Naughty by nature
JF-Expert Member
- Jan 22, 2023
- 2,128
- 2,356
Wakuu kuna mwanamke nilizaa nae mwaka 2007, wakati nikiwa na mke wangu, na sikuwai kuishi nae zaidi ya kuwa nilikuwa naenda alikopanga mara moja moja, na mara nyingine akishindwa kodi ya nyumba nilikuwa namlipia, na pia alikuwa na fremu ya biashara, alikua akishindwa kodi namsaidia. Mimi na wife tuna miaka almost 25 ya ndoa, na tuna nyumba nne, kuna nyumba moja ipo maeneo mbezi pia.
Sasa uyo mwanamke wakati najenga ile nyumba ya Mbezi bado nipo kwenye mahusiano nae, sasa kuna wakati kodi ilimshinda na mimi sikuwa vizuri, nilimsaidia akaenda kukaa kwenye nyumba yangu ya Mbezi yeye na mtoto. Baadae nilimpa milioni tatu akaenda kumalizia nyumba yake akahamia kwake, ilishapita miaka sita hatuko pamoja, na mtoto yupo form 2 anakaa nae.
Sasa bwana mwezi uliopita ameenda kushtaki baraza la kata kuwa nyumba niliyojenga Mbezi eti na yeye anahusika, alitoa ushauri kwahiyo na yeye ana fungu lake!
Hivi mwanamke ana akili kweli? Hivi kuna sheria hawara awe na sehemu kwenye mali za wana ndoa?
Sasa uyo mwanamke wakati najenga ile nyumba ya Mbezi bado nipo kwenye mahusiano nae, sasa kuna wakati kodi ilimshinda na mimi sikuwa vizuri, nilimsaidia akaenda kukaa kwenye nyumba yangu ya Mbezi yeye na mtoto. Baadae nilimpa milioni tatu akaenda kumalizia nyumba yake akahamia kwake, ilishapita miaka sita hatuko pamoja, na mtoto yupo form 2 anakaa nae.
Sasa bwana mwezi uliopita ameenda kushtaki baraza la kata kuwa nyumba niliyojenga Mbezi eti na yeye anahusika, alitoa ushauri kwahiyo na yeye ana fungu lake!
Hivi mwanamke ana akili kweli? Hivi kuna sheria hawara awe na sehemu kwenye mali za wana ndoa?