Ni sahihi mkeo kufanya haya?

Ni sahihi mkeo kufanya haya?

inategemea na tabia za hao waliokuwa shemeji zake hapo before, kama hawaeleweki not proper
 
Je ni sahihi kwa mwanamke uliye muoa na ukamkuta na mtoto tayari kuendelea kuwasiliana na shemeji zake, yaani baba wadogo wa mwanae? Tena mazoea ya kupeana hata appointmetn za kwenda kukaa seheme akiwa na mtoto na baba wadogo wa mtoto huyo.

Ukimuuliza anasema wanajadili kuhusu mtoto mana baba mzazi wa mtoto huyo alifariki.

Naombeni ufafanuzi. Mnalichukuliaje hili?

kama unauhakika ni shemeji zake haina shida mkuu...ila shida ipo kama ni mume mwenzio hapo patachimbika...
 
Je ni sahihi kwa mwanamke uliye muoa na ukamkuta na mtoto tayari kuendelea kuwasiliana na shemeji zake, yaani baba wadogo wa mwanae? Tena mazoea ya kupeana hata appointmetn za kwenda kukaa seheme akiwa na mtoto na baba wadogo wa mtoto huyo.

Ukimuuliza anasema wanajadili kuhusu mtoto mana baba mzazi wa mtoto huyo alifariki.

Naombeni ufafanuzi. Mnalichukuliaje hili?

Si sahihi kabisa, akupe simu ili wawasiliane na wewe ka chochote kuhusu mtoto, otherwise arudishe huyo mtoto kwao wakamtunze.
 
Mkuu handsome1 pole sana tena sana.

Kwanza ni makosa makubwa sana mtu kutoa appointment kwa mke bila ridhaa yako,kumbuka huyo ni mke wako kama bado ana mawasiliano na mashemeji zake wa mwanzo ni vyema hatua zifuatazo zikachukuliwa kwa faida ya ndoa yenu.

1.Mwelezo mke wako kwamba kwakuwa ana mtoto wa watu ni vyema huyu mtoto akachukuliwa na wenyewe ili kuondoa usumbufu wa mawasiliano yenye shaka shaka.

2.Yalikuwa ni makosa yako kuoa mwanamke mwenye mtoto.wasichana vigoli vya ukweli wamejaa kila pembe ya nchi,tena siku hizi vijana mna uwanja mpana wa EA Uganda,Rwanda,Burundi and Kenya kote huko kuna wasichana kibao.Kwakuwa tayari umeshafanya makosa ni lazima mke wako mawasiliano na upande wa pili yasitishwe mara moja.

3.Ikiwa mkeo atagoma mwache aendelee na mawasiliano kwanza makabila mengi mke akifiwa na mume anarithiwa sema hili gonjwa la UKIMWI limekuja tbua mambo mengi.


Je ni sahihi kwa mwanamke uliye muoa na ukamkuta na mtoto tayari kuendelea kuwasiliana na shemeji zake, yaani baba wadogo wa mwanae? Tena mazoea ya kupeana hata appointmetn za kwenda kukaa seheme akiwa na mtoto na baba wadogo wa mtoto huyo.

Ukimuuliza anasema wanajadili kuhusu mtoto mana baba mzazi wa mtoto huyo alifariki.

Naombeni ufafanuzi. Mnalichukuliaje hili?
 
Last edited by a moderator:
Ni sahihi.

Wewe hutaki mtoto ajue baba zake wadogo?

Kama unaona si sawa ulitegemea nini ulipooa mwanamke mwenye mtoto? Ulitegemea umkate mtoto kabisa kutoka familia ya baba yake?
Hapa tatizo sio mtoto kujua baba zake, maana pia wanatakiwa wawajibike kwa malezi maana ni damu yao, ishu hapo ni jinsi mambo yanvyofanyika kienyeji, utafikiri wao ndio wenye mke.
 
hivi kila mwezi kuna majadiliano ya matunzo ya mtoto KWANINI? kwani mkishakubaliana ada ya shule ,mavazi,mahitaji ,muhimu kila mwezi utatoa kiasi kadhaa,majadiliano mengine yanini tena? au baba wakufikia ina wezekana hata mtoto akiumwa hutoi hela ya matibabu na kama unatoa ,nini kinaendelea,mimi nimepitia huko ila sijawahi kutamani majadiliano ya nini zaidi ya kuharibu ndoa yangu ,na je ulishamweleza mwenza wako kuhusu huo wasiwasi wako,minadhani ni muhimu wawe na makubaliano kamili,yanayoeleweka ,kama wanataka kumuona mtoto,wasubiri akifunga shule aende kusalimia kwa muda na kurudi na kama mtoto ni mdogo ,basi ijulikane wazi kwamba mama anampeleka mtoto akaonane na nduguze ,ila sio bar,nasio lazima mtoto apelekwe wao wanaweza kuja kumuona ukiwepo,UNAJUA SISI WAMAMA WAKATI MWINGINE TUNAHARIBU WENYEWE SASA ,UMEOLEWA BADO UNATAKA OFA ZA ZAMANI ZA NINI,KAMA UNAKITU UNATAMANI SI UMWAMBIE MWENZAKO NATAMANI NYAMA CHOMA ,KULIKO KUMFANYA MWENZIO AWAZE MPAKA AOMBE MSAADA ,ILA CHA MSINGI ZUNGUMZA NAE MKUBALIANE KITU KINACHOELEWEKA ,NA URIDHIKE MOYONI ILI MAISHA YAENDELEE,KILA LA KHERI.
 
hivi kila mwezi kuna majadiliano ya matunzo ya mtoto KWANINI? kwani mkishakubaliana ada ya shule ,mavazi,mahitaji ,muhimu kila mwezi utatoa kiasi kadhaa,majadiliano mengine yanini tena? au baba wakufikia ina wezekana hata mtoto akiumwa hutoi hela ya matibabu na kama unatoa ,nini kinaendelea,mimi nimepitia huko ila sijawahi kutamani majadiliano ya nini zaidi ya kuharibu ndoa yangu ,na je ulishamweleza mwenza wako kuhusu huo wasiwasi wako,minadhani ni muhimu wawe na makubaliano kamili,yanayoeleweka ,kama wanataka kumuona mtoto,wasubiri akifunga shule aende kusalimia kwa muda na kurudi na kama mtoto ni mdogo ,basi ijulikane wazi kwamba mama anampeleka mtoto akaonane na nduguze ,ila sio bar,nasio lazima mtoto apelekwe wao wanaweza kuja kumuona ukiwepo,UNAJUA SISI WAMAMA WAKATI MWINGINE TUNAHARIBU WENYEWE SASA ,UMEOLEWA BADO UNATAKA OFA ZA ZAMANI ZA NINI,KAMA UNAKITU UNATAMANI SI UMWAMBIE MWENZAKO NATAMANI NYAMA CHOMA ,KULIKO KUMFANYA MWENZIO AWAZE MPAKA AOMBE MSAADA ,ILA CHA MSINGI ZUNGUMZA NAE MKUBALIANE KITU KINACHOELEWEKA ,NA URIDHIKE MOYONI ILI MAISHA YAENDELEE,KILA LA KHERI.

like like like
Umeongea kitu mhim hapo kwny herufi kubwa!
 
Back
Top Bottom