Nianzie wapi mafao NSSF?

Kwa kuongezea hapo ni kwamba navyo jua mimi ni kwamba ukiwa unachangia kwa hiari utaendelea kufanya hivyo ili kuendelea kuweka akiba yako iweze kuja kukusaidia hapo baadae
 
Asante
 
Mku cheti za utumishi unamaanisha certificate of service ambacho alinipa mwajiri sio au
 

Subiri ufikishe miaka 60 ndio udai mafao yako ya uzeeni.
 
Subiri miaka yako igote 55. Vinginevyo wahi NSSF ukadai fao la kukosa ajira upewe hela ya fegi kila mwezi baada ya miezi 6 tangu umefukuzwa
 
Subiri miaka yako igote 55. Vinginevyo wahi NSSF ukadai fao la kukosa ajira upewe hela ya fegi kila mwezi baada ya miezi 6 tangu umefukuzwa
Pesa inatoka ukiwa umefukuzwa pekee au hata kama mkataba umeisha??
 
kwani lile swala la mpaka baada ya miaka 60 ilishafutwa?? kumbe now fao la kujitoa limerejea au sijaelewa
 
Hao ndugu wanaboa sana kimsingi , na wamesahau kama na wao ni astaafu watarajiwa, nchi imeharibika hela za wastaafu zimeporwa na serikali kiufupi mifuko haina hela na ndiomaana wanawaletea mizengwe wazee wa watu, kipindi hiki cha miaka mitano iliyopita na inayokuja watumishi wa umma na wastaafu watapata tabu sana, hali ni tete ni Mungu tu aingilie kati watu wana vielelezo vyote lakini wanazungushwa sana kuna mmoja mpaka anaulizwa vyeti kama alisoma na amestaafu miaka minne iliyopita sasa haya kama sio makusudi ili adhulumiwe ni nini? Nchi imeharibika kuna kitabaka kidogo sana cha watu ndio wanafaidi lakini waliobaki maumivu tu
 
Cheti cha utumishi sio lazima, hapo kiondoe.
Vinavyohitajiwa kwa ulazima:-
Barua ya mwisho wa mkataba
Kitambulisho cha NSSF.
Picha tatu za rangi.
Bank Statement.
Pamoja Nakala ya kitambulisho cha mpigakura/NIDA.
Hapo Kwenye NIDA, vipi kama una namba tu, id bado?
 
Nashukuru Sana waungwana nimepata picha sasa naanza mchakato nitaleta mrejesho kadri itakavyowezekana
 
kwani lile swala la mpaka baada ya miaka 60 ilishafutwa?? kumbe now fao la kujitoa limerejea au sijaelewa
Sasa hivi kuna FAO LA kutokuwa na ajira kwa wale ambao kazi zao ni za kitaaluma kama mhandisi, daktari, mhasibu n.k, Vilevile FAO LA kujitoa bado linaendelea kwa wale ambao kazi zao sio za kitaaluma, let say vibarua katika viwanda, miradi ya ujenzi na n.k
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…