Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Nchi ya India kwa siku takribani 4 imekubwa na joto kali la maandamano yaliyochochewa na mwanaharakati na mpigania haki Anna Hazare. Mzee huyu mwenye umri wa miaka 74 alikamatwa na polisi wa India baada ya kuanza mgomo wa kutokula kuishinikisha serikali ya india ya india kufanya marekebisho katika muswaada wa kupambana na rushwa. Baadae alikamatwa na kuwekwa korokoroni halii iliyochochea maandamano katika miji kadhaa kama Mumbai, Chennai, Bangalore, Calcutta na miji mingine.
Waandamanaji kwa maelfu walikusanyika nje ya kituo cha polisi alichoshikiliwa Hazare na yeye alishikilia mgomo wa kutokula hadi hapo serikali itakapoufanyia marekebisho muswaada huo. Polisi wamekubali kumtoa kizuizini mwanaharakati huyo kwa sharti kwamba mgomo wake wa kutokula kwa siku 15 akaufanyie katika bustani Ramlila mjini humo.
Waziri mkuu wa India Manmohan Singh amemshutumu Hazare kwa kusababisha vurugu. Mwezi wa Aprili mwaka huu Hazare aliingia tena kwenye mtifuano na serikali ya Indian alipoishinikiza serikali kuandaa muswaada wa sheria itakayoruhusu maofisa wote wa serikali wanaotuhumiwa kwa rushwa kuchunguzwa na kushitakiwa endapo watabainika kushiriki katika kutoa au kupokea mirungula. Na ndio juzi mzee huyo alipoingia tena matatani pale alipogundua kuwa muswaada huo wa sheria unawaepusha viongozi wa juu wa serikali kuhojiwa na kushitakiwa endapo watakutwa na tuhuma za rushwa akiwemo waziri mkuu.
My TAKE: Msimamo wa Hazare kwa ukweli kabisa umenifanya nione kuwa Tanzania kwa hali ilivyo sasa tunahitaji watu wa aina yake watakaotoa shinikizo kwa serikali legelege hii na sisi wananchi tuungane nao. Tuhuma za rushwa na ufisadi zinazowakabili viongozi kibao katika ngazi mbali mbali zinaimaliza nchi na serikali ipo tu inachapa usingizi.....Mbaya kabisa!!
Waandamanaji kwa maelfu walikusanyika nje ya kituo cha polisi alichoshikiliwa Hazare na yeye alishikilia mgomo wa kutokula hadi hapo serikali itakapoufanyia marekebisho muswaada huo. Polisi wamekubali kumtoa kizuizini mwanaharakati huyo kwa sharti kwamba mgomo wake wa kutokula kwa siku 15 akaufanyie katika bustani Ramlila mjini humo.
Waziri mkuu wa India Manmohan Singh amemshutumu Hazare kwa kusababisha vurugu. Mwezi wa Aprili mwaka huu Hazare aliingia tena kwenye mtifuano na serikali ya Indian alipoishinikiza serikali kuandaa muswaada wa sheria itakayoruhusu maofisa wote wa serikali wanaotuhumiwa kwa rushwa kuchunguzwa na kushitakiwa endapo watabainika kushiriki katika kutoa au kupokea mirungula. Na ndio juzi mzee huyo alipoingia tena matatani pale alipogundua kuwa muswaada huo wa sheria unawaepusha viongozi wa juu wa serikali kuhojiwa na kushitakiwa endapo watakutwa na tuhuma za rushwa akiwemo waziri mkuu.
My TAKE: Msimamo wa Hazare kwa ukweli kabisa umenifanya nione kuwa Tanzania kwa hali ilivyo sasa tunahitaji watu wa aina yake watakaotoa shinikizo kwa serikali legelege hii na sisi wananchi tuungane nao. Tuhuma za rushwa na ufisadi zinazowakabili viongozi kibao katika ngazi mbali mbali zinaimaliza nchi na serikali ipo tu inachapa usingizi.....Mbaya kabisa!!