Ligogoma
JF-Expert Member
- Aug 27, 2010
- 3,502
- 6,444
Ndugu wanaJF,
Kuna baadhi ya vitu huwa vinatumiwa tu na wanawake, lakini pia vipo vinavyotumiwa na wanaume tu, japo vipo ambavyo twaweza kutumia pamoja. Sitaki kuzungumzia perfume maana nahc kutakuwa na ubishi sana. Unakuta perfume imeandikwa 'for women' lakini mwanaume kajipulizia nyingi, vitu kama simu kutegemeana na rangi twaweza kutumia wote.
Hoja yangu ni matumizi ya LIPBUM kwa wanaume. Mimi huwa nikienda salon nikipakwa najihc kama njiani nasemwa kwasababu sijui. Naomba tusaidiene hapa hasa wale wanaotupaka au wanaotengeneza au wauzaji.
Nililazimika kuzitrumia kwa mara ya kwanza Iringa ilikuwa ni mwezi wa sita, kuna baridi na upepo mkali sana. Nilipasuka lips mpaka zikawa zinatoa damu pamoja na kujilamba sana lakini haikusaidia, nikaletewa hayo mafuta ya mdomomoni na yalinisaidia sana kupona.
Kikubwa inategemea mtu anazitumia katika mazingira yepi, anajipodoa tu au anatumia kwa sababu za msingi??