Ni kweli hatuoni boriti machoni mwetu??

Nostradamus

JF-Expert Member
Jun 8, 2009
392
6
Kila siku katika kipindi kirefu sasa,Watanzania tumekuwa tumejiingiza katika malumbano na mijadala isiyokwisha.Lakini mjadala uliotuyumbisha zaidi umekuwa ni mjadala kuhusu ufisadi.
Kikubwa kinachonivutia katika mjadala huu ni kwamba wengi wetu tumeshindwa kujiangalia na kujikagua kama kweli kwa nia ya dhati tunastahili kulaani ufisadi.
Hivi kwani fisadi ni nani???? kwa tafsiri yangu ni kwamba" fisadi ni mtu yeyote anayetumia dhamana aliyokabidhiwa na wengi ili awatumikie kwa maslahi binafsi na kuwanyonya wale waliomtuma"(Mwanasiasa,daktari,askari, mhandisi,mkandarasi,mbunge, waziri ,raisi na hata mameneja au wakurugenzi wa mashirika ya umma)
Kwa mantiki hiyo basi,viwango vya ufisadi vinatofautiana kutegemeana na nafasi ya mtu kiutendaji na aina ya shughuli anayoifanya
Just imagine:----
umeajiriwa kwa makubaliano kwamba utaingia kazini saa1:30 asubuhi na utatoka kazini saa10:30 jioni,kwa siku tano za wiki,jumatatu hadi ijumaa.
Lakini badala yake unaingia kazini saa 3 na kutoka saa 9:30 huku muda mwingi ukitumia kunywa chai,kupiga simu za kifamilia,kuchat na marafiki kwenye chat zones,kupiga soga,lunch, na zaidi ni kuchangia hoja katika jamii forums.
Yote niliyoyaorodhesha hapo juu kumbuka hayapo kwenye mkataba wako wa ajira na yana-consume big ammount of your working time.mwisho wa siku unadai nyongeza mshahara huku kwa kigezo maisha yamepanda.
hivi tujiulize,ni nani kati yetu ambaye akikabidhiwa nafasi ya Rostam Aziz, "awe na uwezo wa kuteta na Raisi wa nchi muda wowote,awe na nguvu katika uteuzi wa mawaziri,awe amenunua idadi kubwa ya wajumbe wa vikao vya juu vya chama tawala,awe na wafuasi walio tayari kujidhalilisha na kudhalilisha wenzao kwa maslahi ya huyo bwana.
Je ni nani atayefanya kinyume na anavyofanya huyu bwana leo hii? Au tutafanya zaidi yake.
Siku yule dada aliyekamatwa kwa kosa la uzinzi,alikuwa anaenda kupewa adhabu inayomstahili ambayo ni kupigwa mawe hadi afe, ndipo Bwana Yesu akawaambia" asiyetenda dhambi hii na awe wa kwanza kurusha jiwe" wote tunafahamu nini kilitokea.
Ushauri wangu ni kwamba... Kizazi hiki cha watanzani kimeshaharibika kwa rushwa,uonevu,uzinzi,ubakaji, tamaaa na mbaya zaidi wivu na husda.Na wengi wetu tunaopiga kelele dhidi ya ufisadi ni kwa sababu tumekosa fursa ya kuwa mafisadi na endapo tukipata fursa tutakuwa mafisadi zaidi ya hawa wa sasa.
Tumuombe mungu ashushe gharika na kufuta hiki kizazi chooote au laa basi atokee mzalendo wa kweli atakayepokonya nchi hii toka mikononi mwa wanasiasa(demokrasia) na kuitawala kidikteta huku akitanguliza maslahi ya taifa mbele na sio maslahi yake binafsi.(rejea utawala wa FIDEL CASTROL.MUAMMAR GADDAFI,ROBERT MUGABE au ADOLF HITLER)
nawasilisha hoja...
 
Notradammus,
Uliemtaja kwa jina RA na wale wanaojulikana kama MAFISADI ndio Ndio wenye BORITI tuliobaki tuna vijiti na aliezidi labda atakuwa na kibazi. Huwezi hata kidogo ukalinganisha ULAFI wa JITU kama MKAPA, ROSTAM n Co. na waajiriwa wa kawaida. NYANGUMI na Kidagaa wapi kwa wapi?
 
Argument yako imekaa kama ya sophia simba, na rev.kishoka

My take: "Si kila mtu ni fisadi" No..kuna watu wema na waadilifu wengi tanzania kuliko wachafu na wezi ambao wengi wao ni wafanyakazi wa serikali (wasomi, wanasiasa+experts) na wafanya biashara wachache ..wengine kwenye informal sector 90% ni bidii na ubunifu kwa kwenda mbele
 
Argument yako imekaa kama ya sophia simba, na rev.kishoka

My take: "Si kila mtu ni fisadi" No..kuna watu wema na waadilifu wengi tanzania kuliko wachafu na wezi ambao wengi wao ni wafanyakazi wa serikali (wasomi, wanasiasa+experts) na wafanya biashara wachache ..wengine kwenye informal sector 90% ni bidii na ubunifu kwa kwenda mbele


Tatizo hapa ndugu Tumaini , je hawa wasafi katika ngazi za chini ni kwa nmana gani wanapigana na ufisadi? ufisadi unaanzia level ya mamesenja au masecretary! watu wako kimya, hao unaosema wasafi(well hawapokei rushwa) lakini wengi wao wanatoa!
 
