MSIMISEKI
Senior Member
- Jul 30, 2011
- 123
- 34
Huu muungano kuna watu wameufanya kakichaka kakuficha uovu wao na sehemu ya kuneemesha matumbo yao. Kimsingi kilichoandikwa kwenye KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ambayo ndiyo msingi na kiapo cha watawala walioko madarakani sicho kinachotendwa, kusimamiwa na kulindwa kama walivyoapa. Mengi ni usanii mtupu ambao haufai hata kuelezewa mbele ya watu wenye uoni timilifu.
Tukio la sherehe za mapinduzi tarehe 12 Januari 2014 zilizohudhuriwa na Kikwete kama mgeni wa kawaida huku Shein akiwa mgeni rasmi na Amiri Jeshi Mkuu ni ushahidi usiohitaji elimu ya unajimu wala wapiga ramli.
Rais na amiri jeshi mkuu Dkt Shein alipendeza sana