NIDA Wilaya ya Kasulu mnawasababishia Wananchi usumbufu na kuwaingiza gharama!

Dusabimana

JF-Expert Member
Oct 24, 2019
278
246
Kama kichwa habari hapo juu kinavyosema. Hivi hamuoni kuwa mnasababisha usumbufu kwa kubandika namba za NIDA za Wilaya nzima eneo moja tu. Watu wasafiri toka Vijijini kuja Mjini kuangalia namba za usajili wao, kwa kulipia nauli! Mfano kutoka Kagerakanda, Asante Nyerere, Makere na huko kwingine, nauli ndani ya Gari ikiwa chini ni 5000 au 7000 kwa Mtu mmoja, hapo nikuja Mjini bado kurudi! Bado Msongamano utakao kuwepo hapo Community Center mlipo bandika hizo namba!

Mbaya zaidi namba zimebandikwa ndani ya Compound ambayo ina kieneo kidogo. Leo jion tu ilikuwa ni varangati kwa Watu waliopo hapa Mjini, wakati wakitafuta namba zao, kuanzia kesho si ndo itakuwa kizaa zaa! Mmeshindwa kitu gani kwenda kubandika hizo namba Vijijini na kwenye Mitaa Watu walipo jiandikishia?! Mwaka jana wakati Wananchi wa Kata ya Murusi pekee tu wakipeleka fomu zao za NIDA pale community Center.

Mama mmoja aliyekuwa ana Mtoto Mgongoni bahati mbaya alianguka chini akakanyagiwa chini kwaajili ya Msongamano na Mtoto akapoteza Maisha! Bado hamjifunzi kitu hapo.Badilikeni nasiyo kufanya mambo hovyo hovyo utadhani bado tupo enzi za Ujima. Magari yapo, Barabara zipo.

Pelekeni hizo namba Vijijini na kwenye Mitaa.
 
Daaah rip mtoto
Hapo hata serikali isikie hiyo habari ya hiko kifo cha uyo mtoto japo wamsaidie uyo mama maskini

yess BiShoo haswaaA
 
Daaah rip mtoto
Hapo hata serikali isikie hiyo habari ya hiko kifo cha uyo mtoto japo wamsaidie uyo mama maskini

yess BiShoo haswaaA
Taifa hili tuna baadhi ya Mijitu ya ajabu ipo kwenye nafasi lakini haifikiri wala kutenda vyema!
 
R.I.P mtoto.
Kweli hawapo organised, si kuna watendaji kata na vijiji, kwanini wasipeleke katika kila kata halafu watendaji wa vijiji warahisishe kazi kila kijiji ili kuwaondolea usumbufu wananchi.
Maana safari ya kutoka Kagerankanda mpaka Kasulu ni mwendo haswa!
 
Tz Ni Kama vile Kuna kashetani na kametupanda kichwani! Kashetani kenyewe kanaitwa ujinga! Nida badala wapunguze matatizo wanaongeza
 
R.I.P mtoto.
Kweli hawapo organised, si kuna watendaji kata na vijiji, kwanini wasipeleke katika kila kata halafu watendaji wa vijiji warahisishe kazi kila kijiji ili kuwaondolea usumbufu wananchi.
Maana safari ya kutoka Kagerankanda mpaka Kasulu ni mwendo haswa!
Ni mbali sana! Halafu Mtu anatoa hela yake ya nauli, namba na jina lake asivikute! Leo tu Watu wengi hawajaona namba zao!
 
Tz Ni Kama vile Kuna kashetani na kametupanda kichwani! Kashetani kenyewe kanaitwa ujinga! Nida badala wapunguze matatizo wanaongeza
Hata Enzi za Pilato na Herode walikuwa na utaratibu mzuri kuliko Tz hii ya leo! Tunasoma maandiko.
 
Back
Top Bottom