Ni kweli balozi zetu nje ya nchi zimeishiwa fedha?

Hali itaendelea kuwa mbaya endapo serikali haitaacha kukopa benki za ndani. Wachambuzi wa maswala ya pesa wanasema endapo mabenki yatapungukia pesa za kuwakopesha watu/makumpuni yenye miradi ya uzalishaji; pato la Taifa litapungua na hivyo kufanya makusanyo ya kodi yashuke. Hii ndio hali iliyotokea ulaya; mabenki yalipungukiwa na mitaji ikapelekea miradi ya uzalishaji kukosa mitaji na ndiposa GDP ikashuka na serikali zao kufilisika (mapato ya serikali hayatoshelezi kulipia gharama za uendeshaji + madeni makubwa).

Suluhisho mojawapo ya kujikwamua na kufilisika kwa Serikali yetu kamwe Serikali isikope mabenki ya ndani ili pesa zilizoko kwenye benki zielekezwe kwenye miradi ya uzalishaji hivyo kuinua pato la Taifa (GDP).
 
Jamaa kwani mnataka Tanzania ifilisike mara ngapi? Hapa tulipo ni tia maji- tia maji.
Serikali ipo katika ile hali ya 'hand - to - mouth'
 
CHANZO: NIPASHE 15 FEBRUARI, 2012

Sh. milioni 13, 402,081.20 bila kuzitolea maelezo.
''shilingi milioni 13, 402,081.20'' !!

Bajeti nzima ya serikali haijafikia shilingi ''milioni 13, 402,081.20,'' hata ungejumlisha zote toka uhuru! Sasa huyo mtu kaibaje ''milioni 13, 402,081.20'' ??!! Magazeti yetu feki, waandishi feki, wahariri vilaza wakubwa.


Haule aliambia kamati hiyo kuwa serikali imezuia mafao ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania, Abu Dhabi, Falme za Kiarabu, Mustafa Nyang'anyi, baada ya kubainika kwamba alitumia fedha za ... bila kuzitolea maelezo.
Kwa hiyo hela zikipotea unadaiwa tu na kazini unapeta, hakuna hatua za kisheria zinazoendelea? Angeulizwa huyo Katibu.

Kuhusu mahusiano ya kimataifa, Haule, alisema Tanzania imefunga ubalozi wake nchini Uholanzi kutokana na matatizo mbalimbali yakiwemo ya kupishana mtazamo wa masuala mbalimbali.
Kuna bifu gani ya kidiplomasia iliyofanya tufunge mahusiano ya kibalozi? Hakuna mwandishi aliyeona ni muhimu kumuuliza Katibu Mkuu hizi details? Vyombo vyetu vya habari ni uhoro mtupu. Hakuna professional community bovu Tanzania kama ya waandishi wa habari.
 
TAARIFA YA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA KUHUSU MALIPO YA MISHAHARA KATIKA BALOZI ZETU.


Tarehe 13/2/2010 Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ilifanya kikao cha pamoja na Menejimenti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Lengo la kikao hicho lilikuwa ni kujadili taarifa ya Hesabu za Wizara kwa mwaka wa fedha 2009/2010.

Kufuatia kikao hicho baadhi ya vyombo vya habari vilitoa taarifa ambazo siyo sahihi kufuatia masuala yaliyojadiliwa katika kikao hicho.

Wizara inakanusha taarifa hizo zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari, na sio kweli kwamba Balozi zetu zina matatizo makubwa ya kifedha.

Kilichozungumziwa katika kikao hicho ni kuwa Balozi zetu bado zinatumia viwango vya Posho ya Utumishi wa Nje ambavyo vimepitwa na wakati. Ili kuhakikisha kuwa viwango hivyo vya Posho ya Utumishi wa Nje vinaboreshwa ili kuendana na hali halisi ya maisha; Awali Wizara ilifanya mapitio ya Kanuni za Utumishi wa Nje (Foreign Service Regulations) zinazohusisha Posho ya Utumishi wa Nje na kuziwasilisha katika mamlaka husika. Kwa kuwa mapitio Kanuni hizo ziliandaliwa muda mrefu uliopita, Wizara iliona kuwa upo umuhimu wa kuunda kamati maalum ya kupitia kanuni hizo za Utumishi wa Nje. Kamati hiyo imeshakamilisha kazi yake na kuiwasilisha kwa Menejimenti ya Wizara kwa ajili ya uhakiki na hatimaye kuiwasilisha katika mamlaka husika.

