Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,897
- 942
MHE. FESTO SANGA - NI MUDA MUAFAKA KUONGEZA VIVUTIO VYA UTALII
Mbunge wa Jimbo la Makete Mhe. Festo Richard Sanga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mpango wake wa 'The Royal Tour' ambao umesaidia kuongeza watalii na kuweka rekodi ya kupokea watalii wengi zaidi tangu kuasisiwa kwa sekta hiyo.
Sanga pia amemshauri waziri wa Wizara ya utalii Mohamed Mchengerwa kuwa na mpango wa kufuatilia watalii wanaokuja nchini, kujua wanavyohudumiwa na uzoefu wanaokutana nao ili kutafuta muarobaini wa sababu inayosababisha watalii kutorudi kwa mara ya pili kutalii.
Sanga amesema kujua vyema maisha na uzoefu wa watalii wanaokuja nchini ni vizuri wizara ikazungumza na madereva wa magari ya watalii na wasaidizi wa watalii kwani wao ndiyo wanaokaa muda mrefu na watalii wanaokuja kutalii nchini.
Mbunge huyo wa Makete mkoani Njombe pia ameishauri serikali kuwekeza malazi ya kisasa kwenye maeneo yenye vivutio vya utalii, ikiwa ni pamoja na kuzungumza na taasisi za kifedha ili kusaidia mikopo itakayohamasisha watanzania kujenga hoteli za kisasa kwaajili ya kusisimua utalii kwenye maeneo mbalimbali ya vivutio vya utalii