Tatizo hapa ndugu Tumaini , je hawa wasafi katika ngazi za chini ni kwa nmana gani wanapigana na ufisadi? ufisadi unaanzia level ya mamesenja au masecretary! watu wako kimya, hao unaosema wasafi(well hawapokei rushwa) lakini wengi wao wanatoa!
Hawana kiongozi wa kuwapa matumaini wala maarifa kupigania haki zao na ufisadi...wapinzani wenyewe wakiulizwa mapato wenu yamekaaje wanaanza kufukuzana wanakatisha tamaa, wengine wanafanya maamuzi yao yenyewe yanakuwa ya chama...

Leadership gap iko si kwa ccm tu upinzani is even worse..wanafanya siasa kama one time opportunity (miaka minne wapinzani hawana ajenda nyingine zaidi ya ufisadi) utasema wana akili? au ni kundi la waganga njaa tu wasio na upeo?

Kwani wao hawana agenda kuhusu kilimo kwanini wasitangaze zaidi namna gani watamuinua mkulima na mfanayakzi kuliko ku-deal na issue moja for 4 years?

Wananchi wengi waadilifu wanaamini wapinzani ni mafisadi tu kama ccm lakini tatizo ni kwamba wao hawakushinda..matendo yao yanaonyesha tu jinsi wanavyoendesha vyama vyao..

Tunasubiri Mussa wetu watu sisi waadilifu..kutoka informal sector.
 
In principle, to be human is to be fisadi.

Wakristo wana concept yao ya "original sin" na ingawa sikubaliani na historia na mapokeao yake, lakini kimsingi inaonyesha kwamba wote tuna "dhambi" na hatuwezi kuepuka kutenda "dhambi" kama binadamu.

Still, this is no justification of transgression, rather it is an attempt at looking at things with a sane and sober perspective, without being caught up in an overly idealistic, even utopian, zealotry.

Waswahili walisema, msiba wa wengi harusi. Kwamba kitu kibaya inaweza kukosa makali yake kama kipo kwa kila mtu. Kwa minajili hii, tunapozungumzia ufisadi hapa, hatuzungumzii hizi dhambi ambazo kuzikwepa inabidi uwe mtume.

Of course watu wanachelewa kufika kazini. Lakini wengine wanachelewa kwa sababu ambazo ukiziangalia katika mfumo unaotaka social justice hata huwezi kuwalaumu. Kama city fathers wameiba hela za kujenga barabara, halafu maeneo yote ya karibu na mji ni prohibitively expensive, walalahoi wanakaa huko mwisho wa mji, walalahoi hawa hata wakichelewa kufika kazini mara nyingine inakuwa si issue kubwa, ingawa bado ni kitu kibaya. tena hata hao city fathers wanaweza kuona afueni kwamba walalahoi hawa walioibiwa hawajacharuka na kuwachinjilia mbali hawa city fathers.

Waswahili wanasema ukimchunguza sana bata hutamla. Kwa hiyo hili swala la ufisadi ni relative.Kama alivyosema mkuu hapo juu, huwezi kumlinganisha fisadi anayeiba mamia ya mamilioni ya dola, na kuharibu miundombinu ya nchi, na kuua watu kama matokeao ya hayo, na mtu ambaye yuko underpaid na ameiba karatasi za ofisini ili mtoto wake asome shule. Hapa utilitarian principles zinakataa kabisa.

Kwa hiyo, kama rais anshindwa kujiconduct in a way ya kuonyesha anapiga vita ufisadi ni vigumu kumtaka karani afike kazini on time.

Ndio maana tunaanza na ufisadi mkubwa, maana ukiushinda ufisadi mkubwa huu mdogo utaumaliza bila shida.

Of course kuna wengine wana bottom up philosophy lakini hii iko too theoretical at this point in Tanzania.
 
