PakiJinja
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 7,683
- 15,858
Mabadiliko ya mawaziri ambayo yamekuwa yakifanywa tangu rais Samia aingie madarakani, yamelenga kupunguza wale wenye umri mkubwa (Senior Citizens) katika nafasi hizo ili kuwapisha au kuwaingiza under 50.
Hili litaenda hadi ndani ya majeshi yetu na taaisi nyingine za usalama.
Mkakati uliopo hivi sasa ni kuingiza fikra mpya kwa kuwaingiza vijana zaidi katika nafasi mbalimbali za uongozi nchini.
Tumeona, hata waziri mkuu ameshafunguliwa mlango wa kutokea.
Mkakati ni mzuri, ila bahati mbaya ni kwamba, wanaoingizwa sasa kwenye mfumo hawataweza kuipatia nchi kile kilichokusudiwa sababu wengi wamelelewa na kuwa crippled na mfumo ule ambao jitihada zinafanyika kuachana nao.
Wengi ni wahafidhina wa mifumo na siasa za hovyo, zile za kifisadi, za kubebana, kutowajibika, rushwa n.k
Kati ya marais 6 ambao hadi sasa Tanzania imewahi kuwa nao, wawili ndiyo waliingia katika urais wakiwa na umri wa miaka 60 and/or above. Rais Ali Hassan Mwinyi, aliingia akiwa na miaka 60, wakati rais wa sasa, Samia Suluhu Hassan, yeye aliingia madarakani akiwa na umri wa miaka 61.
Nikionacho hivi sasa, haijarishi ataendelea au ataamua kutoendelea, lakini rais ajaye baada ya Samia atakua na umri chini ya miaka 50.
Wakati huo zaidi ya nusu ya viongozi wengi wa sasa hususana baraza la mawaziri zitakua ni sura mpya kabisa.
Hili litaenda hadi ndani ya majeshi yetu na taaisi nyingine za usalama.
Mkakati uliopo hivi sasa ni kuingiza fikra mpya kwa kuwaingiza vijana zaidi katika nafasi mbalimbali za uongozi nchini.
Tumeona, hata waziri mkuu ameshafunguliwa mlango wa kutokea.
Mkakati ni mzuri, ila bahati mbaya ni kwamba, wanaoingizwa sasa kwenye mfumo hawataweza kuipatia nchi kile kilichokusudiwa sababu wengi wamelelewa na kuwa crippled na mfumo ule ambao jitihada zinafanyika kuachana nao.
Wengi ni wahafidhina wa mifumo na siasa za hovyo, zile za kifisadi, za kubebana, kutowajibika, rushwa n.k
Kati ya marais 6 ambao hadi sasa Tanzania imewahi kuwa nao, wawili ndiyo waliingia katika urais wakiwa na umri wa miaka 60 and/or above. Rais Ali Hassan Mwinyi, aliingia akiwa na miaka 60, wakati rais wa sasa, Samia Suluhu Hassan, yeye aliingia madarakani akiwa na umri wa miaka 61.
Nikionacho hivi sasa, haijarishi ataendelea au ataamua kutoendelea, lakini rais ajaye baada ya Samia atakua na umri chini ya miaka 50.
Wakati huo zaidi ya nusu ya viongozi wengi wa sasa hususana baraza la mawaziri zitakua ni sura mpya kabisa.