Sophist
Platinum Member
- Mar 26, 2009
- 4,486
- 3,411
NIDA Imevunja Katiba ya Nchi
Mamlaka ya Vitambulisho Nchini Tanzania (NIDA) yamekiuka Katiba ya Nchi. NIDAimeundaa mfumo wa kukusanya taarifa za wakaazi nje ya mfumo rasmi wa serikaliuliowekwa na kutambuliwa kikatiba.
Mfumo uliondaliwa na NIDA unamtambua Mjumbe wa Nyumba Kumi wa CCM kamaMamlaka rasmi ya kuthibitisha uhalali wa ukaazi wa mwananchi anayejiandikishakupata kitambulisho cha taifa.
Kwa mujibu wa Katiba na sheria Mjumbe wa Nyumba 10 si sehemu ya mfumo wauongozi wa dola. Mamlaka rasmi wa uongozi wa dola unaanzia kwa Mwanyekiti waMtaa (mijini) au Mwenyekiti wa Kitongoji (vijijini).
Uchunguzi nilioufanya Jijini Dar es Salaam umebaini kuwa mwananchianalazimishwa kumtambua/kutambuliwa na Mjumbe wa Nyumba 10 ili akubaliwekuorodhesha majina ya watu katika kaya yake. Aidha, upande wa kulia katika vitabu(template)vya NIDA unaonesha na kumtaka karani wa NIDA kuandika jina la Mjumbewa Nyumba 10 kama mdhamini kuthibitisha ukweli wa taarifa za mkaazi.
Vilevile, maudhui ya mafunzo kwa makarani wa NIDA yanaonesha (makaraniwamefundishwa hivyo) kuwa Mjumbe wa Nyumba 10 wa CCM ni mamlaka rasmi na kamilikuthibitisha uhalali wa ukaazi wa wanakaya.
Kana kwamba hiyo haitoshi, NIDA inawalipa pesa wajumbe wa nyumba 10 wa CCM kwakazi ya 'kuandaa' wakaazi katika himaya yake ya nyumba 10. Yaani kazi wa uwelediya kuhamasisha watu kujiandikisha kwa ajili ya kupata vitambulisho vya taifawamepewa Wajumbe wa Nyumba 10 wa CCM bila hata kufuata sheria ya manunuzi yaumma ya 2004.
Ni vigumu kuamini kuwa uamuzi huu wa NIDA umetoke kwa bahati mbaya. Hapana.Ni mkakati rasmi wa kisiasa wa Serikali na CCM kutumia fursa, hata kwa kukiukaKatiba na sheria, kujiandalia na kujihakikishia wapiga kura wa 2015. Ni mkakatisawia na ule ulioasisiwa na Komandoo Salmin Amour Zanziba enzi hizo kuzuiaWazanzibari, wengi wao wakiwa Wapemba, wasipate fursa ya kupiga kura katikachaguzi zilizofuata baada ya ule wa mwaka 1995. Tusishangae iwapo masibu ya Zanzibarya vitambulisho wa ukaazi kuamua nani aruusiwe kujiandikisha kupiga kura au layataamia Tanzania Bara come 2015.
Wadau wafuatao wanapashwa kuchukua hatua stahiki, ikiwezekana hata kupelekapublic litigation Mahakama Kuu dhidi ya NIDA kukiuka Katiba na Sheria;
Pale ambapo makosa yamekwishafanyika, mchakato urudiwe upya. Lakini paleamabapo mchakato bado haujaanza panatakiwa marakebisho kurudiwa haraka.
Wahenga walisema, Ada yaMja Kunena; tusipoziba ufa tutakuja kujenga ukuta.
Mamlaka ya Vitambulisho Nchini Tanzania (NIDA) yamekiuka Katiba ya Nchi. NIDAimeundaa mfumo wa kukusanya taarifa za wakaazi nje ya mfumo rasmi wa serikaliuliowekwa na kutambuliwa kikatiba.
Mfumo uliondaliwa na NIDA unamtambua Mjumbe wa Nyumba Kumi wa CCM kamaMamlaka rasmi ya kuthibitisha uhalali wa ukaazi wa mwananchi anayejiandikishakupata kitambulisho cha taifa.
Kwa mujibu wa Katiba na sheria Mjumbe wa Nyumba 10 si sehemu ya mfumo wauongozi wa dola. Mamlaka rasmi wa uongozi wa dola unaanzia kwa Mwanyekiti waMtaa (mijini) au Mwenyekiti wa Kitongoji (vijijini).
Uchunguzi nilioufanya Jijini Dar es Salaam umebaini kuwa mwananchianalazimishwa kumtambua/kutambuliwa na Mjumbe wa Nyumba 10 ili akubaliwekuorodhesha majina ya watu katika kaya yake. Aidha, upande wa kulia katika vitabu(template)vya NIDA unaonesha na kumtaka karani wa NIDA kuandika jina la Mjumbewa Nyumba 10 kama mdhamini kuthibitisha ukweli wa taarifa za mkaazi.
Vilevile, maudhui ya mafunzo kwa makarani wa NIDA yanaonesha (makaraniwamefundishwa hivyo) kuwa Mjumbe wa Nyumba 10 wa CCM ni mamlaka rasmi na kamilikuthibitisha uhalali wa ukaazi wa wanakaya.
Kana kwamba hiyo haitoshi, NIDA inawalipa pesa wajumbe wa nyumba 10 wa CCM kwakazi ya 'kuandaa' wakaazi katika himaya yake ya nyumba 10. Yaani kazi wa uwelediya kuhamasisha watu kujiandikisha kwa ajili ya kupata vitambulisho vya taifawamepewa Wajumbe wa Nyumba 10 wa CCM bila hata kufuata sheria ya manunuzi yaumma ya 2004.
Ni vigumu kuamini kuwa uamuzi huu wa NIDA umetoke kwa bahati mbaya. Hapana.Ni mkakati rasmi wa kisiasa wa Serikali na CCM kutumia fursa, hata kwa kukiukaKatiba na sheria, kujiandalia na kujihakikishia wapiga kura wa 2015. Ni mkakatisawia na ule ulioasisiwa na Komandoo Salmin Amour Zanziba enzi hizo kuzuiaWazanzibari, wengi wao wakiwa Wapemba, wasipate fursa ya kupiga kura katikachaguzi zilizofuata baada ya ule wa mwaka 1995. Tusishangae iwapo masibu ya Zanzibarya vitambulisho wa ukaazi kuamua nani aruusiwe kujiandikisha kupiga kura au layataamia Tanzania Bara come 2015.
Wadau wafuatao wanapashwa kuchukua hatua stahiki, ikiwezekana hata kupelekapublic litigation Mahakama Kuu dhidi ya NIDA kukiuka Katiba na Sheria;
- Vyama vya Siasa,
- Asasi za Kiraia,
- Chama cha wanasheria Tanganyika,
- Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora,
- Vyombo vya habari,
Pale ambapo makosa yamekwishafanyika, mchakato urudiwe upya. Lakini paleamabapo mchakato bado haujaanza panatakiwa marakebisho kurudiwa haraka.
Wahenga walisema, Ada yaMja Kunena; tusipoziba ufa tutakuja kujenga ukuta.