Ni kweli Rais Kikwete hapigiwi Mizinga Zanzibar?

Ni kweli Rais Kikwete hapigiwi Mizinga Zanzibar?

Leo yuko shein kesho akija wa chama kingine mwenye mamlaka hayo mafano seif?maana ndio mkuu wa vkundi vya ulinzi kama kmkm.

Vikundi vya ulinzi kama kmkm havina zana nzito za medani.Military tacticians wa JWTZ sio wajinga ku arm hivyo vikundi na silaha nzito za kimapigano

Hivyo vikundi havina artillery mortars,APCs.fighter jets,radar defence systems.long range missiles na kadhalika

Nacho jaribu kusema ni kuwa hata kichaa kama Hitler awe Rais wa Zanzibar hivyo vikundi vya ulinzi havitaleta adhari zozote kubwa kiusalama

Huwezi kuvuruga amani na SAR au SMG.JWTZ has outgunned all other defence forces
 
Kwa ujumla tu, huu muungano wetu haufai ni lazima tutafute namna ya kuwa na muungano wa kweli na wenye nguvu
 
Ni kweli kabisa hapigiwi mizinga Zenji. Na pia sio mizinga tu hata ziara za kukagua miradi ya maendeleo haendi Zenji kwakuwa ni nchi nyingine. Si yeye wala si Waziri mkuu wa JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. Watu wakielezwa ukweli huu wanaendekeza mipasho na mitusi badala ya kujibu hoja.
 
Huu muungano kuna watu wameufanya kakichaka kakuficha uovu wao na sehemu ya kuneemesha matumbo yao. Kimsingi kilichoandikwa kwenye KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ambayo ndiyo msingi na kiapo cha watawala walioko madarakani sicho kinachotendwa, kusimamiwa na kulindwa kama walivyoapa. Mengi ni usanii mtupu ambao haufai hata kuelezewa mbele ya watu wenye uoni timilifu.

Tukio la sherehe za mapinduzi tarehe 12 Januari 2014 zilizohudhuriwa na Kikwete kama mgeni wa kawaida huku Shein akiwa mgeni rasmi na Amiri Jeshi Mkuu ni ushahidi usiohitaji elimu ya unajimu wala wapiga ramli.
 

Attachments

  • Kikwete 2014.jpg
    Kikwete 2014.jpg
    39.6 KB · Views: 146
  • Shein 2014.jpg
    Shein 2014.jpg
    37.6 KB · Views: 145
  • Shein 2014 1.jpg
    Shein 2014 1.jpg
    65.9 KB · Views: 145
Huwa hajitambulishi kama rais bali mjumbe wa Jk insu ambazo hata Membe au Pinda anaweza kusolve. Nyie Wazinzabar komaeni mtoke kwenye mikufu ya Magamba mukasajili nchi yenu UN, nyie katiba yenu inawatambua ni mamlaka kamili lakini mataifa ulimwenguni yanajua nyie ni Koloni la Tanganyika sababu hamjakamilisha taratibu za kuwa Taifa pale UN kwa kibano cha magamba yanachowapatia!!!

Kwa mvurugano hu wa nchi ilpofika sasa nikufuta serkalj ya zanziar na ibakiserikali ya JMT ili heshima ya rais wa jamuhuri iheshimiwe
 
Mheshimiwa Raisi atabaki kuwa Amiri Jeshi Mkuu pekee nchini.General Mwamunyange ana ripoti kwa Kiwkete na sio mwingine

Kupigiwa mizinga ni ceremonial tu ,kiutendaji Shein hana mamlaka yeyyte ya kijeshi.Tuache upotoshaji

Hujui lolote bora ukae kimya.

Unajua itifaki ya kupigiwa mizinga na kukagua gwaride au we ni wa Rumumba? buku saba
 
Tukiwa na mambo yetu ya ndani Zanzibar ni nchi, Tukitoka kwenye anga za kimataifa inapoteza hali ya kuwa nchi maana ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hicho ndicho nilichokiona kwenye kesi fulani hv ya sovereighty of the state whether Zanzibar is a state. Whether treason can committed in Zanzibar.
 
Hujui lolote bora ukae kimya.

Unajua itifaki ya kupigiwa mizinga na kukagua gwaride au we ni wa Rumumba? buku saba

Mwamunyange ana ripoti kwa nani? Nani kamteua Mwamunyange? Shein au Kikwete?

