Nifanyaje ili nijitoe ktk mfuko wa bima ya afya

Nifanyaje ili nijitoe ktk mfuko wa bima ya afya

wa hapahapa

JF-Expert Member
Joined
Aug 22, 2012
Posts
7,460
Reaction score
4,402
Kwa kuzingatia wajibu wa taasisi hiyo ya kuhudumia huduma za Afya Bure kwa wanachama wake wale walio na utegemezi pamoja na mwanachama mkuu ambaye ana mkataba wa kudumu kazini ambao anaweza kuchangia mfuko huo kila mwezi.


Pamoja na taasisi hiyo kufanya kazi kwa uwezo wake lakini bado hakuna huduma bora au kuwa tija na viwango vya kukidhi ubora ktk vituo vyingi vinavyotumiwa ktk kutoa huduma zao hasa ktk Zahanati na Hospitali za wilaya na hata mkoa kwa kushindwa kuwa na Dawa za kutosha, wataalam na vifaa tiba kulingana na mahitaji, na ukosefu wa huduma nyinginezo kwa wanachama wake.


Kwa kuwa nimeona hayo najiuliza, nifanyaje ili nihame ktk shirika/ taasisi hii maana yapo mashirika mengine yana huduma kama hizo na bora, za kampuni binafsi zinazotoa huduma kwa wakati na ubora zaidi.

Pia najiuliza kwa nini wanachama hawapewi uhuru wa kuwa mwanachama au lah… .. maana inatokea jina la mfanyakazi lipo NHIF pasipo hata ridhaa ya muhusika. Na je kama Hana nia na kuchangia ktk mfuko huo achukue hatua zipi ?/! ili ajitoe


Ni hayo tu wana JF, baada ya kero/ hoja nyingi sn nilizoziona.
 
kwa mantiki hii
1. hakuna haki/fao la kupata mwanachama hakihama ktk huduma za taasisi hiyo ??

2. na je bunge liliunda taasisi hiyo na kuipa madaraka ya kunyanyasa haki za wafanyakazi pasipo ridhaa zao kwa kuwasajiri bila taarifa, kuwanyima haki ya kuhamia ktk kampuni binafsi, pamoja na kutoridhisha kwa huduma za Afya zinazotolewa bure.
 
Jamani hii mifuko ya huduma kwa watumishi inakera sana hasa huu wa bima,unakwenda kutibiwa unaambiwa dawa zimekwisha huende ukanunue kwenye maduka ya dawa lakini kila mwezi nachangia.kwa kweli kama kuna mbinu za kujinasua mimi nitakuwa wa kwanza
 
Tatizo kubwa hasa kwa watumishi ni kuwa
hakuna hiari lujiunga bali ni lazima maana
viongozi hasa wa idara hufaika mno.

Utata unakuja kwenye huduma kuwa mbovu
 
Jamani hii mifuko ya huduma kwa watumishi inakera sana hasa huu wa bima,unakwenda kutibiwa unaambiwa dawa zimekwisha huende ukanunue kwenye maduka ya dawa lakini kila mwezi nachangia.kwa kweli kama kuna mbinu za kujinasua mimi nitakuwa wa kwanza

naamini wapo wengi sana waliochoshwa na shirika hili na wanania kujitoa uanachama, tatizo ni haki/njia ya kujitoa bado hamna taratibu zinazoeleweka.

pia inakera sana pale unapofika ktk ofisi zao zilizopo Dar kwa lengo la kuongeza au kufanya mabadiliko yaani utazungushwa sana ili mradi utoe chochote...,
 
Tatizo kubwa hasa kwa watumishi ni kuwa
hakuna hiari kujiunga bali ni lazima maana
viongozi hasa wa idara hunufaika mno.

