Nifanyaje ili nijitoe ktk mfuko wa bima ya afya

Nifanyaje ili nijitoe ktk mfuko wa bima ya afya

upo sahihi kabisa mkuu wa hapahapa,ufanisi wa NHIF upo chini sana,na kwa bahati mbaya hakuna kiongozi yeyote anayejali,walichofanya hawa viongozi wetu ni kuanzisha card maalum kwa ajili yao na wategemezi wao (NHIF GREEN CARDS) ambazo kimsingi zionawatofautisha wao na wanachama wengine wa NHIF kwa sababu kwa card zao wanapata huduma katika hospitali bora kabisa za binafsi jambo ambalo mimi na wewe hatutaweza kutibiwa!

sisi wa mijini tuna unafuu mkubwa sana maana angalau unaweza kuchagua kituo chenye unafuu,wenzetu hawana uchaguzi huo,wanalazimika kupokea huduma mbovu zilizopo karibu,na pia hata wakipewa fomu maalum ya NHIF ya kwenda kuchukua dawa wanalazimika kusafiri umbali mrefu kuzifuata pharmacy zinazopokea prescription za NHIF na wao pia wanakunyima dawa kwa sababu bei ya NHIF haiwalipi.

Sasa wewe unaongelea miundo mbinu ya vijijini ulitegemea NHIF ifanye nini ikiwa hakuna vituo vyenye ubora huko huoni imejitahidi hata kuingia mikataba na maduka ya dawa muhimu na pharmacies pale ambapo dawa zinakosekana mahospitalini zahanati na vituo vya afya?

ni vema muelewe kuwa NHIF haimiliki kituo chochote cha kutoa huduma inachofanya ni kulipa madeni ya huduma za matibabu ambazo watu huenda kutibiwa iwe yupo karibu na zahanati hospitali ya wilaya au hospitali ya kidini iliyo karibu nae.

wewe umetembea vijijini au unasema tu mimi nimetembea maeneo mengi vijijini hata kama mtumishi asingekuwa na NHIF STILL ANGEKWENDA KATIKA VITUO HIVYO HIVYO VILIVYOPO MAENEO YALIYO KARIBU NAE. hapa tatizo sio NHIF tatizo ni vituo vyetu vyote vya serikali kuwa na huduma mbovu na ukosefu wa dawa na kuwa na uhaba wa vituo vingi vya binafsi vinavyoweza kumpa mtu uchaguzi.

mimi natumia jubilee card ukienda regency foleni ni ile ile huduma mbovu na majibu mabovu kutoka kwa wahudumu wa hospitali sote tunaipata sawa si wa NHIF,JUBILEE WALA AAR hakuna ubaguzi wowote unaofanywa.wote tunateseka tu ukiingia asubuhi unatoka mchana au jioni.
kuhusu green card unaongea usichokijua. jitahidi kujua green card ni kitu gani na utofauti wake na matumizi yake na upatikanaji wake. tafuta taarifa za kutosha ndio useme mambo mengine.
 
....kwa uzoefu wangu tatizo kubwa la NHIF ni kung'ang'aniza watoa huduma wafuate bei zao ambazo mara nyingi huwa zipo chini sana ukilinganisha na bei za soko jambo linalopelekea wanachama wa NHIF kunyanyaswa na kubaguliwa

Hapo umenena sahihi sana mkuu!
 
mimi nafanya kazi BOT card tunayotumia ni JUBILEE

sasa hiyo ya kupitia hiyo Card ya Jubilee mnaweza kupata tiba za ARR ??

kwa nn, tusigawanyike tu, wale wa JUbilee (serikali kuu) wawe ktk taasisi yao na wale wengine TamiseMI wawe na shirika lao jingine tofauti.
 
Wandugu mi napita tu.

Ila matatizo yote yaliyoelezwa hapo juu siyo ya NHIF hayo ni matatizo ya mfumo wa huduma za afya ndani ya nchi yetu. Bima ya Afya imesajili hospitali, zahanati na vituo vyote pamoja na maduka ya dawa bila kujali hospitali ya dini au ya mtu binafsi ili kuhakikisha wanachama wake wanapata huduma sahihi lakini bado tu malalamiko yapo. Je wale wanachama wa ARR, JUBILEE na MOMENTUM wanatibiwa katika vituo vilivyopo nchi gani? Mbona ni hapa hapa Tanzania?

Mi nadhani ni swala la taasisi husika ambazo ni MSD au bohari ya madawa kuhakikisha dawa na vifaa tiba vinapatikana mahospitalini na siyo swala la kulaumu NHIF.

