Price
JF-Expert Member
- Jan 7, 2014
- 1,502
- 922
Tanzania tuna magereza mengi sana na pia wamo wafungwa wengi sana...!! ndiyo si wote wenye hatia lakini kwann kusingekuwa na mashamba humo magerezani? au hata kuwa na trainings mbalimbali... ninamaanisha magereza wanaweza wakasaidia kuongeza chakula na hata maendeleo ya nchi.. kama mtu akiwa gerezani akafundishwa labda ufundi seremala, wengine kutengeneza hata magari na hata ufugaji anapotoka anakuwa na knowledge flani ya kumsaidia yeye baadaye... na tusingekuwa watu wa kuomba msaada wa vyakula.. pangekuwa na mashamba ambayo magereza wenyewe wangekuwa wanayalima na kupanda mazao ya vyakula nafikiri ingepunguza baa la njaa... hata wangeanzisha kilimo cha mbogomboga na kuuza nafiki pia ingesaidia hata magereza kujiendesha yenyewe..mfano yapo ambayo wafungwa hawana mavazi/sare zao. ni mtazamo wangu!!!