Wakuu nimekuwa nikipata shida sana naomba anaejua AM inaanza saa ngapi na kama inaisha saa ngapi animbie pamoja na PM pia
==========
==========
AM na PM inatumika ktk mfumo wa masaa 12, sio masaa 24.
Hivyo ukiona namba kisha ina AM au PM, jua kwamba ni mfumo wa masaa 12, usitegemee kuona AM na PM ktk muda kama 1300, 1547 1800 etc.
AM kirefu chake ni ANTE MERIDEAM (before middday-kabla ya mchana) na PM kirefu chake ni POST MERIDEAM (past midday-Baada ya mchana).
AM huanza kutumika saa sita usiku mpaka saa tano na dk 59 asubuhi. Pm hutumika kuanzia saa sita mchana mpaka saa tano na dk 59 usiku.