Mnakuza mambo mbona hata biblia inasema kuna watumishi wa Mungu walitupiwa majini na kuponywa.
Katika kitabu cha Tobiti, Mungu anamtuma malaika Rafaeli ili awaponye wote wawili: Tobiti na Sara (Tobiti 3:17). Kwa upande wa Sara, uponyaji wake ulikuwa ni kuachiliwa huru kutoka kwa pepo mchafu, na sio ugonjwa wa kimwili.
Simulizi hilo linaendelea hivi:
· Tobiti 6:16–18: Rafaeli anamwambia Tobia asimwogope yule jini, na amwambie jinsi ya kumfukuza kwa kutumia moyo na ini ya samaki. Anamwambia, “Basi yule jini ataisikia harufu yake na kukimbia, wala hatakuja tena kamwe” (Tobiti 6:18).
· Tobiti 8:1–3: Baada ya harusi, Tobia anafanya kama Rafaeli alivyomwagiza. Anachoma moyo na ini ya samaki, na moshi wake unamfukuza yule jini, ambaye anakimbilia Misri. Kisha, Rafaeli anamfuata na kumfunga yule jini (Tobiti 8:3).