Ni wakati muafaka sasa Polisi waratibiwe na kusimamiwa kazi zao

El Roi

JF-Expert Member
May 29, 2020
263
502
Mnamo mwaka 2011 nchini Kenya, ilipitishwa Sheria ya bunge iliyounda chombo au wakala wa kusimamia na kiratibu utendaji wa kazi wa Jeshi la polisi, INDEPENDENT POLICING OVERSIGHT AUTHORITY. (IPOA)

Na masukumo mkubwa wa kuanzisha chombo hiki ulitokana na historia ya muda mrefu ya kutaka kubadili dhana ya upolisi iliyokuwepo ya utumiaji wa nguvu zisizo na kiasi( unreasonable force), jeshi kujihusisha na uingiliaji wa mambo ya Kisiasa( political interference, na ukiukaji ulokuwa umekithiri wa haki za binadamu(wide spread violations of human rights).

Ndiposa kianzishwa chombo au wakala huo. Kazi zake pamoja na majukumu yake yaliyopelekea kupitishwa kwa wakala huu ni pamoja na:

1)kuchunguza vifo na majeraha makubwa yalosababoshwa na matendo ya polisi
( To investigate deaths and serious injuries caused by police actions.)

2)kuchunguza mwenendo mbaya wa polisi ( To invistigate police misconduct)

3)kusimamia, kufanya rejea na kukagua uchunguzi na matendo yanayofanywa na unit inayosimamia utendaji wa kila siku wa polisi ( To monitor, review and audit investigations and actions by the internal affairs unit of the police)

4) kufanya ukaguzi wa makazi na maeneo ya polisi (To conduct the inspection of police premises).


Kama nilivyoanza kusema au kuandika hapo juu huu ndo wakati muafaka nionao was sisi pia kuwa na chombo hiki.

Chombo hiki ni Cha kiraia na kinaundwa hasa na raia wenye taaluma tofauti ingawa pia uhusisha polisi wastaafu kama sehemu ya makamishina kwa ajili ya kutoa hints za kitaalamu ba hasa za upolisi wenyewe.

Kwa mtazamo was wengi, na ndivyo ilivyo, polisi wetu hapa wana madaraka yaliyopindukia na hawana usimamizi wowote wa Kila siku wa kazi zao.

Polisi wanakamata( arrest) wanapeleleza( investigation) na sehemu kubwa wao bado ndo waendesha mashitaka( prosecution)

Hivi hapa kweli kutakuwa na haki inayopaswa kutolewa?

Hapa jamvini kumejaa malalamiko ya watu juu ya vitendo mbalimbali vinavyoendelea ndani ya jeshi letu. Hivi wao wanawajibika Kwa nani wakati wanapofanya mambo yaliyo kinyume na kazi zao?

Ninajua Kuna mamlaka zao za nidhamu ktk majukumu yao lakini nani anamwajibisha nani wakati kazi na pengine hata hulka zao zimeshafanana kwa sababu ya nature ya kazi zao?

Nimeona juzi msajili wa vyama vya siasa akiomba kukutana na wakuu wa jeshi la polisi bila shaka kurekebisha( to regulate) yanayoendelea Sasa ambapo polisi wanavamia na kutawanya vikao vya ndani vya vyama jambo ambalo hawana jurisdiction ya kulifanya..

Sijui, kama nikisoma katikati ya mistari polisi wanaweza wasimsilize maana yeye hahusiku nao kisheria tena Wana uwezo hata wa kumkamata yeye kwenye kikao hicho wakitaka maana wao ndo kila kitu . Vipi kungekuwa na over sighting body huoni wangejua kwamba Wana mahali wanapowajika na kuchukuliwa hatua? There is no authority not under another authority"..

Haya mauaji yanayosababishwa na polisi, wanachunguza wenyewe, wanapeleleza wenyewe na kushitaki wao, KESI ya nyani unampa nyani mwenziwe,mwenye mahindi atapata haki yake?

Kuchunguza mienendo mibaya ya polisi. Nani amchunguze mwenzake na kweli hatua zichukuliwe? Ndiyo wanaweza kulindana wao ndani kwa ndani lakini ulinzi wa kweli uko nje.

Malalamiko ya wananchi juu ya mienendo na tabia mbaya za polisi yalipaswa yapelekwe siyo kwa OCD au hata RPC bali chombo huru ambacho polisi wanawajibika kwacho. Kulindana na kukingiana kifua ni kwingi kwa sababu kazi Yao ni moja na wakati mwingi wanafahamiana
Je unategemea nini hapo?

