Ni utamaduni/utaratibu gani mpya uliowahi kukutana nao katika maisha yako?

Daby

JF-Expert Member
Oct 26, 2014
33,648
75,732
Iwe ndani ya nchi yako au nje naamini ulishawahi kukutana na utaratibu au utamaduni mpya ambao haujawahi kufikiria kama upo duniani. Tupeane uzoefu inaweza kuwa msaada kwa mtu atakayekutana na hilo kwa mara ya kwanza.

Moja, Hapa Tanzania mkoani Arusha kuna kabla linaitwa wasonjo/watemi lipo ngorongoro karibia na kenya. Katika kuzungukazunguka nikawakuta hawa watu bwana. Wanasherehe zao za kuimba, sasa utakuta wanaume wanaanza kuingia uwanjani wakiimba kwa mistari/raws baada ya muda wanawake nao wanaingia.

Kila mwanamke hapo anajichagulia mwanaume wa kuimba naye. Na mwanamke unapoingia kuimba na mwanaume ni sharti matiti na kifua chote kiwe wazi bila kujali kuna kaka au baba yako. Ni lazima na hakuna cha kupinga. Nilishangaa saana kuona chuchu saa sita. Huu utamaduni ulinishangaza saana ila pia niliupenda.


Sikubahatika kupiga picha maana niliambiwa ukionekana unachezea. Ila mfano wa utaratibu wa uimbaji huu hapa nimezikuta mtandaoni japo hawapo vifua wazi.
45aeb66900b55e8e6f3c6d07a0b16faa.jpg
691fad3a3c36700102d5fea28d55912f.jpg


Share utamaduni/utaratibu uliyowahi kukutana nao iwe nje ya nchi au ndani ya nchi.
 
Hakuna siasa, Ningekuwa na uwezo ningemfuta huyo mdau ila huo utamaduni kwa mara ya kwanza kuusikia na kuuona ni siku hiyo. Ningekuwa na picha nyingine ningeiweka kufuta siasa jamaa wasijewakahamia kwenye uzi huu na kupoteza ladha ya uzi.
Teh haya bwana.

Ila hilo kabla lilinishangaza saana. Na hawaoni kama kinyume na maadili kama tulivyozoea kwa dada zetu wa mjini.

Kule mdada akivua nguo na kuimba na mwanaume ndiyo heshima yenyewe.
 
kuna huu utamaduni niliusikia nadhani utakua ukouko kwa wamasai
mwanaume kama umeoa kasichana kako kazuri siku ukitoka kuchunga mifugo yako na ukarudi nyumbani ukapepesa macho ukiona mkuki umechomekwa ardhini na nyumba imefungwa basi ujue mke wako anagegedwa ndani uko
na hakuna kupanic hapo ndo utamaduni huyo, hapo wewe unatulia pembeni huku unamsikiliza mke wako akilia kwa key za vinanda na marimba
mchezo ukiisha unaingia ndani kinyoonge!
 
Wasukuma,mwanamke lazima apige goti wakati wa kusalimia hata kama ni barabarani. Akitumwa maji akileta anapiga goti mpaka anayekunywa maji amalize kunywa na kumpa kikombe au kata ndio anaruhusiwa kusimama na kuondoka.

Wakati wa kula wanawake na watoto wanakaa sehemu yao na wanaume sehemu yao hakuna kuchanganyika.
 
Teh haya bwana.

Ila hilo kabla lilinishangaza saana. Na hawaoni kama kinyume na maadili kama tulivyozoea kwa dada zetu wa mjini.