Pia pambaneni na serikali iboreshe huduma za Afya nchini maana kazi ya NHIF ni kuhakikisha inakulipia huduma popote nchini sasa kama hiyo huduma haipatikani sehemu fulani hilo siyo kosa la NHIF.
 
sasa hiyo ya kupitia hiyo Card ya Jubilee mnaweza kupata tiba za ARR ??

kwa nn, tusigawanyike tu, wale wa JUbilee (serikali kuu) wawe ktk taasisi yao na wale wengine TamiseMI wawe na shirika lao jingine tofauti.

ninachoweza kukuhakikishia ni kuwa kadi zote hizo zina ukomo wa matibabu lakini NHIF haina ukomo wa matibabu.

la pili hilo ni wazo lifikishe panapohusika lifanyiwe kazi ( bungeni) maana hapo ndipo pana marekebisho ya sheria.
 
Wafanyakazi wa serikali nao wanabaguliwa. Mimi nafanya kazi katika shirika la uma (SU) na nililazimishwa kujiunga na NHIF. Lakini nina marafiki kadhaa wanaofanya BoT, wameniambia wafanyakazi wa pale wamekatiwa bima ya AAR.
Cha kushangaza hii bima ya afya kuna dawa ambazo ni lazima mgonjwa alipie, eti hospitali zote zimeandikiwa dawa zitakazolipiwa na NHIF. Kwa mfano dawa za malaria ni mseto, lakini cotexin hailipiwi. yaani itakubidi unywe dawa ambazo hutumii, kisa umekata bima ya afya.

yaani hadi leo tupo ktk zama za utumwa kwa kujitakia au kulazimishwa japo ni karne ya 21.
ndio maana mimi nataka kujitoa uanachama pasipo kuacha kazi,
1. kwa kutotumia huduma za NHIF japo nachangia.
2. namimi nitaandikisha wale ngugu zangu maskini wa vijijini wanataka utumwa kama huo.
 
Sasa wewe unaongelea miundo mbinu ya vijijini ulitegemea NHIF ifanye nini ikiwa hakuna vituo vyenye ubora huko huoni imejitahidi hata kuingia mikataba na maduka ya dawa muhimu na pharmacies pale ambapo dawa zinakosekana mahospitalini zahanati na vituo vya afya?

ni vema muelewe kuwa NHIF haimiliki kituo chochote cha kutoa huduma inachofanya ni kulipa madeni ya huduma za matibabu ambazo watu huenda kutibiwa iwe yupo karibu na zahanati hospitali ya wilaya au hospitali ya kidini iliyo karibu nae.

wewe umetembea vijijini au unasema tu mimi nimetembea maeneo mengi vijijini hata kama mtumishi asingekuwa na NHIF STILL ANGEKWENDA KATIKA VITUO HIVYO HIVYO VILIVYOPO MAENEO YALIYO KARIBU NAE. hapa tatizo sio NHIF tatizo ni vituo vyetu vyote vya serikali kuwa na huduma mbovu na ukosefu wa dawa na kuwa na uhaba wa vituo vingi vya binafsi vinavyoweza kumpa mtu uchaguzi.

mimi natumia jubilee card ukienda regency foleni ni ile ile huduma mbovu na majibu mabovu kutoka kwa wahudumu wa hospitali sote tunaipata sawa si wa NHIF,JUBILEE WALA AAR hakuna ubaguzi wowote unaofanywa.wote tunateseka tu ukiingia asubuhi unatoka mchana au jioni.
kuhusu green card unaongea usichokijua. jitahidi kujua green card ni kitu gani na utofauti wake na matumizi yake na upatikanaji wake. tafuta taarifa za kutosha ndio useme mambo mengine.

nimekusoma Iron Lady,mimi ni mtumishi mwandamizi wa afya na kila siku nawahudumia wanachama wa NHIF. kwa kazi yangu nimezunguka karibu mikoa yote tanzania na ninayafahamu vizuri sana mazingira na changamoto za huduma za afya vijijini na nilichokisema ni kwamba kama wa mjini mnalalamika kuhusu huduma za afya,waliopo vijijini ndio wana hali mbaya kabisa! nafahamu sio jukumu la NHIF kujenga na kuboresha miundo mbinu vijijini lakini inauma sana mtu anapokuwa anakatwa mshahara wake na inamchukua zaidi ya mwaka kupata NHIF CARD na hata akiipata haimtofautishi na yule asie nayo kwani anapata huduma mbovu japo ameshazilipia kwa kukatwa mshahara! na nikwambie tu kwa kazi yangu nilishapewa offer ya kubadilisha NHIF card yangu nipewe GREEN CARD lakini sikuona faida yake kwa sababu kwa hapa nilipo hata uwe na kadi gani huduma ni zilezile,sina choice kama ulizonazo wewe hapo Dar.

ni kweli pia kwamba NHIF wameingia mikataba na private pharmacies lakini hebu siku moja jaribu kuzunguka na prescrition ya NHIF uone utakavyopigwa danadana,sio kwamba hawana dawa ila bei elekezi ya NHIF kwenye baadhi ya dawa haitoshi hata kufidia bei ya kunulilia kwa wholesale,nikwambie tu bei elekezi za NHIF zinazotumika sasa zilifanyiwa review march 2012!
 