Utata unakuja kwenye huduma kuwa mbovu

yaani hapo ktk red, ndio nnapochoka mimi, kwa nn iwe SHURTI kuwa mwanachama, hapohapoa HUDUMA zenyewe mbovu, utaambiwa ambulance mbovu au lipia mafuta, ukifika hospitali napo dawa zilizopo ni za maumivu/ panado tu nyingne mgaonjwa akanunue Pharmacy.... huku taasisi hiyo ikichukua michango kila mwezi kwa wanachama wake

taasisi hiyo pia inasaidia kiasi wanachama waliopo hapa mjini lakini wa huko mbali na Dar nawashauri wajitoe tu maana huko Sitimbi/ au vijijini huduma hii ni Kimvuli tu . na haina msaada ni heri ulipie huduma kama wateja/ wagonjwa wengne.
 
suruhu acha kazi

naamini akili zako zina shida kdg..... hapa ishu sio kuacha kazi, ni haki/hiari ya mwanachama wa bima iko wapi ??,

si suruhu kwa mwanachama kuacha kazi kwaajiri ya NHIF.... hatakuwa CHIZi

shida watz wamezoea kusukumwa/kuburuzwa kama ng'ombe na wenye kufuata mkumbo wa maslahi ya wachache kama bendera ifuatavyo upepo.
 
naamini wapo wengi sana waliochoshwa na shirika hili na wanania kujitoa uanachama, tatizo ni haki/njia ya kujitoa bado hamna taratibu zinazoeleweka.

pia inakera sana pale unapofika ktk ofisi zao zilizopo Dar kwa lengo la kuongeza au kufanya mabadiliko yaani utazungushwa sana ili mradi utoe chochote...,

naamini akili zako zina shida kdg..... hapa ishu sio kuacha kazi, ni haki/hiari ya mwanachama wa bima iko wapi ??,

si suruhu kwa mwanachama kuacha kazi kwaajiri ya NHIF.... hatakuwa CHIZi

shida watz wamezoea kusukumwa/kuburuzwa kama ng'ombe na wenye kufuata mkumbo wa maslahi ya wachache kama bendera ifuatavyo upepo.

kwa sheria namba 8 ya mwaka 1999 CAP 395 R.E 2002,
Mtumishi yoyote wa serikali kwa mujibu wa sheria hii ni mwanachama wa mfuko wa taifa wa bima ya afya. uanachama ni lazima kwa watu hawa. sheria ilipitishwa na bunge la jamuhuri la muungano wa tanzania. bunge ni uwakilishi wa wananchi hivyo mimi na wewe tuliwakilishwa na wabunge wetu wakapitisha sheria hii.

hivyo basi kigezo cha kwanza kabisa cha wewe kuwa mwanachama ni wewe mtumishi wa serikali kama hutaki yafuatayo unatakiwa kufwata
1. kama mtumishi wa serikali acha kazi au jiajiri mwenyewe au ajiriwa katika mashirika binafsi uweze kuchagua bima ya afya unayoitaka.
2. mwambie mbunge wako apeleke hoja binafsi bungeni kutoa sheria hii. ikijadiliwa na kuonekana inafaa kutolewa au kurekebishwa na kuweka uhiari basi itafanyika kuwa hivyo.
 
n mfuko ambao umejaa ukirtimba ndan yake sana hata tu form yao kuijaza wanahitaji watoto na wazaz na sio wategemezi!!!!! sasa swal la msingi n hl kama mtu n mnufaikaji wa mfuko husika na hajaoa wala kuolewa na wazaz wake n wanufaikaji wa mfuko je! hatuon mtu huyu anakatwa hela bure?
 
naamini wapo wengi sana waliochoshwa na shirika hili na wanania kujitoa uanachama, tatizo ni haki/njia ya kujitoa bado hamna taratibu zinazoeleweka.

pia inakera sana pale unapofika ktk ofisi zao zilizopo Dar kwa lengo la kuongeza au kufanya mabadiliko yaani utazungushwa sana ili mradi utoe chochote...,

mkuu wa hapahapa pole kwa masaibu yaliyokupata,sijui kama wewe ni mwajiriwa wa serikali au taasisi binafsi,kwa sababu kama ni mwajiriwa wa serikali huna uchaguzi,kwa baadhi ya taasisi binafsi mwajiri na mwajiriwa mnaweza kukubaliana kujiunga ama la,na kwa uzoefu wangu tatizo kubwa la NHIF ni kung'ang'aniza watoa huduma wafuate bei zao ambazo mara nyingi huwa zipo chini sana ukilinganisha na bei za soko jambo linalopelekea wanachama wa NHIF kunyanyaswa na kubaguliwa.
 
