Nichague kufanya kazi wapi?

Nichague kufanya kazi wapi?

Kayoka

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2011
Posts
2,366
Reaction score
2,151
Habari Wakuu!
Nafanya kazi international NGO moja huku kanda ya ziwa kwa mkataba wa part time miezi sita sita, nalipwa kwa kila siku ninayofanya kazi, nisipokuwepo kazini silipwi hata kama naumwa au nimefiwa. Nikifanya kazi mfululizo kwa mwezi napata malipo yasiyopungua 1. 4M, mpaka sasa nimetimiza mwaka mmoja kazini ila sioni maendeleo yoyote kazini.

Mapema mwezi huu nikifanya usaili shirika lingine na nimeitwa kuanza kazi (contract ya miezi mitano mitano full time), mshahara kwa mwezi ni laki 8.6 huku nikikatwa NSSF kwenye huo mshahara.

Tupeane ushauri Wakuu, niko dilemma mwenzenu ni maamuzi gani nifanye kati ya kuendelea kufanya kazi kama PART TIME au FULL TIME ?
 
Nenda kwa NGO ya pili hapo mbeleni kuna fursa kama vile. promotion,etc, lakini pia unatunisha mfuko wako wa hifadhi ya jamii, nahis pia watakua na programme ya healthcare, binafsi naona fursa nzuri zaidi kwa hiyo NGO ya pili.
Nawasilisha.
 
Watu wengine unakuta. Majigambo tu hamna lokote eti nalipwa 1.4 na huku lak nane mmh acha kuwarusha wenzio ambap wanatafuta ata kibarua cha lak 3 hawajapata kana vipi una ndugu zako kibao ebu kaa nao chini mshauriane kabla ujawarusha roho wenzip
 
Nenda kwa NGO ya pili hapo mbeleni kuna fursa kama vile. promotion,etc, lakini pia unatunisha mfuko wako wa hifadhi ya jamii, nahis pia watakua na programme ya healthcare, binafsi naona fursa nzuri zaidi kwa hiyo NGO ya pili.
Nawasilisha.

Ahsante sana Mkuu kwa ushauri wako.
 
Hii dunia haiko balance imekata chesisi haiwezekani watu wanalia wapewe hata mshahara wa laki halafu kuna MTU anatafuta ushauli aziache million zipi not fair mleta mada hiyo ni kufuru

Hapana Mkuu ni mambo ya kawaida tu, usikate tamaa ipo siku na wewe Mungu atakujaalia fursa kama hii.
 
baki ya kwanza, endelea kutafuta nyingine nzuri zaidi
 
Watu wengine unakuta. Majigambo tu hamna lokote eti nalipwa 1.4 na huku lak nane mmh acha kuwarusha wenzio ambap wanatafuta ata kibarua cha lak 3 hawajapata kana vipi una ndugu zako kibao ebu kaa nao chini mshauriane kabla ujawarusha roho wenzip

Sorry Mkuu kama nimekukwaza, lengo langu si kuwarusha roho job seekers wenzangu ila ni kutaka kupata ushauri tu toka kwao na kwa wadau wengine.

Mungu hawapi ridhiki watu wote kwa kwa wakati mmoja bali huwapa watu wachache kwa wakati tofauti.
 
Nenda kwa NGO ya pili hapo mbeleni kuna fursa kama vile. promotion,etc, lakini pia unatunisha mfuko wako wa hifadhi ya jamii, nahis pia watakua na programme ya healthcare, binafsi naona fursa nzuri zaidi kwa hiyo NGO ya pili.
Nawasilisha.

Mifuko yenyewe huchukui hela mpaka ufike miaka 60!!!

Part time - 1,400,000
Full time - 860,000 (ukiweka makato itakuwa chini ya hapa)

Unataka siku unazo umwa ulipwe kivipi? Baki hapohapo ulipo Huku ukiendelea kutafuta mchongo mzuri zaidi, huo uliopata sioni Kama unazidi wa sasa kiivyo
 
Mifuko yenyewe huchukui hela mpaka ufike miaka 60!!!

Part time - 1,400,000
Full time - 860,000 (ukiweka makato itakuwa chini ya hapa)

Unataka siku unazo umwa ulipwe kivipi? Baki hapohapo ulipo Huku ukiendelea kutafuta mchongo mzuri zaidi, huo uliopata sioni Kama unazidi wa sasa kiivyo

Ahsante Mkuu kwa ushauri wako!
Ninaamini kuwa wadau wengi humu mnaweza kuwa na ushauri wa maana kuliko hata vile ninavyofikiria.
 
Nenda kwa NGO ya pili hapo mbeleni kuna fursa kama vile. promotion,etc, lakini pia unatunisha mfuko wako wa hifadhi ya jamii, nahis pia watakua na programme ya healthcare, binafsi naona fursa nzuri zaidi kwa hiyo NGO ya pili.
Nawasilisha.
Zingine ndoto tu acha kutishika na simba wa kuchora mkuu. We uliziona hizo milioni?
 
Nenda hiyo mpya,kwa sababu kuna angalau job security.ya kesho huyajui
 
Back
Top Bottom