Nani anafuatilia utendaji wa kila siku wa central unit ya Polisi?
Ni kweli IGP abawajibika kwa waziri na kwa Rais. Lakini je nani anakutana naye mara kwa mara kumuhoji na hata kumuonyesha yeye na makamanda wake mahali wanapoacha taaluma Yao, unyanyanyasaji nk.
Waziri ni mwanasiasa, wakati mwingine unyanyasaji wa haki A watu na hasa za kisiasa no mtaji kwake . Nani atamwambia yeye na timu yake kwamba" you have gone beyond boundaries"na akaogopa?

Nawashauri serikali katika wimbi hili ambako polisi wanalaumiwa kila mahali na vilio ni vingi juu ya kukiukwa Kwa haki za binadamu na manyanyaso yanayodaiwa kutendwa na polisi, ni wakati sahihi sasa iwepo mamlaka ya kiraia kama ilivyo IPOA Kenya itajayosimamia haki za raia wenzao. Kuwaacha polisi watambe na kwa sababu ni chombo cha nguvu chenye madaraka makubwa ni kuwaumiza raia wa nchi husika na mwisho wa siku wataichukia serikali.

Mara zote husema madaraka yasiyodhibitiwa huharibu kabisa" absolute power corrupts absolutely" polisi wetu Wana absolute power wadhibitiwe.

Leo nimesikia kutupwa kwa KESI ya mbowe ambayo pamoja na mambo mengine alikuwa analakamika juu ya kukamatwa kwake kwamba haki zake zilikiukwa. Ukiacha technicalities na mambo ya mahakama, chombo kinachoaimamia polisi kama IPOA, kingepokea makakamiko hayo na kumwita IGP au afisa mhusika wa polisi kujibu maswali kama;.

Kwa nini kiongozi was hadhi ya mbowe anavamiwa na kukamatwa kama jambazi? Of course angeambiwa hiyo siyo professionalism

Kwa Nini kumfunga mtu kitambaa toka mwanza mpaka Dar! ( Kama ni kweli maana mambo mengine nasi tunayasoma tu) ? Wangefanya uchunguzi na hata kuwawajibisha polisi waliofanya hivyo, kupendekeza kuwashusha vyeo nk ingebidi.

Mahakama haiwezi ona mambo ya nature hiyo kabisa.

Ni wakati sasa tuwe na chombo kinacholeta checks and balances kati ya polisi na jamii na hasa kuwafanya polisi wawe disciplined na wawe na hofu Kwa maana ya reverence wanapotekeleza majukumu yao.

Hata hivyo bado tunawahitaji polisi na Jeshi lao maana ni watu wa muhimu kuwa nao.

Wasalaam
 
Umeelezea mengi ila kwa kifupi nchi yetu tunahitaji IPID hawa ni polisi na sio raia na kazi yao ni kuchunguza na ku arrest member wa police aliyefanya kosa na pia kesi zote zinazohusisha police wao ndio jukumu lao kusimamia kesi za namna hii,mfano kesi ya Hamza (rip)polisi walikua ni suspects means hawakusitahili kujichunguza na kujitolea uamuzi na kujipa nishani za ushujaa!
 
Polisi kufanya watakavyo ni sababu ya kuwa na katiba inayotoa mamlaka ya rais kuwa juu ya sheria, na wakati huo huo jeshi la polisi kuwajibika kwa rais. Na kwa namna muundo wa nchi yetu ulivyo, ccm ndio wanaweza kukaa madarakani bila kujali maamuzi ya kura za wananchi. Kadiri ccm inavyozidi kupoteza ushawishi kwa umma, ndio rais anavyozidi kulitumia jeshi la polisi kufanya atakavyo. Kwa sasa imefikia mahali Rais na chama chake hawana uwezo tena wa kushinda uchaguzi bila nguvu ya jeshi la polisi. Matokea yake rais hadhubutu kuwahoji tena hata wakikosea na kuwachukulia hatua, maana polisi ndio hasa waliomuweka madarakani na chama chake.

Hali hii ya polisi kufanya watakalo ni matokeo ya serekali iliyoko madarakani kuingia kwa nguvu ya vyombo vya dola, huku polisi wakiwa mstari wa mbele kabisa kwenye uovu huo. Na serikali iliyopo haithububutu kufanya mabadiliko yoyote ya kulifanya jeshi hilo lifanye kwa weledi, maana chama kilicho madarakani sasa, kitakuwa muhanga wa mabadiliko hayo. Kinachofanyika kwa sasa baina ya serikali iliyoko madarakani na jeshi la polisi, ni unilinde kwa jua, nami nikulinde kwa mvua. Hivyo usitegemee serikali iliyopo madarakani ikemee uovu wa polisi, maana hata yenyewe inategemea uovu wa jeshi la polisi kukaa madarakani.
 