Last edited by a moderator:
kwa sheria namba 8 ya mwaka 1999 CAP 395 R.E 2002,
Mtumishi yoyote wa serikali kwa mujibu wa sheria hii ni mwanachama wa mfuko wa taifa wa bima ya afya. uanachama ni lazima kwa watu hawa. sheria ilipitishwa na bunge la jamuhuri la muungano wa tanzania. bunge ni uwakilishi wa wananchi hivyo mimi na wewe tuliwakilishwa na wabunge wetu wakapitisha sheria hii.

hivyo basi kigezo cha kwanza kabisa cha wewe kuwa mwanachama ni wewe mtumishi wa serikali kama hutaki yafuatayo unatakiwa kufwata
1. kama mtumishi wa serikali acha kazi au jiajiri mwenyewe au ajiriwa katika mashirika binafsi uweze kuchagua bima ya afya unayoitaka.
2. mwambie mbunge wako apeleke hoja binafsi bungeni kutoa sheria hii. ikijadiliwa na kuonekana inafaa kutolewa au kurekebishwa na kuweka uhiari basi itafanyika kuwa hivyo.

AKSANTE SANA,
NAAMINI NA WENGINE WATAELEWA KWA NINI UANACHAMA NI SHURTI KUJIUNGA, JAPO TUPO KTK DUNIA YA FREEDOM OF CHOICE, kwamba kila mtu anauhuru wa kuchagua anachotaka ikiwa ataweza kukigharamia na kiwe HALALI kisheria.
 
kwa mantiki hii
1. hakuna haki/fao la kupata mwanachama hakihama ktk huduma za taasisi hiyo ??

2. na je bunge liliunda taasisi hiyo na kuipa madaraka ya kunyanyasa haki za wafanyakazi pasipo ridhaa zao kwa kuwasajiri bila taarifa, kuwanyima haki ya kuhamia ktk kampuni binafsi, pamoja na kutoridhisha kwa huduma za Afya zinazotolewa bure.
Mkuu huduma zile hazitolewi bure si unachanga every month?
 
mkuu wa hapahapa pole kwa masaibu yaliyokupata,sijui kama wewe ni mwajiriwa wa serikali au taasisi binafsi,kwa sababu kama ni mwajiriwa wa serikali huna uchaguzi,kwa baadhi ya taasisi binafsi mwajiri na mwajiriwa mnaweza kukubaliana kujiunga ama la,na kwa uzoefu wangu tatizo kubwa la NHIF ni kung'ang'aniza watoa huduma wafuate bei zao ambazo mara nyingi huwa zipo chini sana ukilinganisha na bei za soko jambo linalopelekea wanachama wa NHIF kunyanyaswa na kubaguliwa.

kifupi, mi naona taasisi hii Efficiency yake ni ndogo sana na wanaonufaika ni wachache
sio wachangiaji wote wanapata huduma na kuridhika nayo ktk taasisi hii.
 
Mkuu huduma zile hazitolewi bure si unachanga every month?

ni kweli kila mwezi wanachama wanachanga....
lakini huduma zao ni kichefu chefu kabisa, tena hasa hizi zinazotolewa na vituo vya serikali.

cjui wamepanga kutudhurumu pesa zetu kweupe mchana wkt huduma zao ni za kubahatisha.
 
kwa sheria namba 8 ya mwaka 1999 CAP 395 R.E 2002,
Mtumishi yoyote wa serikali kwa mujibu wa sheria hii ni mwanachama wa mfuko wa taifa wa bima ya afya. uanachama ni lazima kwa watu hawa. sheria ilipitishwa na bunge la jamuhuri la muungano wa tanzania. bunge ni uwakilishi wa wananchi hivyo mimi na wewe tuliwakilishwa na wabunge wetu wakapitisha sheria hii.

hivyo basi kigezo cha kwanza kabisa cha wewe kuwa mwanachama ni wewe mtumishi wa serikali kama hutaki yafuatayo unatakiwa kufwata
1. kama mtumishi wa serikali acha kazi au jiajiri mwenyewe au ajiriwa katika mashirika binafsi uweze kuchagua bima ya afya unayoitaka.
2. mwambie mbunge wako apeleke hoja binafsi bungeni kutoa sheria hii. ikijadiliwa na kuonekana inafaa kutolewa au kurekebishwa na kuweka uhiari basi itafanyika kuwa hivyo.
asante kaka umenisaidia,maana yeye kaomba msaada sasa watu tunamsaidia ,yeye anatutia vidole vya macho wakati yeye ndio mwenye shida,na huu ni ushauri tu mshikaji usijenge chuki.
 
