Hiii yangu mwenyewe kabisa.........
Sin moja wala mbili saa SITA mchana nakamatwa.
Kosa wizi wa gari,,, wezi wamekatwa huko nikatajwa Mimi na Mr.
Ilikuwa hivi Mr ana duka la spare za magari aina zote used na mpya sasa alinunua spare used sasa kumbe dereva alifanya anavyojua ( hapa naweka code) basi sprare zilifika dukani zikanunuliwa maisha yakaendelea!!!!!
mwenye gari ni boss mmoja hivi anafahamika tz nzima. Mchongo huo ulifatiliwa mpaka tukakamatwa....
Picha linaanza muda nakamatwa Mr tayari yuko mahabusu tajiri Hana maelezo anataka gari nzima huku sisi tulinunua engine weweweeee hawa maboss wa kibongo waone kwenye tv tu ila usiwe na msala nao..........
Huku akiwa na ushahidi na document zote alizonunulia gari plus maelekezo toka juu.
Nikiwa chini ya special escort nenda mpka benk kwangua vihela vyote, nyumba ya kuishi ilienda, viwanja vyote, tugari thamani zote za ndani duka looote lilipigwa mnada ndo vikapatikana vihela kiasi tajiri akapoa kidogo ,,ndugu yangu ana connection sasa niliweza kupata mkopo benk mkubwa kwa haraka ndani ya masaa24 pia ikapatikana pesa tajiri akazidi kupoa....... Mr akatoka na tukaenda kuandikishana tarehe ya kulipa lile deni haya yote yalikuwa yakifanyika chini ya uangalizi maalum...
Basi Mr alivyotoka hatuna pa kwenda yaani maisha yamepinduka.......
Nakumbuka tulienda kwa mjomba wangu. Basi tulipewa pesa kiasi ili mume wangu aondoke nibaki Mimi uncle akatupa nyumba ilikuwa haijaisha vizuri!!!!!!! Iseee nakumbuka siku Mr anaondoka hatukuweza hata kulombana Mimi kisimi hakikusimama wala Mr dudu lake lilikuwa limelala tu!!!!
Mr alikimbilia mpanda, tulisota sana hapo nimechwa na mimba.
Nilikuwa na smart phone Mr aliniachia nakumbuka ilikuwa black berry kama sijakosea. Mbona nilifanya utapeli wa kujifanya Nina wadada wa kazi!!!!! Yaani unatuma laki ya udalali na nauli nakutumia msichana wa kazi. Nikawa naenda stand naangalia wale wasichana wanaolanda landa nawaunganisha mi nachukua naipata Hela ya kula maana hapo pia nilikuwa na watoto 2
Aisee nimekula sana ugali na majani ya viazi,,, nilishinda njaa na mimba yangu!!!!! Kuna muda nilikuwa nasikia njaa mpaka natapika...Marafiki wote walitukimbia.
Basi muda ukapita tajiri kuja na kukuta ile Hali mjomba alimpa kiasi kadhaa akaondoka...
Hiyo mimba sikwendaga hata clinic manes walichamba lakini walinizalisha!!! Bahati nikapata watoto mapacha wawili na nilizalishwa na mganga mkuu wa hospitali moja hivi ilikuwa kama bahati na alinihudumia Mimi na watoto maana baada ya kuzaa tu nilianza kulia mwenyewe kwa uchungu.
Nakwambia hivi hawa watoto walianza kula na miezi 3,,,,, nilikuwa nawalambisha vimchuzi na chai ya rangi nawapa kuwapoza njaa...,, maziwa yalikauka yenyewe kwa mawazo.
Bwana weweee nikaona nimfate Mr huko huko huwezi amini yaani kenge wangu kule alikuwa anauza duka na kushusha mizigo huku analima!!!!!!??
Basi baada ya miaka miwili Mungu alianza kufungua riziki zake.
Mr alilima mpunga na kupata zaidi ya magunia 100.
Akarudi kwenye madini na kuingia mpanda mining huko mambo hayakuwa mbaya sana tulisota miaka 3 na pesa ya mwisho kumlipa huyo boss niliipeleka mwenyewe mkononi
Yaani nilipanda bus.
Maisha yalianza kunoga Tena mpka tukarudi manispaa kuendeleza tulipokwama.
Ile mimba ya mapacha sasa ni wakubwa miaka 9.
Mpaka sasa ukiniuliza kutendwa na maisha hii kiboko na ilinipa ukomavu mkubwaaaa mnoooo.........