Zero One Two
JF-Expert Member
- Sep 16, 2007
- 9,347
- 3,023
Nimeish na mume wangu miaka 11,wote tulikuana hatuna uwezo,tukaanza maisha pamoja,mimi nilikua nimeajiriwa nauza duka na yeye dereva,Badae niliacha kazi kulea mtoto wetu wa kwanza,Yeye aliendelea na kazi na mimi nikaendelea kumshauri afanye maendeleo,tukajenga,tukafungua miradi,Tukanunua gari 3.Badae nikajiajiri kwa kufungua duka letu,Kumbe mwenzangu kazaa nje na kudhamiria kuniacha mimi ili aoe huyo mwanamke wkt kwa sasa tayari nina mtoto mwingine wa miez kadhaa,Alichofanya yeye ili ahakikise sipati kitu ni KUBADILISHA HATI ZA MALI ZETU ZOTE NA KUANDIKA JINA LA MTOTO WANGU MDOGO, je baada ya ndoa kuvunjika nani atasimamia hizo mali ni mimi au yeye? Na je baada ya ndoa kuvunjika, kisheria naruhusiwa kudai kumilikishwa mali kwa jina langu na si la mtoto?NISAIDIENI JAMANI