Ni sahihi lakini, Feedback (Mrejesho wa taarifa) ni muhimu zaidi

Hamza Nsiha

JF-Expert Member
Jul 25, 2022
208
191
Leo, nimetenga muda wangu kupitia maoni ya ndugu zangu kuhusiana na changamoto juu ya mabasi yaendayo kasi, ni dhahiri kuwa ni jambo ambalo kwa sasa linahitaji kutiliwa maanani kwa sababu hata mimi leo nime_experience hizo changamoto hadi nikaamua kughairi safari ilihali nilikuwa nmeingia ndani ya kituo nikiwa na dhumuni la kuelekea Kimara kutokea Magomeni mida ya saa kumi na mbili jioni.

Kwangu, ninaweza kusema kuwa kuongeza mabasi ndio suluhisho kuu lakini kwa kuwa kila jambo linahitaji process ikiwemo masuala ya budgeting n.k lakini mamlaka husika ingekuwa ikitoa hata Mrejesho wa mara kwa mara kuhusiana na changamoto hizo.

Kutotoa taarifa, huleta tafsri tofauti tofauti na huibua maswali mengi kwa walengwa kwani hata kama jambo haliwezi kutimia katika siku za hivi karibuni La! Hasha tunahitaji kuhuishwa juu ya upokelewaji wa kero zetu, mikakati iliyowekwa na ni kwa muda gani tunaweza subiri ili tuandae fikra zetu.

Anyway, nmekosa hadi usingizi nikitafakari juu ya 750/=Tsh yangu ambayo imekwenda bure pasipokufanikisha safari yangu.
 
Hela za mwendokasi nadhani kuna sehemu hupelekwa na haziwezi rudi kwenye mradi husika.
Either zinalipa mikopo, Zinatumika kwenye sector tofauti, kwa uchache inawezekana zinaliwa....

Mbili kwakweli mwendokasi ni mpango ambao haupo makini kabisaaaaa...

Bora wewe unayetoka magomeni.
Wapo wale wa kibaha mpaka kimara stop over,

Hakuna vituo vinavyowazuia kwa jua wala mvua.
Wanakaa almost 30-50 mins kupata usafiri kwa mida ya mchana.

Asubuhi zinajaaa saaaaana. Kero kero kero.
Raisi hapandi, makamu wake hapandi, mawaziri hawapandi, wala wabunge.
They don’t see ila watanzania wanateseka saaaana mioyo kwa utaratibu wa mwendokasi.
Usiombe uwe una wahi asubuhi. Lazma ubanane.
Usiombe unatoka mchana jua ni kali sanaaaa
Usiombe kuwe na mvua lazma ulowe.
Usiombe una haraka lazma uchelewe.
MWENDOKASI NI MAUMIVU MAKALI SAAANA.
Jiwe aliendesha akiwa na watu kumi tu. Ila kiuhalisia hawajui nature ya zile gari. Wanazijaza saaaana

ONLY HELP NI HUPATI FOLENI UKISHALIPANDA LINA NJIA YAKE TU. ILA NI BIG FAILURE MWENDOKASI.
 
Back
Top Bottom