Last edited by a moderator:
Mi nadhani Nhif bado ni BABALao ukilinganisha na hizi insurance binafsi
 
Mi nadhani Nhif bado ni BABALao ukilinganisha na hizi insurance binafsi

ni level au status yake kwa kuwa ipo ngazi ya taifa na imekuwa established na Bunge lakini ni hamna kitu, ni wachache wanao nufaika na wengine kuibiwa michango yao.
 
ni kwamba kama wa mjini mnalalamika kuhusu huduma za afya,waliopo vijijini ndio wana hali mbaya kabisa! nafahamu sio jukumu la NHIF kujenga na kuboresha miundo mbinu vijijini lakini inauma sana mtu anapokuwa anakatwa mshahara wake na inamchukua zaidi ya mwaka kupata NHIF CARD na hata akiipata haimtofautishi na yule asie nayo kwani anapata huduma mbovu japo ameshazilipia kwa kukatwa mshahara!

ni kweli pia kwamba NHIF wameingia mikataba na private pharmacies lakini hebu siku moja jaribu kuzunguka na prescrition ya NHIF uone utakavyopigwa danadana,sio kwamba hawana dawa ila bei elekezi ya NHIF kwenye baadhi ya dawa haitoshi hata kufidia bei ya kunulilia kwa wholesale,nikwambie tu bei elekezi za NHIF zinazotumika sasa zilifanyiwa review march 2012!

hapo ktk red, hata mimi pananigusa sn.... yaani tafikiri jamaa wana kufanyia Recruitment ya ajira kumbe ni registration ya kawaida ya huduma ambayo cku hizi technolojia inasaidia kuwa rahisi lakini mambo yanafanyika kiurasimu sana.
 
hapo ktk red, hata mimi pananigusa sn.... yaani tafikiri jamaa wana kufanyia Recruitment ya ajira kumbe ni registration ya kawaida ya huduma ambayo cku hizi technolojia inasaidia kuwa rahisi lakini mambo yanafanyika kiurasimu sana.

mkuu wa hapahapa jambo hili linasikitisha na kushangaza sana,ndugu yangu amekatwa mshahara miaka mitatu bila kupata NHIF card mpaka amerudi tena kusoma bila kufaidika na jasho lake! halafu kadi zenyewe mbona ni za kawaida sana? kwa nini inachukua muda na usumbufu mwingi kupatikana?
 
Last edited by a moderator:
Wandugu mi napita tu.

Ila matatizo yote yaliyoelezwa hapo juu siyo ya NHIF hayo ni matatizo ya mfumo wa huduma za afya ndani ya nchi yetu. Bima ya Afya imesajili hospitali, zahanati na vituo vyote pamoja na maduka ya dawa bila kujali hospitali ya dini au ya mtu binafsi ili kuhakikisha wanachama wake wanapata huduma sahihi lakini bado tu malalamiko yapo. Je wale wanachama wa ARR, JUBILEE na MOMENTUM wanatibiwa katika vituo vilivyopo nchi gani? Mbona ni hapa hapa Tanzania?

Mi nadhani ni swala la taasisi husika ambazo ni MSD au bohari ya madawa kuhakikisha dawa na vifaa tiba vinapatikana mahospitalini na siyo swala la kulaumu NHIF.

Pia pambaneni na serikali iboreshe huduma za Afya nchini maana kazi ya NHIF ni kuhakikisha inakulipia huduma popote nchini sasa kama hiyo huduma haipatikani sehemu fulani hilo siyo kosa la NHIF.

mkuu uko sahihi kabisa kwamba tatizo la msingi ni ubovu wa mfumo wa huduma za afya lakini sio kweli kwamba NHIF wameingia mkataba na hospitali ZOTE,walianza na za serikali,mashirika ya umma na madhehebu ya dini,kwa sasa hata baadhi ya vituo vya mashirika binafsi (NGOs) vimeanza kusajiliwa,sijui kama wanasajili vituo vinavyomilikiwa na watu binafsi ambavyo ndio vipo vingi hasa maeneo ya mijini.
 
