Ni sahihi kumtoa mama yako kwa baba yako kwa sababu ya kuteswa?

LA7

JF-Expert Member
Aug 26, 2019
457
1,721
Binafsi natamani siku moja mama yangu akae kwa amani lakini ndo hivo nawaza bado sina pa kumlaza pia yule ni mumewe na hatujui walikutana vipi.

Nawapenda sana wazazi wangu wote wawili ila kinachoniumiza haupiti mwezi bila baba kumkosesha mama amani.

Kwa vitu ambavo baba ndo huanzisha ugomvi, mm nipo mbali na nyumbani ila kuna ugomvi umetokea huko.

Mama yangu anauzaga vitumbua sasa alikuwa amesafiri kama siku tatu hivi baada ya kurudi akakuta baba ameuza yale mahindi kwenye gunia moja ametoa debe mbili mahindi ambayo ni yametokana na vitumbua.

Sasa alipoulizwa akawa mkali eti amenunua mbolea, ni kweli amenunua mbolea ila hiyo haikuwa shida sana, shida inakuwa hapa hiyo mbolea aliyonunua huwa anapeleka kwa wanawake wengine, yaani baba ana ndoa za wake 3

Na hakunaga usawa hawezi toa huko kwa wake wadogo alete kwa mama yangu zaidi ni kutoa kwa mama na kupeleka kwa wake wale wadogo.

Kuna kipindi sisi tunaweza lala njaa ila kule kwingine wakala lakini kule kukiwa hakuna unga anakuja ndani anachota na kupeleka kwa wake wadogo na mama akiongea tu anaanza kumpiga japo ss hivi amebakia kwenye mdomo tu, ila mama yangu ndo namuonea huruma

Hanaga roho mbaya yakipikwa mkande jungu kubwa mchana mpaka jioni huyakuti ila kwa wake wengine mpaka kesho yapo ikibidi na kichacha kabisa, nafikiri mmenielewa,

Ila shida yangu namsaidiaje huyu mama yangu
 
Kama unauwezo mtoe mama yani msaidie utapata baraka nyingi sana, mimi nisingeuliza hata hili swali huku ningekua nimeshafanya muda, wewe huoni mama anapitia mengi mama ana maumivu mengi sana ukiongea nae atakua amepoteza hata nuru, ukichanganya na maumivu ya mapenzi anayoyakosa kwa baba yako, ndugu wewe upo sawa kabisa hili ni la mpaka uombe ushauri juu ya nini ufanye?
 
Dah apo kumbuka pia mzee anapeleka chakula kwa wadogo zako pia, huna namna ndugu yangu tikiti bovu lipo shambani kwako.

Mimi nilienda kutoa ushahidi mahakani maza kuachana na mzee (baba wa kambo) miaka ya nyuma uko nilikua mdogo sana darasa 3 hivi ndoa ikavunjwa baada ya ugomvi wa mara kwa mara

Wadogo zangu wamekua wakubwa wameambiwa mi ndio nilitoa ushahidi mahakaman ndoa ikavunjwa mmoja ameanza kunichukia kiaina now yupo karibu sana na wazee wake kiufikupi amenuna dah!
 
Dah apo kumbuka pia mzee anapeleka chakula kwa wadogo zako pia,huna namna ndugu yangu tikiti bovu lipo shambani kwako.

Mimi nilienda kutoa ushahidi mahakani maza kuachana na mzee (baba wa kambo) miaka ya nyuma uko nilikua mdogo sana darasa 3 hivi ndoa ikavunjwa baada ya ugomvi wa mara kwa mara

Wadogo zangu wamekua wakubwa wameambiwa mi ndio nilitoa ushahidi mahakaman ndoa ikavunjwa mmoja ameanza kunichukia kiaina now yupo karibu sana na wazee wake kiufikupi amenuna dah!

Huna kosa usiogope kuchukiwa if you are doing the right thing, wazazi wetu wanapitia mengi hasa mama zetu tunatakiwa tuwatetee na kuja kuwasaidia maana ni wavumilivu kuna tabia
Za kijinga za wazazi wetu wa kiume, na sisi tusirudie ujinga huo
 
Wewe kama mtoto huna uwezo wa kumtoa mama yako kwa baba yako na kumpeleka unapotaka.

Kumbuka hyo unayemuita mama yako ni mke wa mtu ambaye ni baba yako.

Mshauri mama yako adai talaka akishakuwa divorced mchukuwe.

Vinginevyo utagombamba na mzee wako.

Nakupa ushauri kikubwa,,
 
Huyo ni mke wa baba yako sio wako

Situation kama hizo ni ngumu sana. Wameanza kugombana kabla hujazaliwa na bado wapo

Ugomvi wa wazazi ni ngumu kuingilia
Utamchukua utakaa naye then baba yako ataleta ugomvi au mama utashangaa na mumewe wanayajenga anakwambia nirudishe kwa mume wangu..
 
Wewe kama mtoto huna uwezo wa kumtoa mama yako kwa baba yako na kumpeleka unapotaka.

Kumbuka hyo unayemuita mama yako ni mke wa mtu ambaye ni baba yako.