Kule mdada akivua nguo na kuimba na mwanaume ndiyo heshima yenyewe.
Hao jamaa hatari, wakifanya hayo mazoezi kagiza kakiwa kanaingiaingia sioni kama kunakuwa na usalama wa kihisia hapo...
 
kuna huu utamaduni niliusikia nadhani utakua ukouko kwa wamasai
mwanaume kama umeoa kasichana kako kazuri siku ukitoka kuchunga mifugo yako na ukarudi nyumbani ukapepesa macho ukiona mkuki umechomekwa ardhini na nyumba imefungwa basi ujue mke wako anagegedwa ndani uko
na hakuna kupanic hapo ndo utamaduni huyo, hapo wewe unatulia pembeni huku unamsikiliza mke wako akilia kwa key za vinanda na marimba
mchezo ukiisha unaingia ndani kinyoonge!
Mkuu mimi nimetokea kwenye hii jamii ila mwenyewe nimekuta stori tu kama wewe ulivyoziskia sijawahi kuona na nimeishi pia umasaini.

Labda waliowahi kuona watathibitisha hili.
 
Wasukuma,mwanamke lazima apige goti wakati wa kusalimia hata kama ni barabarani. Akitumwa maji akileta anapiga goti mpaka anayekunywa maji amalize kunywa na kumpa kikombe au kata ndio anaruhusiwa kusimama na kuondoka.

Wakati wa kula wanawake na watoto wanakaa sehemu yao na wanaume sehemu yao hakuna kuchanganyika.
Aseeh. Interesting.

Hadi sasa hivi au umeisha
 
Wasukuma,mwanamke lazima apige goti wakati wa kusalimia hata kama ni barabarani. Akitumwa maji akileta anapiga goti mpaka anayekunywa maji amalize kunywa na kumpa kikombe au kata ndio anaruhusiwa kusimama na kuondoka.

Wakati wa kula wanawake na watoto wanakaa sehemu yao na wanaume sehemu yao hakuna kuchanganyika.

ii numbisa kule kwetu lazima ufanye ivo,utawezaa!?
 
kuna huu utamaduni niliusikia nadhani utakua ukouko kwa wamasai
mwanaume kama umeoa kasichana kako kazuri siku ukitoka kuchunga mifugo yako na ukarudi nyumbani ukapepesa macho ukiona mkuki umechomekwa ardhini na nyumba imefungwa basi ujue mke wako anagegedwa ndani uko
na hakuna kupanic hapo ndo utamaduni huyo, hapo wewe unatulia pembeni huku unamsikiliza mke wako akilia kwa key za vinanda na marimba
mchezo ukiisha unaingia ndani kinyoonge!
Hapana nawewe unaenda kwa mke wa huyo jamaa
 
Kwa mjini hali imepungua wameelimika ila vijijini hali mbaya.

Mwanamke akimtengea chakula mwanaume\wanaume huku anacheka jamaa (w)anakizira chakula ati kina nuksi hivyo kinapikwa kingine
Aseeh. Interesting.

Hadi sasa hivi au umeisha
 
Hata masai wa Ngorongoro hasa kule Nainokanoka,Bulati,Kapenjiro,Olbalbal na Piaya Pinyinyi kipelekewa mahindi na serikali ni utamaduni mpya sana kwangu ulikua.
 
Kwa mjini hali imepungua wameelimika ila vijijini hali mbaya.

Mwanamke akimtengea chakula mwanaume\wanaume huku anacheka jamaa (w)anakizira chakula ati kina nuksi hivyo kinapikwa kingine
Hivi ni halali kusema kufuata hizo mila ni kutokuelimika?

Kwangu naona kama tunadharau mila mila zetu na tulikotoka kwa ujumla.

Hata maasai mwanamke ni mwiko kula sehemu moja na Morani hadi leo ipo hii.
 
kuna huu utamaduni niliusikia nadhani utakua ukouko kwa wamasai
mwanaume kama umeoa kasichana kako kazuri siku ukitoka kuchunga mifugo yako na ukarudi nyumbani ukapepesa macho ukiona mkuki umechomekwa ardhini na nyumba imefungwa basi ujue mke wako anagegedwa ndani uko
na hakuna kupanic hapo ndo utamaduni huyo, hapo wewe unatulia pembeni huku unamsikiliza mke wako akilia kwa key za vinanda na marimba
mchezo ukiisha unaingia ndani kinyoonge!
Wale hawaliagi mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom