MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Naomba kuwauliza hivi hiki kipindi kipya kiitwacho GIRL TALK kinachorushwa na Star tv kina maudhui gani au kimewekwa kwa maana gani? Kiukweli ninayoyasikia katika hiki kipindi nadhani ni udhalilishaji tu dhidi yenu na ushamba mtupu na nahisi hata aliyekibuni hicho kipindi atakuwa alipigika sana pande za KIMBOKA kama siyo AFRIKA SANA.
Tokea nianze kukiangalia sasa ni dakika ya 42 ninayoyasikia ni maneno kama haya yafuatayo:
Nitawashukuruni mno dada zangu kama mkinijibu na ni kipindi ambacho huwa kipo hewani Startv kila siku ya Jumamosi saa 4 na nusu hadi saa 5 na nusu usiku.
Binafsi kimenishtua na kunisikitisha mno kwani kiukweli kabisa hakiendani kwa 100% na maadili ya kitanzania.
Tokea nianze kukiangalia sasa ni dakika ya 42 ninayoyasikia ni maneno kama haya yafuatayo:
- Mwanamke anatakiwa kuvaa chupi gani.
- Mwanamke anatakiwa kunyoa mavuzi yake mara ngapi kwa wiki.
- Sehemu za SIRI za Mwanamke zina maana gani.
- Uvaaji wa PEDI.
- Wanawake kuvaliana nguo hasa SKIN TIGHTS na CHUPI.
- Mwanamke wa KIJANJA unatakiwa uweje au aweje.
- Mwanamke UMASIKINI anautaka mwenyewe.
Nitawashukuruni mno dada zangu kama mkinijibu na ni kipindi ambacho huwa kipo hewani Startv kila siku ya Jumamosi saa 4 na nusu hadi saa 5 na nusu usiku.
Binafsi kimenishtua na kunisikitisha mno kwani kiukweli kabisa hakiendani kwa 100% na maadili ya kitanzania.