Poor Brain
JF-Expert Member
- Jul 5, 2019
- 27,402
- 54,846
Hapo mkuu nimekuelewa mazima aiseee yaani hapo nimekupata daah..Unajua mkuu wewe unachanganya mambo ndio maana hunielewi. Kuna tofauti kati ya mtu anayefanya biashara ili apate miambili ya kula leo na anayefanya ili aidhi kidon. Ninachokisema mimi, hio 500 ni nyingi sana hio, sasa ninaposema nyingi wewe unaanza kuwaza afanye biashara ya 500k apate faida anunue gari, ajenge aishi vizuri, hapana. Ukienda uswahilini kuna akina mama wanachoma mandazi, chapati au vitumbua. Mtaji wao hata 100k haufiki. Anaamka asubuhi achoma maandazi, kufika saa5 yameisha. Anachukua faida ananunua unga na fungu la samaki mchana umepita, jioni wali maharage, kesho tena. Hio ni biashara, vipi huyo wa 500k?
Sheria ya biashara ni moja tu, pamoja na kuwa na akili, uendeshaji sahihi nk, ila pia ili upate faida kubwa lazima u wekeze zaidi, hilo halikwepeki. Ukiuza pipi utawekeza kidogo na faida itakua ndogo, ukiuza magari utawekeza zaidi na faida itakua kubwa.
Narudia tena 500k ni hela kubwa sana na biashara za huo mtaji zipo nyingi. Amini kwamba 500k ni dream mtaji wa watu wengi sana, kuna watu wanaitafuta hata nusu tu ya hio ili waamze safari zao. Narudia usichanganye kupata faida kubwa, kubadili maisha na huo mtaji mdogo, havitawezekana kirahisi
Maana nayoona hapa kwangu naona kabisa kuja kujenga daaah nikaze sana an sana sana mno