Caroline Danzi
JF-Expert Member
- Dec 19, 2008
- 3,713
- 1,269
Ni nini hasa Mwanamke anahitaji kutoka kwa Mwanamume na katika Maisha yake?
Assume:
1. Ni binti Mrembo wa asili wazazi wako ni watu makini, waelewa, wasomi na wanaoheshimika sana katika jamii na wamekulea vema, ukapata mume makini anayejiheshimu na mwenye upendo wa kweli akakuoa - Hutaki kutulia macho juu juu, memeo akagundua nyendo zako na kukukanya, ukaomba msamaha akakusamehe maisha yakaendelea.
2. Ulikuwa huna kazi, mumeo akakukabidhi kampuni uiendeshe, ukaifanya kampuni kijiwe cha mashoga zako na mawasiliano na wanaume zako na kisha kutafuna mapato ya kampuni, mumeo akakuondoa kukunusuru wewe na kampuni. Ukakusamehe makosa yako maisha yakaendelea.
3. Mumeo kwa upendo ili usiwe bored akakutafutia kazi nzuri na makini ya kuheshimika, ukaanza kufanya kazi lakini kiwango chako cha utendaji kikawa chini na pia bado unajihusisha na wanaume nje ya ndoa. Mumeo akagundua, kakukanya tena ukaomba msamaha. Mwajiri akaamua kukuondoa kazini kwa kuwa kazi huwezi.
4. Mumeo akaamua kukutafutia mtaji mkubwa ufanye biashara zako, ukatumia bado nafasi hiyo kuendeleza mambo yako na wanaume.
5. Bado mumeo kakununulia gari na unaweza kutumia magari mengine yaliyopo nyumbani, lakini bado huonekani kuridhika.
6. Mumeo huyo, anakuonyesha mapenzi makubwa usiku na mchana, anakutunza, anakupa kila kitu utakacho, anakupa pesa zozote unazohitaji na kukupeleka popote utakapo nakuridhisha kwa mahitaji yako yote ya kimapenzi, kimwili, kihali na kimali lakini bado hutulii wewe na wanaume tu.
7. Elimu yako ilikuwa ya chini akakuendeleza kufikia level ya Chuo Kikuu (Degree), lakini bado wewe na wanaume tu kila kukicha.
8. Mumeo kwa upendo hakutaka mambo yako yajulikane nje hata hivyo mara kadhaa katumia rafiki yake wa familia wa karibu sana kukuonya ili ujirekebishe, kila wakati unaomba msamaha utaacha na kujirekebisha lakini huachi. Anajitahidi kukuchukua mara kwa mara mkapime HIV ili kujinusuru na kukufanya uwe makini lakini somo halieleweki.
9. Mumeo anakuchukua nje ya nchi mahali kwa likizo muwe wawili tu mpate kudumisha mapenzi na kurelax, lakini muda mwingi wewe unautumia kupiga simu kuongea na wanaaume wako na SMS kibao.
10. Hatimaye mume wako anaamua kukufuatilia ajue ni nini shida yako hasa, anagundua miaka yote mliyopo katika ndoa umekuwa na mahusiano na wanaume wengine na kibaya zaidi ni kuwa si moja tu bali ni zaidi ya watatu. Ili kusikia kauli yako kama ni kweli unafanya hayo mambo safari hii anamuhusisha mama yako mzazi ambaye ndoyo tegemeo la mwisho la kwako, unakubali mbele ya mama na mumeo kuwa ni kweli hayo mambo umekuwa ukiyafanya na kutahayari kuonyesha kuchanganyikiwa na sasa mume umeamua "Kujiweka Pembeni, kuepusha msongamano".
Lakini bado hili jambo linaaacha maswali mengi moja wapo ni hili: NI NINI HASA MWANAMKE ANAHITAJI KUTOKA KWA MWANAUME NA KATIKA MAISHA YAKE?