kwa sheria namba 8 ya mwaka 1999 CAP 395 R.E 2002,
Mtumishi yoyote wa serikali kwa mujibu wa sheria hii ni mwanachama wa mfuko wa taifa wa bima ya afya. uanachama ni lazima kwa watu hawa. sheria ilipitishwa na bunge la jamuhuri la muungano wa tanzania. bunge ni uwakilishi wa wananchi hivyo mimi na wewe tuliwakilishwa na wabunge wetu wakapitisha sheria hii.

hivyo basi kigezo cha kwanza kabisa cha wewe kuwa mwanachama ni wewe mtumishi wa serikali kama hutaki yafuatayo unatakiwa kufwata
1. kama mtumishi wa serikali acha kazi au jiajiri mwenyewe au ajiriwa katika mashirika binafsi uweze kuchagua bima ya afya unayoitaka.
2. mwambie mbunge wako apeleke hoja binafsi bungeni kutoa sheria hii. ikijadiliwa na kuonekana inafaa kutolewa au kurekebishwa na kuweka uhiari basi itafanyika kuwa hivyo.


Good reply!!
 
mkuu uko sahihi kabisa kwamba tatizo la msingi ni ubovu wa mfumo wa huduma za afya lakini sio kweli kwamba NHIF wameingia mkataba na hospitali ZOTE,walianza nppa za serikali,mashirika ya umma na madhehebu ya dini,kwa sasa hata baadhi ya vituo vya mashirika binafsi (NGOs) vimeanza kusajiliwa,sijui kama wanasajili vituo vinavyomilikiwa na watu binafsi ambavyo ndio vipo vingi hasa maeneo ya mijini.
Vyote husajiliwa kiongozi. Kiwe ni cha mtu binafsi au shirika la dini ili mladi kina usajili wa wizara ya afya nhif wanakisajili.
 
Acha kuumwa utatoka automatic

mmmhh ........... kama ujaeleweka ?/! ugonjwa upi, na hicho kifaa kinapatikana ktk mitambo,
au una comment zaid ya hiyo...... tupo sote lkn ktk JF.
 
mkuu wa hapahapa jambo hili linasikitisha na kushangaza sana,ndugu yangu amekatwa mshahara miaka mitatu bila kupata NHIF card mpaka amerudi tena kusoma bila kufaidika na jasho lake! halafu kadi zenyewe mbona ni za kawaida sana? kwa nini inachukua muda na usumbufu mwingi kupatikana?

hapo ndipo inaposikitisha na kukatisha tamaa na mashirika au taasisi kama hizi kwa kumkata mtu fedha ya mchango kila mwezi kwa miaka kadhaa na pasipo kupata huduma staili yeye mhusika/mfanyakazi au mtegemezi wake... si haki

pia kwa teknolojia ya sasa hata ukipoteza ATM card ya Benki haiwezi kuzidi wiki 4 hadi 6 kadi yako mteja unapata na kuendelea na transaction kama kawaida........
lakini ktk taasisi hii suala hili limekuwa na changamoto sana hadi wateja wanashindwa kupata usajiri wa Card kwa wakati.... (hii inatia mashaka hata ktk matumizi ya shirika, ukusanyaji wa mapato na utoaji wa ruzuku).

lakini hapo juu Iron lady kasema mengine ni ya Bungeni lakini nako huko ni NZZZZZ!!!!!!/?
 
sasa maswali mengine hayana kichwa wala mguu. wewe ulijiunga vp hadi uulize jf ujitoe vp? huna HR hapo unapofanyia kazi? wakati unajaza fomu na kusubmit picha ulimpa nani? kamuulize huyohuyo utoke vp.
 
Wafanyakazi wa serikali nao wanabaguliwa. Mimi nafanya kazi katika shirika la uma (SU) na nililazimishwa kujiunga na NHIF. Lakini nina marafiki kadhaa wanaofanya BoT, wameniambia wafanyakazi wa pale wamekatiwa bima ya AAR.
Cha kushangaza hii bima ya afya kuna dawa ambazo ni lazima mgonjwa alipie, eti hospitali zote zimeandikiwa dawa zitakazolipiwa na NHIF. Kwa mfano dawa za malaria ni mseto, lakini cotexin hailipiwi. yaani itakubidi unywe dawa ambazo hutumii, kisa umekata bima ya afya.

Sio BOT tu, hata Tanesco nao wanatumia AAR,,

Mashirika ya serikali makubwa yamegoma wafanyakazi wake kutumia nhif sababu wanajua ni magumashi..

Wafanyakazi wa BOT, Tanesco,etc wanatibiwa hospitali za nguvu as Aga khan, first track muhimbili, etc ambapo hizo hospitali haziitaki nhif
 
Back
Top Bottom