Niache kula kuku Sea Cliff kisa kupeleka watoto English Medium?

Mtoa mada unapoint. Me binafsi nmesoma shule za serikali toka primary hadi chuo kikuu.
Nilivokuwa sekondari mlezi wangu alikua ananipa vitabu vyote vya kujisomea kuanzia english mpaka science. Leo nikiongea ngeli unaweza fikiri nilisoma hizo international schools coz i was shaped to be like this. Nawe unaweza msimamia mwanao kwenye shule za serikali akawa msomi mzuri tu.
 
Naungana na wew kwa jambo moja tu, badala la kutumia fedha nying kuwasomesha ni vyema ukawaandalia assets zao za badae huku wakiendelea na shule za kawaida kwa kuwasisitiza kusoma na kuwafuatilia.
Ila hilo swala la kula bata ili usiwapeleke watoto shule sio jambo zuri hata kidogo!!
CR7 ana uwezo wa kuwasomesha watoto wake na akawapa chochote wanachotaka!.
N.B.kila mmoja afanye kitu kulingana na uwezo wake.
 
Mi wanangu watasoma tu huko kwenye kingereza,mama yao nimesoma kayumba,kidumu na mfagio,kutembea kwa mguu mpaka shule,darasani tunajaa 120 na mwalim wa 121,tunabanana na kupumuliana,mwalimu asipokuja darasani ni shangwe....

Akhaaa mwenzangu,watasoma shule nzuri,walimu wa kutosha ns shule wanaenda kwa gari akirudi nyumban ananifundisha na mimi kingereza,uhakika wa kufaulu ni 90% basi hela yangu inakua imeenda kihalali,
 
Amesema lini anatamani? Maana Ronaldo yuko bize na mtoto wake uwanja wa mazoezi.

PhD bila hela ni ujinga tu, tena hizi za wabongo ndo zero kabisa
 
Hujaachaga tu mkuu
 
Nadhani una miaka 18 haya unayoongele Bado hujafikia yani hujui unachokiongea
Nilipokuwa na miaka kama yako nilidhani najua kila kitu
Lakini kadiri miaka ilivyokwenda nilizidi kujua mambo mengi ambayo sikuwa nikiyajua ndio nikagundua kuwa wazee ni watu muhimu sana
Wanajua mengi nawaheshimu sana
Lakini pia usijali ukikuwa!!! Utaacha!!
 
Nilikutana na mtoto wa kishua chuo kimoja hapa Tz cha government aliyesoma kuanzia kind gate mpaka kidato cha 6 aseee na ile hali ya ma lecturer kutujazia notes kibao za kusoma mara individual/group presentations haziish bas ilifikia hatua analia tu nikamuuliza kulikon akajibu hajazoea usomaj wa hivyo na hapo nikapata jibu kuwa sometimes shule hizi za gharama kwa mtoto mwanzo mwenga zinawapunguzia watoto kuumiza akili
 
Amesema lini anatamani? Maana Ronaldo yuko bize na mtoto wake uwanja wa mazoezi.

PhD bila hela ni ujinga tu, tena hizi za wabongo ndo zero kabisa
Kukurupa si jambo jema wala usitake kuonekana ni mpinzani. Tumia busara na hoja zenye maana kamili.
 
Mimi nimesoma shule za serikali,,, na watoto wngu watasoma shule za serikali..watakutana CHUO NA HAO wa TABLE UNDER THE CHAIR....muhimu ni kupata elimu ya MSINGI..SECONDARY NA CHUO..na KUWAWEKEA MKAZO KTK TUITION basi..hakuna namna...now najikita na kuwekeza kwny ARDHI...wakikuwa watakutana nazo...
 
Kwani ukiwaandalia elimu nzuri Ardhi watashindwa kujinunulia? Tatizo tuseme ukweli kwamba maisha magumu tusitoe reference za uongo, kila MTU anapenda mtoto wake asome shule nzuri na aishi vizuri sema tu mambo yanatubana
 
Kwani ukiwaandalia elimu nzuri Ardhi watashindwa kujinunulia? Tatizo tuseme ukweli kwamba maisha magumu tusitoe reference za uongo, kila MTU anapenda mtoto wake asome shule nzuri na aishi vizuri sema tu mambo yanatubana
hivi kwani unahisi KUMPELEKA MTOTO ENGLISH MEDIUM ni UWEZO?kuna watu wana UWEZO na watoto wao wapo shule za kawaida na wapo ambao wanasomesha huko wanatusumbuwa sisi DAILY...WENGI WENU NI FASSION TU,,,na KUJUWA English.... Watakutana CHUO...Mimi nawawekea ASSETS...wakikuwa WAPATE PA KUANZIA...
 
mwambie mkeo na wanao.....matatizo na raha zako hazituhusu sisi na familia zetu...!!!
 
Na maprofesa wanatamani wawe diamond
Always unatamani usichokua nacho ,its human nature
 
Hahhaaahah! Chizi kalogwa tena!


Elimu ni mtu mwenyewe.

Watu wamesoma International Schools na bado tunawapeleka huku kitaa katika Nyanja zote za maisha.

Sio kingereza, sio pesa, sio kuzurura duniani. Sio kufaulu, Sio uwezo wa kuchambua mambo.

Kiufupi Elimu ni mtu mwenyewe. Kama vile yalivyo maisha. Maisha ni mtu mwenyewe.

Kumsomesha mtoto sijui medium sijui Kata sio Guarantee ya yeye kuwa na elimu bora. Mtu anaweza kuwa shule bora lakini asipate elimu bora.

Muhimu, Kila mtu ampeleke mtoto wake kwenye shule ambayo anauwezo nayo.

Ujinga na upumbavu ni pale huna uwezo alafu unapeleka mtoto kwenye shule zenye gharama kubwa. Hapa ndio wale wazazi wanalalamika kwa kitu kidogo mtoto anapokosea. Mara sijui nimechoma ada yangu. Na blah bla zingine.

Ujinga na upumbavu ni pale unamsomesha mtoto shule ya kata wakati unauwezo wa kumsomesha shule nzuri zaidi.

Ni hayo tuu
 
unawaza ada mil 2 kwa Mwaka?hiyo ni hela Ya bia, Kula ,petrol na kutombea kwa wiki, tafuta hela usomeshe watoto pimbi wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…