Vicious cycle
Polisi kufanya watakavyo ni sababu ya kuwa na katiba inayotoa mamlaka ya rais kuwa juu ya sheria, na wakati huo huo jeshi la polisi kuwajibika kwa rais. Na kwa namna muundo wa nchi yetu ulivyo, ccm ndio wanaweza kukaa madarakani bila kujali maamuzi ya kura za wananchi. Kadiri ccm inavyozidi kupoteza ushawishi kwa umma, ndio rais anavyozidi kulitumia jeshi la polisi kufanya atakavyo. Kwa sasa imefikia mahali Rais na chama chake hawana uwezo tena wa kushinda uchaguzi bila nguvu ya jeshi la polisi. Matokea yake rais hadhubutu kuwahoji tena hata wakikosea na kuwachukulia hatua, maana polisi ndio hasa waliomuweka madarakani na chama chake.

Hali hii ya polisi kufanya watakalo ni matokeo ya serekali iliyoko madarakani kuingia kwa nguvu ya vyombo vya dola, huku polisi wakiwa mstari wa mbele kabisa kwenye uovu huo. Na serikali iliyopo haithububutu kufanya mabadiliko yoyote ya kulifanya jeshi hilo lifanye kwa weledi, maana chama kilicho madarakani sasa, kitakuwa muhanga wa mabadiliko hayo. Kinachofanyika kwa sasa baina ya serikali iliyoko madarakani na jeshi la polisi, ni unilinde kwa jua, nami nikulinde kwa mvua. Hivyo usitegemee serikali iliyopo madarakani ikemee uovu wa polisi, maana hata yenyewe inategemea uovu wa jeshi la polisi kukaa madarakani.
 
Kwa nchi yetu itachukua miaka 50 kuja kumiliki chombo cha aina hiyo. Kwa sasa wacha tu waendelee kutumiwa na wanasiasa uchwara wa ccm.
 
Hivi mapolisi Tanzania huwa wanafanyiwa hata psychological evaluation kuwapima kama wako stable kichwani? Unampaje silaha na madaraka makubwa mtu ambaye huna uhakika kama yuko salama kichwani?

Polisi wengi ni ma psychopath wanaosikia raha kuwaumiza raia wasio na hatia.
 
Umeelezea mengi ila kwa kifupi nchi yetu tunahitaji IPID hawa ni polisi na sio raia na kazi yao ni kuchunguza na ku arrest member wa police aliyefanya kosa na pia kesi zote zinazohusisha police wao ndio jukumu lao kusimamia kesi za namna hii,mfano kesi ya Hamza (rip)polisi walikua ni suspects means hawakusitahili kujichunguza na kujitolea uamuzi na kujipa nishani za ushujaa!
Ukinisoma vema nimeeleza tayari. Haiwezekani wajichunguze wao alafu kuwe na equal division of people's rights.
Tunahitaji chombo huru tofauti na wao wenyewe.
 
Hua naumia sana hawa watu kua na uhalali Wa kuitwa jeshi, hawana nidhamu, wanabambikia kesi, wala rushwa, wezi na watesi then tunawaita JESHI, jeshi huwa na nidhamu ningekuwa na uwezo wangeitwa GENGE LA POLISI si jeshi.
 
Mtoa mada, mawazo yako ni ya kujenga sana, lakini usishangae wakapatikana wa kukubeza. Tunao watu wengi, uwezo wao wa kuona, kufikiri na kutafakari unaishia walipokaa au kusimama. Hawajui yaliyompata Mbowe, yanaweza kumpata hata yeye, kama si leo, basi hata miaka 10 ijayo. Tina sheria za ovyo, tina Jeshi la Polisi la hovyo. Ukichanganya yote hayo, tunaishi kwenye hatari kubwa.

Siku moja nilikuwa naongea na Polisi, ambaye aliamini mimi ni rafiki yake, baada ya kumsaidia shilingi laki 2 (sina urafiki na mtu mwovu, hasa anayeonea watu), akaniambia, 'mtu yeyote akikusumbua, niambie. Tunamkamata tunamweka ndani. Akiwa huko, kosa litapatikana tu'. Kisha akasema, hivi unajua nikikukamata hata dola 100, naweza kukufungulia kesi ya utakatishaji fedha? Sheria iliyopo haina kiwango, hata dola 50, unakaa mahabusu hadi unaoza'. Ilinifikirisha sana, na kujiuliza maswali mengi. Nikajilaumu kwa nini nilimpa hata hiyo laki 2.

Watanzania tuungane, tudai katiba nzuri mpya, tudai sheria za ovyo zinazowapa polisi mamlaka ya kupindukia, zifutwe. La sivyo, kila mmoja yupo kwenye hatari ya wakati wowote kutendewa uovu uliobarikiwa na sheria zetu haramu.
 
Back
Top Bottom