Unajua kuwa Mkuu wa nchi na Amiri jeshi Mkuu ni vitu viwili tofauti?
 
huitaji kuwa mzanzibar au zanzibar kulijua hili, sherehe za mapinduzi hurushwa live tbc na itv muda mwingine.

Sio tu kutopigiwa mizinga ila hutakiwa kuwahi kuingia uwanjani ili ampokee mgeni rasmi rais wa znz ambaye ndio mkuu wa nchi hiyo.

watakachakachuo hadi hizo kumbukumbu za video

Mtashangaa kuona Kikwete anapigiwa mizinga na inamuonyesha kuwa ni wa Mwisho kuingia, na wa kwanza kuondoka.
 
Ni kweli hapigiwi lakini hata hivyo licha ya Zanzibar kuwa nchi yenye mamlaka kamili, Rais wake hana tofauti na Rais wa TFF!!!
duh hii kali. Raisi wa nchi ya zanzibar ni kama wa tff? Hivi wa tff anapigiwa mizinga eh?
 
Ni kweli hapigiwi lakini hata hivyo licha ya Zanzibar kuwa nchi yenye mamlaka kamili, Rais wake hana tofauti na Rais wa TFF!!!

kanywe uji wa mtoto wako kelvin,baada ya hapo,tulia dk mbili,utapata akili kidogo.
 
kanywe uji wa mtoto wako kelvin,baada ya hapo,tulia dk mbili,utapata akili kidogo.

Sasa mkuu mbona povu tena?? Emu fanyeni jitihada mkasajili nchi yenu UN Mjue kabisa magamba hayawezi kuachia koloni lake kama mtabaki kuchekacheka na kunywa urojo!
 
Rais wa Jamhuri kama amiri jeshi mkuu akiingia uwanjani anapokewa kwa heshima zote za utii na majeshi ya ulinzi na usalama,kwa wanaofuatilia,na wimbo wa taifa hupigwa! Hiyo ndio protocal.acheni kuargue vitu unless ur conversant with the protocal of the Commander in Chief!

Asante. Lakini swali hujajibu, Rais wa JMT huwa anapigiwa mizinga 21 kama Itifaki inavyofahamika?

Wewe unaona kuwa ni simple argument, lakini kama Mkuu wa nchi na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama kutopigiwa miaizinga unaona ni jambo dogo? Labda uniambie kuwa TL alichemka, na hoja zake sio za kweli. Dawa ya tatizo ni kulikabili, badlala ya kulikimbia.
 
Huu muungano kuna watu wameufanya kakichaka kakuficha uovu wao na sehemu ya kuneemesha matumbo yao. Kimsingi kilichoandikwa kwenye KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ambayo ndiyo msingi na kiapo cha watawala walioko madarakani sicho kinachotendwa, kusimamiwa na kulindwa kama walivyoapa. Mengi ni usanii mtupu ambao haufai hata kuelezewa mbele ya watu wenye uoni timilifu.

Tukio la sherehe za mapinduzi tarehe 12 Januari 2014 zilizohudhuriwa na Kikwete kama mgeni wa kawaida huku Shein akiwa mgeni rasmi na Amiri Jeshi Mkuu ni ushahidi usiohitaji elimu ya unajimu wala wapiga ramli.

Nijuavyo mimi kwa kuwa ni Amri Jeshi Mkuu basi kwa heshima hiyo hupigiwa mizinga kunapokuwa na dhifa ya kitaifa...

Ufuatao ni ushahidi wa picha alipopigiwa mizinga 21 wakati wa sherehe za Mapinduzi mwaka 2011...

GO9G0848.JPG


Sosi: i s a a c k i n . com: RAIS KIKWETE KATIKA SHEREHE ZA MAPINDUZI

Watu8, sasa kipi ni kipi kati ya hiziz nukuu kutoka kwako na mwenzako? Tusaidieni, kipi ni sahihi?
 
Mwenye macho haambiwi ona!
Tunazo serikali mbili na nchi mbili ndani ya United Republic!
Tunao Raisi wawili na Amiri Jeshi Wakuu wawili!
01.jpg


Nimekodoa macho simuoni Kikwete, namuona Shein!

IMG_5392.JPG


Nisaidieni jamani, Kikwete kajificha wapi?

057.jpg


Kwa pembeni naona picha ya Shein, simuoni Kikwete!


 
Back
Top Bottom