Habari wadada wa MMU? Kwanza kabisa niwape hongera kwa kuolewa, ukitaka kujua thamani ya mumeo angalia wadada walio single kwenye age ya kuolewa, wanavyotamani na kumuomba Mungu usiku na mchana wapate mume. Ni kweli kwenye ndoa kuna changamoto nyingi hasa ukipta mume asiyejua wajibu wake, au tu anajua but hapendi kufanya kama ambavyo, anapaswa. Ni vema kukumbuka pia kuwa kuna mambo mengine yanatokea kwasababu tu ya tofauti tulizo nazo. Pamoja na hayo yetu, wadada/wamama wenzangu naomba niwatie moyo kuwa ni vema kubembeleza mume, kumpa mahitaji ya kihisia na vihuduma vidogovidogo, inapendezesha sana ndoa. Baba anaporudi, mkaribishe kwa tabasamu, inamsaidia kupunguza mastress aliyoshinda nayo mchana, mpe kitu cha kunwa au kula preferably matunda inasaidia kuandaa tumbo lake kabla hajala, na kumuongea kinga kwa ile huduma yetu special. Kisha jitahidi sana chakula umpe wewe usiruhusu mdada wa kazi ampe kama upo, inaongeza care(hata kama hukukipika wewe), wanaume wanapenda sana kujaliwa. Pia kama una watoto jitahidi waone unavyomhudumia baba yao, inamuongezea sana heshima na mwisho naomba wanawake wenzangu kupunguza midomo ( kwa wale wanaopenda kupig makelele (iwe kwa watoto, msichana au mumeo mwenyewe), wanaume wanapenda kukaa sehemu ya nyumba ni penye utulivu. mbarikiwe