Kila siku katika kipindi kirefu sasa,Watanzania tumekuwa tumejiingiza katika malumbano na mijadala isiyokwisha.Lakini mjadala uliotuyumbisha zaidi umekuwa ni mjadala kuhusu ufisadi.
Kikubwa kinachonivutia katika mjadala huu ni kwamba wengi wetu tumeshindwa kujiangalia na kujikagua kama kweli kwa nia ya dhati tunastahili kulaani ufisadi.
Hivi kwani fisadi ni nani???? kwa tafsiri yangu ni kwamba" fisadi ni mtu yeyote anayetumia dhamana aliyokabidhiwa na wengi ili awatumikie kwa maslahi binafsi na kuwanyonya wale waliomtuma"(Mwanasiasa,daktari,askari, mhandisi,mkandarasi,mbunge, waziri ,raisi na hata mameneja au wakurugenzi wa mashirika ya umma)
Kwa mantiki hiyo basi,viwango vya ufisadi vinatofautiana kutegemeana na nafasi ya mtu kiutendaji na aina ya shughuli anayoifanya
Just imagine:----
umeajiriwa kwa makubaliano kwamba utaingia kazini saa1:30 asubuhi na utatoka kazini saa10:30 jioni,kwa siku tano za wiki,jumatatu hadi ijumaa.
Lakini badala yake unaingia kazini saa 3 na kutoka saa 9:30 huku muda mwingi ukitumia kunywa chai,kupiga simu za kifamilia,kuchat na marafiki kwenye chat zones,kupiga soga,lunch, na zaidi ni kuchangia hoja katika jamii forums.
Yote niliyoyaorodhesha hapo juu kumbuka hayapo kwenye mkataba wako wa ajira na yana-consume big ammount of your working time.mwisho wa siku unadai nyongeza mshahara huku kwa kigezo maisha yamepanda.
hivi tujiulize,ni nani kati yetu ambaye akikabidhiwa nafasi ya Rostam Aziz, "awe na uwezo wa kuteta na Raisi wa nchi muda wowote,awe na nguvu katika uteuzi wa mawaziri,awe amenunua idadi kubwa ya wajumbe wa vikao vya juu vya chama tawala,awe na wafuasi walio tayari kujidhalilisha na kudhalilisha wenzao kwa maslahi ya huyo bwana.
Je ni nani atayefanya kinyume na anavyofanya huyu bwana leo hii? Au tutafanya zaidi yake.
Siku yule dada aliyekamatwa kwa kosa la uzinzi,alikuwa anaenda kupewa adhabu inayomstahili ambayo ni kupigwa mawe hadi afe, ndipo Bwana Yesu akawaambia" asiyetenda dhambi hii na awe wa kwanza kurusha jiwe" wote tunafahamu nini kilitokea.
Ushauri wangu ni kwamba... Kizazi hiki cha watanzani kimeshaharibika kwa rushwa,uonevu,uzinzi,ubakaji, tamaaa na mbaya zaidi wivu na husda.Na wengi wetu tunaopiga kelele dhidi ya ufisadi ni kwa sababu tumekosa fursa ya kuwa mafisadi na endapo tukipata fursa tutakuwa mafisadi zaidi ya hawa wa sasa.
Tumuombe mungu ashushe gharika na kufuta hiki kizazi chooote au laa basi atokee mzalendo wa kweli atakayepokonya nchi hii toka mikononi mwa wanasiasa(demokrasia) na kuitawala kidikteta huku akitanguliza maslahi ya taifa mbele na sio maslahi yake binafsi.(rejea utawala wa FIDEL CASTROL.MUAMMAR GADDAFI,ROBERT MUGABE au ADOLF HITLER)
nawasilisha hoja...

Nchi zote za kiafrika zinaweza kuendelea tu iwapo zitatawaliwa ki dikteta, hizi bla bla za politics kila kukicha is just wasting our time bila kujijua, BELIEVE ME.

Kagame pale anafanya kazi nzuri sana, siku ataanza ujinga ujinga wa kuingiza demokrasia ya umma na vyama lukuki vitaanza hapo ndipo longo longo za wababaishaji wa wale wangangaji njaa wataanza kurudisha nyuma maendeleo.

Pia sisi watanzania HATUHESHIMIANI sababu hatujawahi pigana - Kenya wameanza kusonga sababu kuna heshima - kule kenya waziri hawezi kusema pumba akawa salama - ila kwetu mandam una mdomo we toa pumba kesho tunasoma magazeti then tunabaki kunun'gunika tu na kumwachia mungu - Watanzania Amkeni mmelala, Hii nchi ni Yenu na hawa ni watawala tu - Wanamaliza kila kitu watoto na wajukuu zenu watawacheka sana wakati wanasoma HISTORI ya nchi yenu - WAKE UP GUYS.

alutaaa...
 
"Huwezi hata kidogo ukalinganisha ULAFI wa JITU kama MKAPA, ROSTAM n Co. na waajiriwa wa kawaida. NYANGUMI na Kidagaa wapi kwa wapi?"

haijalishi dhambi kafanya nani na kwa kiwango gani,dhambi ni dhambi tu. hebu fikiria,ni wangapi watakaopata mwanya wa kufanya ufisadi watafanya kinyume? nina hakika ni wachache saana.
nilishawahi kusema jamii isiyojitambua haiwezi kujikwamua kutoka katika matatizo yake,na kutotambua matatizo yetu ndio kunakotufanya tushindwe kutokomeza swala la ufisadi..
jiulize.. unamuandaa mwanao kuwa nani baadae!?
Nina wasiwasi wengi mnawaandaa watoto wenu kuwa mafisadi wa siku za usoni kutokana na aina ya elimu munaoshinikiza kuwapa,hamuwaandai watoto wenu kuwa wakulima,wajasiria mali au wazalendo wenye mapenzi na nchi bali mnawaandaa waje kuwa wafanyakazi wa maofisini(wakurugenzi,mameneja,wahasibu,wanasiasa n.k ili kupitia huko wawe na mafanikio mazuri ya kimaisha ambayo hayaletwi bila kupita shortcut(ufisadi)
 
Back
Top Bottom