Ni kweli kuwa hii miti inaua?

Ni kweli kuwa hii miti inaua?

Hapa Afrika hususani Tanzania kuna imani za aina mbalimbali zihusuzo mambo tofautitofauti katika jamii yetu.Zimekuwepo tangu enzi na enzi na kadri miaka inavyokwenda nazi zinaendekea kuwepo ingawa sio kwa ukubwa huo.

Zipo imani kwenye vyakula(food taboos) mfano mama mja mzito na mayai.Wengine wanasema ukilala usiku na mfupa wa kitimoto wanga hawakusumbui!Sijui ikitokea mama mja mzito akamchukia mtu basi kuna uwezekano mkubwa akazaa mtoto anayefanana na huyo mtu!Ukimuona bundi ni dalili ya mkosi....na kadhalika na kadhalika.

Sasa kuna hii nyingine ambayo Kwangu ni mpya na imenishangaza sana.Sijui wenzangu kama mmeisikia au kuwatokea labda...

Kuna mzee wa makamo tulisafiri nae kwenye basi.Kwenye ile kuangalia mazingira kando ya barabara akaona nyumba moja ina miti ile mirefu inayokuwa na matawi kama ngazi ngazi(siijui jina kwakweli).Ni mizuri kimuonekano na inapendezesha Sana nyumba.Akaanza kudai kuwa mizizi ya hiyo miti ni mirefu na huwa inaingia ndani.Ikishakuwa hivyo nyumba yenye hiyo miti ni lazima afe mwanaume.Na pia migogoro ndani ya nyumba ya hivyo haiishi hasa ya mme na mke!Anashuhudia kuwa kuna rafiki zake wawili wameshafariki kabla hajajulishwa hiki suala.Pia kuna mama baada ya kufiwa na me wake akawa haelewani na watoto wake,hawapigi hata simu.Baada ya kutembea kwa wataalam(hapa naeleweka vizuri tuu!) akaambjwa aukate huo mti na kisha amwagie oili Ili kuua mizizi Iliyoingia ndani Baada ya kufanya hivyo watoto wake wakabadilika wakawa na mapenzi nae.Mzee anaongea kwa kujiamini kuwa anamaanisha anachokisema na akawashauri watu mule ndani kama wana hiyo miti wakaikate kabla haijaanza kuwaathiri.....

Je kuna mtu pia kawahi sikia kuhusu hili..ukweli ukoje maana hii dunia ina siri nyingi sana huwezi amini

Huo mti huitwa panga uzazi, wengine sijui huuita nini. Hata mimi nimesikia hayo, lakini sina uhakika.

Miti yote ya Mwenyezi Mungu, yeye ndie ameumba miti hiyo, sasa iweje mti huo uwe na madhara! Kuna jamaa zangu wana mti mkubwa ndani ya fensi, tena miaka, lakini hakuna kibaya kilichotokea.
 
Ungemuuliza jina la hiyo miti maana miti yenye ngazi ipo aina nyingi sana

Itakua anamaanisha panga uzazi
images.jpeg
 
SSijui chochote kuhusu hii Imani ila nachoweza kusema pale nyumbani kwa Mzee wangu. Hii miti aliiotesha nadhani Ni Kama miaka 8 iliyopita.

Cha ajabu Kama miaka 2 au 3 iliyopita, nimefika pale nyumbani nikakuta Yote imekatwa. Ilikuwa miti mitatu. Kumuuliza Mzee, ndio akaniambia ameikata kwa sababu hiyo uliyoitaja kwenye huu uzi
 
Huu ujinga utakuta ameuanzisha mswahili mmoja tu kwa ujinga wake, hii miti kiuhalisia asili yake sio afrika ilitoka ithink ni ulaya lakini cha ajabu sijawahi kusikia eti wazungu wanailalamikia eti inaleta mikosi, je nyumba zisizo na hii miti mikosi yao inatokana na nini na je maeneo ya jangwani ambako mimea ni nadra hakuna mikosi, hii miti kwetu tumeipanda ina miaka 13 sasa
Usibishe au kukebehi kila kitu mkuu, mwisho wa wewe kujua jambo ndio mwanzo wa mwingine kulijua zaidi.
 
Nyumbani tunauita UZAZI WA MPANGO

Miaka ya 2000s ilipoingia ikawa ndo ujanja na maendeleo kuipanda lakini watu waliikata sana kuanzia mwaka 2016 waliposikia habari hizo mpaka sasa haipo tena kwenye mji wetu

Binafsi hadi kwetu ulikatwa kipindi hiko nipo chuoni ila nikaishia kuwalaumu tu kwa kitendo hicho maana ulikubali sana pale uwanjani... kwa kipande kingine hayo yanayosemwa yote ni kama yanaakisi na familia yetu

Tena siyo huo tu kuna mwingine una maua fulani mekundu mazuri (mingine maua meupe) uma tabia ya kutanda juu ukitengenezewa unakuwa kama paa chini mnapata kivuli, ulipandwa zamani sana na mzee uwanjani kwetu enzi hizo ni mimea ya heshima kwelikweli, na wenyewe nikasikia stori hizo napo nikikumbuka kilichotikeaga kule mpaka leo imebaki stori tu...
 
waliowengi wamesikia tu,hata mimi nimesikia tena miaka ya 2000's huko lakini sija proove.
 
MTU akiyeelimika na mwenye iman thabiti hawezi kuamini vitu vya kijinga kama hivi. Mleta uswahili tu hapa
Unajua chochote kuhusu elimu ya mimea?
Unajua chochote kuhusu nguvu za asili?
Unajua chochote kuhusu Roho, nafsi na mwili?
Unajua chochote kuhusu elimu ya maumbo ya vitu, wanyama, ndege, upepo, moto, maji, nk
Hivi ni kwa uchache tu
 
Kwani mkuu, watu kama Hitler, Osama etc waliumbwa na nani? Mbona walileta madhara kwenye dunia...
Wale walikuwa ni mashetani waliovaa mwili wa mtu shetani katika umbo la mwanadamu thus Hittler alikuwa akibadilika sura anatoka kwenye ubinanadamu pindi akiivaa ile roho impayo nguvu hiki kitendo cha kubadilika sura wanacho wachawi wengi wa degree ya 33 freemason wakiwemo
 
Ni nafsi ya mtu tu hiyo, mbona huongelei marekani na washirika wake unyama walioufanya kwa civilians!!
Hapo ndio point yangu ilipo, kwamba vibaya na vizuri vyote vipo kwenye hii dunia na viliumbwa kwa sababu maalum... Tatizo linakuja pale binadamu tunapo vitumia vitu vinavyo tuzunguka bila kuwa na maarifa ya kutosha.
 
Wale walikuwa ni mashetani waliovaa mwili wa mtu shetani katika umbo la mwanadamu thus Hittler alikuwa akibadilika sura anatoka kwenye ubinanadamu pindi akiivaa ile roho impayo nguvu hiki kitendo cha kubadilika sura wanacho wachawi wengi wa degree ya 33 freemason wakiwemo
Ndio mkuu, lakini tunarudi palepale vyote viliumbwa.
 
Huu ujinga utakuta ameuanzisha mswahili mmoja tu kwa ujinga wake, hii miti kiuhalisia asili yake sio afrika ilitoka ithink ni ulaya lakini cha ajabu sijawahi kusikia eti wazungu wanailalamikia eti inaleta mikosi, je nyumba zisizo na hii miti mikosi yao inatokana na nini na je maeneo ya jangwani ambako mimea ni nadra hakuna mikosi, hii miti kwetu tumeipanda ina miaka 13 sasa
Chanzo cha mikosi ni vingi sio lazima mti huo.
Maisha ya wazungu hayafungamani na mizimu tofauti na waafrika kwa maana mizimu ndio chanzo cha waafrika walivyo, so imani hii uenda ikawa na nguvu zaidi afrika.
 
Unajua chochote kuhusu elimu ya mimea?
Unajua chochote kuhusu nguvu za asili?
Unajua chochote kuhusu Roho, nafsi na mwili?
Unajua chochote kuhusu elimu ya maumbo ya vitu, wanyama, ndege, upepo, moto, maji, nk
Hivi ni kwa uchache tu
A always mnbnbnnsn
Unajua chochote kuhusu elimu ya mimea?
Unajua chochote kuhusu nguvu za asili?
Unajua chochote kuhusu Roho, nafsi na mwili?
Unajua chochote kuhusu elimu ya maumbo ya vitu, wanyama, ndege, upepo, moto, maji, nk
Hivi ni kwa uchache tu
I always naamini katika sayansi tu hivyo vingine kama maumbo, moto, maji, upepo ukivitafsiri vibaya lazima vikuletee madhara
 
Back
Top Bottom