kifupi, mi naona taasisi hii Efficiency yake ni ndogo sana na wanaonufaika ni wachache
sio wachangiaji wote wanapata huduma na kuridhika nayo ktk taasisi hii.

upo sahihi kabisa mkuu wa hapahapa,ufanisi wa NHIF upo chini sana,na kwa bahati mbaya hakuna kiongozi yeyote anayejali,walichofanya hawa viongozi wetu ni kuanzisha card maalum kwa ajili yao na wategemezi wao (NHIF GREEN CARDS) ambazo kimsingi zionawatofautisha wao na wanachama wengine wa NHIF kwa sababu kwa card zao wanapata huduma katika hospitali bora kabisa za binafsi jambo ambalo mimi na wewe hatutaweza kutibiwa!

sisi wa mijini tuna unafuu mkubwa sana maana angalau unaweza kuchagua kituo chenye unafuu,wenzetu hawana uchaguzi huo,wanalazimika kupokea huduma mbovu zilizopo karibu,na pia hata wakipewa fomu maalum ya NHIF ya kwenda kuchukua dawa wanalazimika kusafiri umbali mrefu kuzifuata pharmacy zinazopokea prescription za NHIF na wao pia wanakunyima dawa kwa sababu bei ya NHIF haiwalipi.
 
Last edited by a moderator:
Wafanyakazi wa serikali nao wanabaguliwa. Mimi nafanya kazi katika shirika la uma (SU) na nililazimishwa kujiunga na NHIF. Lakini nina marafiki kadhaa wanaofanya BoT, wameniambia wafanyakazi wa pale wamekatiwa bima ya AAR.
Cha kushangaza hii bima ya afya kuna dawa ambazo ni lazima mgonjwa alipie, eti hospitali zote zimeandikiwa dawa zitakazolipiwa na NHIF. Kwa mfano dawa za malaria ni mseto, lakini cotexin hailipiwi. yaani itakubidi unywe dawa ambazo hutumii, kisa umekata bima ya afya.
 
Wafanyakazi wa serikali nao wanabaguliwa. Mimi nafanya kazi katika shirika la uma (SU) na nililazimishwa kujiunga na NHIF. Lakini nina marafiki kadhaa wanaofanya BoT, wameniambia wafanyakazi wa pale wamekatiwa bima ya AAR.
Cha kushangaza hii bima ya afya kuna dawa ambazo ni lazima mgonjwa alipie, eti hospitali zote zimeandikiwa dawa zitakazolipiwa na NHIF. Kwa mfano dawa za malaria ni mseto, lakini cotexin hailipiwi. yaani itakubidi unywe dawa ambazo hutumii, kisa umekata bima ya afya.

mimi nafanya kazi BOT card tunayotumia ni JUBILEE
 
upo sahihi kabisa mkuu wa hapahapa,ufanisi wa NHIF upo chini sana,na kwa bahati mbaya hakuna kiongozi yeyote anayejali,walichofanya hawa viongozi wetu ni kuanzisha card maalum kwa ajili yao na wategemezi wao (NHIF GREEN CARDS) ambazo kimsingi zionawatofautisha wao na wanachama wengine wa NHIF kwa sababu kwa card zao wanapata huduma katika hospitali bora kabisa za binafsi jambo ambalo mimi na wewe hatutaweza kutibiwa!

sisi wa mijini tuna unafuu mkubwa sana maana angalau unaweza kuchagua kituo chenye unafuu,wenzetu hawana uchaguzi huo,wanalazimika kupokea huduma mbovu zilizopo karibu,na pia hata wakipewa fomu maalum ya NHIF ya kwenda kuchukua dawa wanalazimika kusafiri umbali mrefu kuzifuata pharmacy zinazopokea prescription za NHIF na wao pia wanakunyima dawa kwa sababu bei ya NHIF haiwalipi.

kwaiyo hawa wanaotumia Green Card ndio wa Serikali Kuu na ile nyingine ni kwa TAMISEmi wa vijijini..... huu ni ubaguzi kabisa.

hii nchi tafikiri inaendeshwa na majongoo.
.... hapo hamna usawa.
 
Back
Top Bottom