Mshauri mama yako adai talaka akishakuwa divorced mchukuwe.

Vinginevyo utagombamba na mzee wako.

Nakupa ushauri kikubwa,,
Umeongea point sana na kikubwa sana uwezi mchukua mtu ambaye ni mama ambaye ni mke wa mtu ili hali bado hajaachika Amchukue akiwa ashapewa talaka sasa akishakaa nae alafu mzee akijifanya kuja kuomba msamaa hapo ndo atampa masharti yake
 
Huna kosa usiogope kuchukiwa if you are doing the right thing, wazazi wetu wanapitia mengi hasa mama zetu tunatakiwa tuwatetee na kuja kuwasaidia maana ni wavumilivu kuna tabia
Za kijinga za wazazi wetu wa kiume, na sisi tusirudie ujinga huo
Kwa hiyo wazazi wana mambo ya KIJINGA???Hebu jitafakari
 
Huyo ni mke wa baba yako sio wako

Situation kama hizo ni ngumu sana. Wameanza kugombana kabla hujazaliwa na bado wapo

Ugomvi wa wazazi ni ngumu kuingilia
Utamchukua utakaa naye then baba yako ataleta ugomvi au mama utashangaa na mumewe wanayajenga anakwambia nirudishe kwa mume wangu..
Naongezea tu, Kwa ujumla hiyo familia bado ni walala hoi, hata huyo kijana bado hajawa na kifua cha kumtunza mama yake, ukute hata kuoa bado.
 
Wewe ni Kijana mpumbavu sana na unasikiliza habari za upande mmoja wa Mama yako!

Mama yako inaonyesha ni mshenzi na anakudanganya, na wewe ulivyo mjinga umejaa!

Vipi Mama yako ameshakuambia alivyokuwa anamnyima baba yako unyumba hadi kupelekea kuoa wake wadogo?!

Mangapi mazuri Baba yako amemfanyia Mama yako na hakuelezi wewe mtoto!?

Wewe na Mama yako hizo debe mbili za Mahindi alizochukua Baba yako ndizo mnaona za maana?!

Unasema nyie mnalala njaa lakini wake wengine wanakula, wewe hua unajuaje kama sio uongo na wivu wa mama yako tu kwa wake wenza!

Ambacho Mama yako hakuelezi ni kwamba Baba yako baada ya kupata wake wadogo sasa hapati unyumba ule aliokuwa anamringishia Baba yako!!

Hiyo ndiyo njaa ambayo Mama yako analala kwa sasa , usiingilie huo ugomvi!!

Hata huo Mtaji wa vitumbua ukichunguza vizuri utakuta Baba yako ndo alimpa Mama yako!

Watoto na hasa wa kiume msipende sana kuingilia ugomvi wa Wazazi wenu na hasa kuchukua upande wa Mama zenu!
 
Binafsi natamani siku moja mama yangu akae kwa amani lakini ndo hivo nawaza bado sina pa kumlaza pia yule ni mumewe na hatujui walikutana vip,

Nawapenda sana wazazi wangu wote wawili ila kinachoniumiza haupiti mwezi bila baba kumkosesha mama amani

Kwa vitu ambavo baba ndo huanzisha ugomvi, mm nipo mbali na nyumbani ila kuna ugomvi umetokea huko,

Mama yangu anauzaga vitumbua sasa alikuwa amesafiri kama siku tatu hivi baada ya kurudi akakuta baba ameuza yale mahindi kwenye gunia moja ametoa debe mbili mahindi ambayo ni yametokana na vitumbua,

Sasa alipoulizwa akawa mkali eti amenunua mbolea, ni kweli amenunua mbolea ila hiyo haikuwa shida sana, shida inakuwa hapa hiyo mbolea aliyonunua huwa anapeleka kwa wanawake wengine, yaani baba ana ndoa za wake 3

Na hakunaga usawa hawezi toa huko kwa wake wadogo alete kwa mama yangu zaidi ni kutoa kwa mama na kupeleka kwa wake wale wadogo.

Kuna kipindi sisi tunaweza lala njaa ila kule kwingine wakala lakini kule kukiwa hakuna unga anakuja ndani anachota na kupeleka kwa wake wadogo na mama akiongea tu anaanza kumpiga japo ss hivi amebakia kwenye mdomo tu, ila mama yangu ndo namuonea huruma

Hanaga roho mbaya yakipikwa mkande jungu kubwa mchana mpaka jioni huyakuti ila kwa wake wengine mpaka kesho yapo ikibidi na kichacha kabisa, nafikiri mmenielewa,

Ila shida yangu namsaidiaje huyu mama yangu
Mkuu
Fanya maamuzi. Mchukue mama ukae naye miezi mitatu apumzike kisha arudi kwake
 
  • Thanks
Reactions: jpb
Pole Sana Inaumiza Hasa Family Zetu Ambazo Ugomvi Ndiyo Maisha
Mtoe Hapo Akikataa Mama Mwenyewe Muelezee Faida Na Hasara
Wakati Mwingine Family Zetu Zinaleta Aibu Kubwa Mtaani
 
Back
Top Bottom