo wake kama mke ambao naamini sasa umepungua au haupo tena kwani huko nyumba ndogo unavutwa na damu yako, tatu baada ya kitambo kidogo i.e hadi mwaka ukitekeleza kwanza na pili hapo juu kaa na mkeo katika hali ya kimahaba umuulize mkasa mzima, naamini utaambiwa vitu ambayo vinaweza kukuliza kwa kumwonea huruma au kukujaza hasira kwa kumwona mzembe ila upokee vyote katika hali ya upendo wa hali ya juu na Mwisho nakushauri umpe nafasi ya upendo moyoni mwako kwani miaka 10 ya ndoa yako inatoa picha ya maisha mazuri mliyokaa pamoja. Sina la kushauri kuhusu nyumba ndogo ila waweza rejea viapo vyako vya ndoa.