Ni upi msimamo wa Uislam na Ukristo juu ya Artificial Intelligence.?

The August

JF-Expert Member
Oct 9, 2018
1,080
2,024
Habari za weekend wakuu?

Kwa wafuatiliaji wa maendeleo ya sayansi duniani, inafahamika kuwa Artificial Intelligence ndio muelekeo wa dunia. Kwa sasa kuna magari na ndege yasiyo na dereva mwanadamu, pia kuna mwanadamu wa bandia mwenye hisia mithili ya mwanadamu. Hivi Karibuni kampuni ya kimarekani iliyopo nchini China ya Hanson Robotics imemzindua mtu huyu kwa jina anaitwa Sophia.

Tazama video hii, ambayo Muigizaji Will Smith akifanya mazungumzo na Sophia.



Hapa pia akifanya mahojiano na mwanahabari wa UN



Nirudi kwenye hoja/swali langu.

Tunajua kuwa dini (kwa maana ya Uislam na Ukristo) zimeeleza takribani kila kitu kitokeacho duniani kwa utabiri (Prophesized) au kimeweka msimamo wake juu ya jambo fulani aidha kwa kulikubali au kulipinga. Je, ni upi mtizamo au msimamo wa dini hizi kuu mbili juu ya Artificial intelligence? Je, ni inaweza kuwa ni muendelezo au mwanzo wa kile kiitwacho Mpinga Kristo (Anti Christ) ambaye anazungumzwa kwenye dini zote mbili?



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengine wanasema hivyo ni vitabu vya hadithi tu za kale.
Hivi kweli hivyo vitabu viseme kuhusu sensors, image, speech processing, machine learning, microcontrollers, ARM etc?
Kuna mtaalam ametupa hii.
Screenshot_20190413-131317.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati upi ni wa mwisho? Infinity? Namaanisha huo wakati wa mwisho ni upi hasa? Maarifa kuongezeka hata enzi za kutoka kula raw meat na kuanza kutumia moto ni maarifa yaliongezeka. Kina Galileo waligundua vitu zamani sana (maarifa yaliongezeka). Sasa watu now kugundua AI ndio maarifa yameongezeka as ni wakati wa mwisho huu?
 
Vitabu vyenu na imanizenu bakizeni huko kwenye majumba yenu ya kuabudia..

Mambo ya technologia na sayansi hayahitaji/hayatumii imani..na farytales stories..

Hivyo usichanganye madesa hapaa
 
Huwezi kufananisha kipindi cha kuna Galileo na sasa saivi maarifa yamepanuka sana na dunia inaenda kasi kuliko kawaida miaka ya 90 generation ya computer ilikuwa taratibu sana ila miaka15 nyuma tulikuwa na 1G saiv 5G na kupoteza shughuli nyingi za kibinadamu mbeleni dunia itakuwa vululuvululu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari za weekend wakuu?

Kwa wafuatiliaji wa maendeleo ya sayansi duniani, inafahamika kuwa Artificial Intelligence ndio muelekeo wa dunia. Kwa sasa kuna magari na ndege yasiyo na dereva mwanadamu, pia kuna mwanadamu wa bandia mwenye hisia mithili ya mwanadamu. Hivi Karibuni kampuni ya kimarekani iliyopo nchini China ya Hanson Robotics imemzindua mtu huyu kwa jina anaitwa Sophia.

Tazama video hii, ambayo Muigizaji Will Smith akifanya mazungumzo na Sophia.



Hapa pia akifanya mahojiano na mwanahabari wa UN



Nirudi kwenye hoja/swali langu.

Tunajua kuwa dini (kwa maana ya Uislam na Ukristo) zimeeleza takribani kila kitu kitokeacho duniani kwa utabiri (Prophesized) au kimeweka msimamo wake juu ya jambo fulani aidha kwa kulikubali au kulipinga. Je, ni upi mtizamo au msimamo wa dini hizi kuu mbili juu ya Artificial intelligence? Je, ni inaweza kuwa ni muendelezo au mwanzo wa kile kiitwacho Mpinga Kristo (Anti Christ) ambaye anazungumzwa kwenye dini zote mbili?



Sent using Jamii Forums mobile app

mkuu msimamo wa dini uko pale pale kwamba ni kumuamini mungu yupo,kumuomba mungu na kumuabudu na kuomba msamaha....haya ni matukio tuu ya kawaida kumbuka hata zamani kuna watu walikua magenius ni muendelezo wa ufanyaji akili za binadamu ndio zinazo endelea....na mpinga christo ni mtu yeyote yule anaye kwenda kinyume na matakwa ya mwenyezi mungu kwa maana hata huyo alitengeneza a.i kajaaliwa namungu pia so katika hali ya kawaida ni maendeleo na yeye akitoka hapo anamsukuru mungu kwa uwezo wa kiakili za kibinadamu kugundua
 
Back
Top Bottom