Pole sana superman, tatizo liko kwako unatakiwa upate KIKOMBE upate kupona
Kumfukuza mwanamke, si suluhisho, kwani kama hautafanya utafiti na kugundua tatizo yaaani utawafukuza mwisho utajifukuza nawe pia
Mwanamke mpe vyooote, kuanzia gari mpaka utajiri wako wote lakini vyote ni bure, jamaa watakukanyagia mpaka pasi
Hili ni tatizo kwa wanaume wengi, kwani wengi wetu hatuna elimu ya kufanya mapenzi, tulivyokuwa form two tulikuwa tukidanganyana kuwa wanawake wanapenda shaft kubwa, tukaangaika kuchacha madodoki na mihogo ili tuwe na shaft kubwa na kuwatosheleza marafiki zetu wa kike, mara oooohh, mara wengine mawazo yao ni kuwa ukiwa na shaft fupi huwezi kumtosheleza mwanamke unatakiwa uwe na shaft ndefu ukiipenyeza ikaribie nyumba ya uzazi ili apate raha anayohitaji. Tulutoka sekondari tukiwa kila mtu na lake.
Mwanamke anahitaji ufanisi wa tendo la ndoa, si shaft nene, fupi, au ndefu wala vitu vya kifahari.
Mwanamke anahitaji maandalizi, chukua mfano wa daktari anayejiandaa kumfanyia mgonjwa upasuaji, hakurupuki kuchukua mkasi na kuanza kufanya upasuaji, kwanza lazima amkague mgonjwa wake, ahakikishe dawa ya usingizi imekolea sawa sawa kisha ndio upasuaji utaendelea. Vivyo vivyo kwa mwanake.
Mwanamke anahitaji muda wa maandalizi kabla ya tendo, si una mchojoa nguo kisha unapaka mate na kuzama ndani, hapo utamuumiiza na mwisho wa siku lazima usaidiwe na wajuvi wa mambo. kuna sehemu si za kukimbilia kupapasa, mfano ukishamuweka mamaa kitandani unakimbilia kutomasa kinembe, kwa taarifa yako hapa unampa maumivu, na kumfanya asifurahie tendo la ndoa, anza na nyayo, ukifika hapo kati ruka endelea na tumbo mpaka utosi, kisha rudi kati, baada ya hapo unaweza kuanza kuchimba madini.
Superman tuonane kwenye pm kwa ushauri zaidi, huyo mwanamama usimuache, dawa ipo kaka
Nawashauri jamani wanaume na wanaake tuombee mungu atupe wake/waume wema, atuondolee tamaa za mwili, atupe hekima ya kipekee kujua nani anakupenda na asiye. waleeni wake na waume zenu kidini zaidi. Mambo magumu, huna cha kumfanyia mtu uliyekutana ne ukubwani. siyo mtoto uliyemzaa unajua tabia zake tangu utoto.
Tunamshirikisha mungu kwa sababu hakuna zaidi. Kila mtu ana shetani lake, mambo yake ya kuzaliwa, kurithi sasa umtoe huko kumleta kwenye mstari ulionyooka ni ngumu ila kwa nguvu za Mungu yote yawezekana.
Bado mpaka leo sifahamu Mwanamke Anahitaji nini hasa.
Kuna wahenga wa kizungu husema, kwa wanaume; " Never try to understand a woman, just love her"
Mwanaume hapendwi, maana ukimpenda utakuwa umekaribisha presha, kisukari na kiharusi papo hapo, mwelewe tu akisema yuko meeting akati ni jumapili elewa, akisafiri alafu ukaiona gari yake mitaani, assume ni dereva anaendesha sio yy.
Mwanamke hata yy mwenyewe hajielewi ila anajipenda sasa ww mtu wa pembeni utamwelewaje?
Na kwa wanawake; " Never try to love a man, just understand him"
Kongosho sante mkuu nimeiweka ktk ubongo wa kna.ntajtahd kuelewa ila dah saa sta ucku anatoka tn wkend au anarud saa 7 ucku tn wkend+then unaambiwa nlikuwa kkaz zaid,inauma hyo ila 2taelewa 2.
thanks