NiagizeDar (Testing Mode) *149*46*14#

mzizi1

JF-Expert Member
Oct 9, 2017
255
691
Mfumo umefungwa kwa sasa

Habari wakuu, nawakaribisha katika mfumo huu mpya wa kidigitali kwa ajili ya majaribio *149*46*14# Buree kwa watumiaji wa Vodacom, Tigo na Airtel
View attachment 2611511

Nunua Bidhaa kupitia Instagram, Facebook, WhatsApp nk, kisha tuagize sisi kwenda kuhakikisha bidhaa yako na kuisafirisha

NiagizeDar
Ni mfumo wa kisasa unaolenga kupunguza gharama za watu walioko Mikoani kuagiza bidhaa Dar.

Kwa kutumia mfumo huu tunao mawakala wa kuaminika waliopo wilaya nne za jiji la Dar (ilala, ubungo,kinondoni na Temeke). Ambao utawatumia kwenda kukuhakikishia mzigo wako au bidhaa yako ulionunua na watahusika kuisafirisha kutoka Dar kwenda mkoani au popote ulipo kwa uamini mkubwa.

Faida kubwa ni kwamba tutapunguza kutapeliwa au kubadirishiwa bidhaa. Na pia kutengeneza fursa za ajira kwa vijana waliopo Dar

Hatua za kufuata ili kuagiza nasi
1.
Piga *149*46*14# kisha
2. Chagua aina ya Huduma: kama ni muuzaji ( kwa ajili ya kutuma mzigo) au Mnunuzi (Kwa ajili ya kuagiza Bidhaa)

3. Ingiza Eneo/wilaya ya Bidhaa ulionunua ( kama ni Ubungo, kinondoni, Temeke na Ilala )

4. Ingiza namba ya Muuzaji (
namba hii ni ya muuzaji ulonunua bidhaa kwake, itatumika kwa ajili ya kwenda kuhakiki bidhaa)

Mfumo utaweza kukuunganisha na Wakala wetu ambae atafuatilia uhakiki wa mzigo wako na ukiridhika basi tutafanya utaratibu wa kuusafirisha na kuhakikisha unakufikia kwa usalama kabisa

Karibu kwa majaribio na ushauri piah
 
Habari wakuu, nawakaribisha katika mfumo huu mpya wa kidigitali kwa ajili ya majaribio *149*46*14# Buree kwa watumiaji wa Vodacom, Tigo na Airtel
View attachment 2611511

Nunua Bidhaa kupitia Instagram, Facebook, WhatsApp nk, kisha tuagize sisi kwenda kuhakikisha bidhaa yako na kuisafirisha

NiagizeDar
Ni mfumo wa kisasa unaolenga kupunguza gharama za watu walioko Mikoani kuagiza bidhaa Dar.

Kwa kutumia mfumo huu tunao mawakala wa kuaminika waliopo wilaya nne za jiji la Dar (ilala, ubungo,kinondoni na Temeke). Ambao utawatumia kwenda kukuhakikishia mzigo wako au bidhaa yako ulionunua na watahusika kuisafirisha kutoka Dar kwenda mkoani au popote ulipo kwa uamini mkubwa.

Faida kubwa ni kwamba tutapunguza kutapeliwa au kubadirishiwa bidhaa. Na pia kutengeneza fursa za ajira kwa vijana waliopo Dar

Hatua za kufuata ili kuagiza nasi
1.
Piga *149*46*14# kisha
2. Chagua aina ya Huduma: kama ni muuzaji ( kwa ajili ya kutuma mzigo) au Mnunuzi (Kwa ajili ya kuagiza Bidhaa)

3. Ingiza Eneo/wilaya ya Bidhaa ulionunua ( kama ni Ubungo, kinondoni, Temeke na Ilala )

4. Ingiza namba ya Muuzaji (
namba hii ni ya muuzaji ulonunua bidhaa kwake, itatumika kwa ajili ya kwenda kuhakiki bidhaa)

Mfumo utaweza kukuunganisha na Wakala wetu ambae atafuatilia uhakiki wa mzigo wako na ukiridhika basi tutafanya utaratibu wa kuusafirisha na kuhakikisha unakufikia kwa usalama kabisa

Karibu kwa majaribio na ushauri piah
Nzuri sana ila naomba unihakikishie usalama wa mali yangu .

Gharama zenu , siku ngapi mzigo kufika ? Je mnaweza kunieleza ikiwa sitapata mzigo wangu kwa wakati tuliokubaliana mtanilipa au hapana ?
 
Na mambo yakienda ndivyo sivyo nawawajibisha vp?

Tararibu zenu zinasemaje?
Tumejidhatiti na yote mkuu kuhakikisha mzigo wako unakufikia salama, sisi tunakuhakikishia wewe uliopo mbali na dar uweze kupata mzigo wako kama ulivyoagiza, kuokoa gharama za wizi utapeli nk
 
Nzuri sana ila naomba unihakikishie usalama wa mali yangu .

Gharama zenu , siku ngapi mzigo kufika ? Je mnaweza kunieleza ikiwa sitapata mzigo wangu kwa wakati tuliokubaliana mtanilipa au hapana ?
Shukran, sisi hatuna bidhaa hata moja, wewe utapatana na wauzaji, kisha utatuachia sisi jukumu la kwenda kuhakikisha mzigo wako kama ni sahihi na kwa uharaka zaidi tutakufikishia popote ulipo ndani ya dar au nje ya jiji. Hatuna gharama yoyote inayoongezeka kwako mkuu. Ni gharama zilezile za kutuma mzigo mkoani, tukiufikisha kwenye basi husika basi details na saa ya basi kuondoka zote utazipata kupitia mfumo. Hatujapanga kumpotezea muda mteja kwa kuchelewesha mzigo wake. Endapo litatokea hili gharama za kutuma mzigo zitarudishwa
 
Inaweza kua nzuri. Sijajua gharama za commission yenu
Hatuna plan za kuongeza gharama kwa mteja, kama mzigo huwa unatuma kwa 5k, basi pia sisi tutatuma kwa gharama iyoiyo. Lengo ni kuongeza uaminifu kupunguza utapeli na kuokoa gharama
 
Hatuna plan za kuongeza gharama kwa mteja, kama mzigo huwa unatuma kwa 5k, basi pia sisi tutatuma kwa gharama iyoiyo. Lengo ni kuongeza uaminifu kupunguza utapeli na kuokoa gharama
Hongera kwa kutoka kua pipe had platform
Swali langu ni je Ikitokea mzgo wangu haujafika, malalamiko yangu yanasikilizwa na nani?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom