Ni kweli Kakakuona anatabiri?

Ni kweli Kakakuona anatabiri?

Mi nafikiri ana uwezo wa kutabiri nimeshaona siku za nyuma akitabiri kuwepo kwa mvua, na mavuno, mengine mengi
 
Naona ameonekana DSM na anaoneshwa kwenye taarifa ya habari ya Clouds Tv. Kuna watu uwa wanaamini kwamba ana uwezo wa kutabiri je ni kweli ana uwezo huo?
Ni kweli Dr M.J Kikwete ni Neurosurgeon!? Ni kweli Mh Mizengo ni male super model for Calvin Klein's briefs and boxers 2015 summer collection !? Ukiweza kujiuliza maswali Kama hayo na kupata majibu sahihi basi Ujue Kakakuona anaweza kutabiri mvua na kufanya biashara ya miamvuli na makoti ya mvua.
 
Mi nafikiri ana uwezo wa kutabiri nimeshaona siku za nyuma akitabiri kuwepo kwa mvua, na mavuno, mengine mengi
Siku za nyuma tulikuwa na misitu mingi hata ukifika pembezoni mwa mji wa dar es salaam utakuta watu wanalima mpunga na mazao karibia mengi maana mvua zilikuwa za kutosha na majira ya mwaka yanaenda sawia. Leo hii unaenda bagamoyo kote kumekuwa mji wakati zamani ukifika tegeta ni pori linaanzia huko na huku kimara mbezi ndio shamba hata watu kununua maeneo hawataki upande wa mbagala hadi ndio hata kongowe huko watu hawakujui wanaona kama sio dar wakati sasa mtu wa pwani anakuambia yupo dar yote hii ni miji imekutana hakuna mapori tena hata mito na mabwawa yamekuwa historia
 
Nadhani ni mbweha

Wanadai mbweha ni fox au jackal,...., pengine labda coyote ni jamii ya mbweha ila si mbweha perce,... au?

Coyote nilimsoma mara ya kwanza kwenye novel moja inaitwa CAIN AND ABEL. Huyu coyote alimsaidia mama fulani kujifungua mtoto akiwa peke yake msituni, na akawa anaendelea kumpa kampani hadi mama akawa anajisisikia kama yuko na binadamu,..., sasa najaribu kupiga picha mbweha hayuko na tabia za namna hii,.. huyu mnyama anaonekana yuko rafiki sana na binadamu na pengine kuzidi hata mbwa, na sometimes anaweza kuwa semi-divine (according to the novel anyway).
 
Naona ameonekana DSM na anaoneshwa kwenye taarifa ya habari ya Clouds Tv. Kuna watu uwa wanaamini kwamba ana uwezo wa kutabiri je ni kweli ana uwezo huo?

Jawabu ni ndiyo kama amekuzidi akili!kinyume na hapo utabiri my foot!
 
Watu wataendelea kubisha tu hata wingu zito likitanda juu na huku kuna upepo mtulivu hawatakubali kwamba kuna mvua kubwa yaja kunyesha.

Ninyi ndio mnaorudisha nyuma tafiti ambazo zinasaidia kujenga na kuimarisha mfumo wa kusoma ishara za nyakati.

Hata biblia Nabii Issa alisema mtakapoona ishara za taifa moja kulishambulia jingine, matetemeko ya ardhi na mengineyo ujue mwisho wa dunia unakaribia.

Hii ina maanisha kuna mambo mengi kadhaa na matukio kadhaa ambayo huashiria kitu fulani kwa wajuzi wa kusoma. Unakumbuka Joseph alivyomtabiria Farao Misri miaka 7 ya neema na itafuata miaka 7 ya dhiki na njaa? Yalitokea, angepuuzi unabii huo angejua kuzaliwa.

Ndugu unamzungumzia nabii au mnyama kaka kuona na magamba yake atembeaye usiku, huishi kwa kula wadudu kama mchwa mwenye uwezo wa kuishi takriban miaka kumi?
 
Si
Mapokea ya mnyama Kakakuona ni kuonekana kwake kwa nadra mno isivyo kawaia kitu ambacho huashiria jambo fulani katika jamii kutokea. Tofauti ya mtazamo wako ni kwamba huyu kakakuona achukuliwe awe anatabiri kila siku jambo ambalo umekwenda kinyume cha maana ya tukio hilo. Tafsiri ya kuonekana kwa nadra kakakuona linatafsiriwa hivyo kutokana na pale anapotokea pasipotegemewa na wenye uzoefu wa kumsoma hupata tafsiri ya kuashiria kitu au jambo fulani kuhusianisha na jamii.

!

Kwamba afugwe haita leta maana tena kwa vile akifugwa hatatokea kwa bahati ya pekee akama inavyotokea bali ni kuonekana kila siku kitu ambacho hakitatuletea tafsiri kadiri ya ishara za nyakati alizotuandalia Muumba wetu. Jaribu Sabayi kukuza kipaji chako cha critical thinking. Thanks.
Kuonekana kwake si nadra kama unavyo fikiri wewe na wenzako wengi wapo noctunal animals wengi tu unaweza usiwaone for a life time ,lakiniukiwafuata katika mazingira yao na muda wao wa kutembea/kujilisha hakika utawaona kila siku!
 
ukiamini Kakakuona ...sitashangaa ukiamini tunguri za manyau nyau
 
Back
Top Bottom