Ni kweli Kakakuona anatabiri?

Kwa hiyo tuwe na imani naye!!! Yaani ningeomba atabiri amani yetu iliyopotea awamu ya nne.
 
Huo ushirikina ndio umetufikisha hapa tulipo. Badala ya kumtegemea Mungu watu watategemea wadudu na wachawi. Inavyoelekea huyo kaka kuona ni pepo tu anawachanganya. Hatuhitaji sijui mdudu /mnyama kututabiria mambo wakati tuna watumishi wa Mungu kila mahali.
 
Tungefikiria sayansi ni ushirikina yasingegundulika yote haya, leo unajua kama alasiri saa kumi kuna mvua, basi huu nao ni ushirikiana? Baadhi ya watoto wanapozaliwa kuna mambo fulani yasiyo ya kawaida kuwepo au mtoto kuonyesha ishara zisizo za kawaida ingawa ni ishara za wakunga na wazazi lakini kuna kitu kinachoashiria upekee wa mtoto katika maisha yake ndani ya jamii inayomzunguka au dunia.

Hata maskini Lazaro alipokuwa anahangaika kuokota masazo ya tajiri yule aliona ni haki yake. Siku alipokufa Lazaro, tajiri naye yakamkuta yayo baada ya maskini Lazamo kuwa kifuani mwa Abraham, tajiri alivyotaabika kule ahera na kutamani Abraham amtume lazaro walao amtilie tone la maji ndani ya kinywa chake kukata kiu. Alikatishwa tamaa kwamba kati yao hakupitiki na yule tajiri aliashiria basi Lazaro afufuke akawatahadharishe ndugu zake wasifanya aliyomfanyia Lazaro.

Jibu lililomkatisha tamaa ni kwamba, wapo manabii huko, wasipowasikiliza hao, hata aliyefufuka kutoka kuzimu hatasikilizwa pia.

Kwa nini wengine huwa wazito kuukubali ujumbe wa wazi? Kazi kwelikweli.

Usitake kufananisha hizi habari na sayansi, utapata aibu.

Journal gani linaloheshimiwa kisayansi limeandika paper yoyote kuhusu Ngakakuona?

Huyo Lazaro hata hatujui kama alikuwapo kweli au ni hadithi kama za Huck Finn.
 
jamani au mwamfananisha na babu wa loliondo, ambaye hadi viongozi walimsujudia na kumwamini na wakalishwa maji taka?
 
Huo ushirikina ndio umetufikisha hapa tulipo. Badala ya kumtegemea Mungu watu watategemea wadudu na wachawi. Inavyoelekea huyo kaka kuona ni pepo tu anawachanganya. Hatuhitaji sijui mdudu /mnyama kututabiria mambo wakati tuna watumishi wa Mungu kila mahali.

mbona unachanganya habari?!, kama unakemea utabiri wa kakakuona kemea pia na unajimu wa hao viongozi wako wa dini maana nao ni viumbe kama alivyo huyo mnyama.
 
Mapokea ya mnyama Kakakuona ni kuonekana kwake kwa nadra mno isivyo kawaia kitu ambacho huashiria jambo fulani katika jamii kutokea. Tofauti ya mtazamo wako ni kwamba huyu kakakuona achukuliwe awe anatabiri kila siku jambo ambalo umekwenda kinyume cha maana ya tukio hilo. Tafsiri ya kuonekana kwa nadra kakakuona linatafsiriwa hivyo kutokana na pale anapotokea pasipotegemewa na wenye uzoefu wa kumsoma hupata tafsiri ya kuashiria kitu au jambo fulani kuhusianisha na jamii.

Kwamba afugwe haita leta maana tena kwa vile akifugwa hatatokea kwa bahati ya pekee akama inavyotokea bali ni kuonekana kila siku kitu ambacho hakitatuletea tafsiri kadiri ya ishara za nyakati alizotuandalia Muumba wetu. Jaribu Sabayi kukuza kipaji chako cha critical thinking. Thanks.

Mkuu hizo ni Imani tu umuhimu wake upo kwenye kuamini kama haumanini it doesn't make sense anayetafuta majibu rahisi kwenye mambo magumu ndo anahitaji kukuza kipaji chake cha critical thinking kama hatutaki kulima kwa njia za kisasa hautaji kakakuona kujua kama kutakuwa na njaa,kama hakuna haki na usawa ktk nchi hauhitaji kakakuona kujua kuwa Amani inaweza kuvurugika
 
Naona ameonekana DSM na anaoneshwa kwenye taarifa ya habari ya Clouds Tv. Kuna watu uwa wanaamini kwamba ana uwezo wa kutabiri je ni kweli ana uwezo huo?

Hivi Kakakuona ndiyo "Coyote" kwa lugha ya wenzetu?
 
Wamatumbi nyie kiboko, wajerumani wakitumia pweza kutabiri mtapongeza na kuona ugunduzi lakini wamatumbi wenzenu wakitumia kakakuona mnajidai mnashangaa, mbona hata nyuki wanaakili kuliko binadamu katika kutengeneza asali? binadamu hajakamilika na vingine anapata kutoka katika wanyama pia. Kama mbwa anatumika kunusa madawa ya kulevya na panya wananusa mabomu.
 
mbona mbwa na paka wanaweza kutoa taarifa za kifo cha mtu.....au hata hilo tunalibishia?
 
huyu mdudu ni muhimu sana na kuonekana kwake ni mara 1 ktk miaka zaidi ya 10, huwa anatumika kama mtabiri i.e anawekewa unga, bunduki etc akichagua bunduki ujue hali ya amani itakuwa tete na akichagua unga basi ujue kuna njaa kubwa inakuja,,, na pia kipande cha gamba lake kilikuwa kikiuzwa kwa bei mbaya sana kikiaminika kumletea mtu bahati anapotembea nacho, biashara, siasa etc

kwaio ndo "mwenye nyumba" anatembea na gambalake huko nchi za watu ili awe na bahati ya kugaiwa vyandaru vya fut 3?
 
huyu anaitwa Pangolin na ni kitoweo kwa nchi nyingi za Africa na Asia.....
how to cook a pangolin as described by a Guangdong
chef 'We keep them alive in
cages until the customer makes an order.
Then we hammer them unconscious, cut their
throats and drain the blood. It is a slow death.
We then boil them to remove the scales. We
cut the meat into small pieces and use it to make a number of dishes, including braised
meat and soup. Usually the customers take the blood home with them afterwards.'"
source:
en.m.wikipedia.org/wiki/Pangolin
 
mbona unachanganya habari?!, kama unakemea utabiri wa kakakuona kemea pia na unajimu wa hao viongozi wako wa dini maana nao ni viumbe kama alivyo huyo mnyama.

uyo kakakuona kwani katabiri nini hasa? hizi ni imani tu zisizo rasmi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom