Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,769
- 2,544
wasanii wetu hasa wa bongo fleva huwa wakati mwingine wana nyimbo nzuri sana sema tatizo ni matamshi ya maneno katika nyimbo hizo. hili nadhani linachangiwa na lahaja na kiwango cha elimu pia. mfano kuna wimbo mmoja wa juma necha 'usicheze mbali unga robo' ni wimbo mzuri sema 'kaharibu ile mbaya. kuna sehemu anaongea, "hari ii itakwisha rini?" (hali hii itakwisha lini?) yaani hata hao maproducer hawajui lugha? nani wa kuwanyooshea kiswahili hawa wasanii?