Pamoja na kuwepo kwa changamoto hiyo ya kuwa na viwango vya Posho ya Utumishi wa Nje vilivyopitwa na wakati, Balozi zetu zimeweza kupelekewa mishahara yao ya kila mwezi pasipo kuchelewa. Aidha, tatizo jingine lililoelezwa ni upungufu wa Bajeti unaotokana na kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya Fedha nyingine za Kigeni.

Katika kuwezesha kutatua tatizo hili Hazina imekuwa ikilipa kwa wakati fidia inayotokana na kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania katika kila kipindi cha robo mwaka.

Kwa ujumla Balozi zetu zimeendelea kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa kutumia rasilimali fedha zilizopo katika Bajeti. Aidha, siku zote Wizara imekuwa ikipata ushirikiano mkubwa kutoka Hazina katika kushughulikia masuala ya fedha Balozini.

IMETOLEWA NA: WIZARA YA MAMBO YA NJE
NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, DAR ES SALAAM

14/2/2012

Hii nchi huko inakoelekea Mungu atunusuru maana tumekosa dira. Hakuna uhusiano kwa serikali kuishiwa fedha na mambo yaliyotabiriwa kwa sababu kukosa fedha kwa serikali yetu ni kwa sababu ya wizi na ufujaji wa mali na kujilimbikizia mali kwa viongozi wetu tuliowapa dhamana ya kutuongoza. Nchi hii sio masikini na ndiyo maana mheshimiwa alipoulizwa swali huko ughaibuni "kwa nini Tanzania ni maskini" alikosa jibu.

Hivi karibuni kulikuwa na habari kwenye vyombo vya habari kwamba mheshimiwa mmoja (Gaba-choli) alikuwa na mpango wa kuhamisha fedha zake na kuzipeleka nje ya nchi akazihifadhi huko. Kitendo hicho kimeitingisha benki moja hapa nchini hadi kuunda kamati ya kumfuata mfanyabiashara huyo kada wa ccm na kumuomba asihamishe fedha zake. Ilisemekana mfanyabiashara huyo anazo fedha zaidi ya asilimia hamsini (50) ya fedha zote katika benki hiyo.

Sasa mambo kama haya huyu ni mmoja tu anaitishia benki kwamba kama atatoa fedha zake uhai wa benki hiyo uko hatarini sasa fikiria wako wangapi wa namna hiyo? Matrillioni ya fedha yamewekwa huko kwenye mabenki ya ughaibuni na wakubwa hawa wa chama cha magamba bila aibu huku nchi inapoteza heshima kwa kutokuwa hata na hela ya mishahara kwa watumishi.

Inasikitisha na kusononesha sana kuona hata watanzania walio wengi wapo wapo tu na hawajui hasa kinachoendelea katika nchi hii kiasi kwamba na wakubwa nao wanalijua hili ndiyo maana hawajali wanaendelea kutesa. Utaona kesho ukitokea uchaguzi badala ya kurekebisha mambo wanawachagua hao hao. Kwa kweli tutaishia hivi hivi lakini na nchi nayo ndiyo inakwenda shimoni sasa. Ee Mungu tunusuru na huu utawala wa magamba. Amina
 
''shilingi milioni 13, 402,081.20'' !!

Bajeti nzima ya serikali haijafikia shilingi ''milioni 13, 402,081.20,'' hata ungejumlisha zote toka uhuru! Sasa huyo mtu kaibaje ''milioni 13, 402,081.20'' ??!! Magazeti yetu feki, waandishi feki, wahariri vilaza wakubwa.


Kwa hiyo hela zikipotea unadaiwa tu na kazini unapeta, hakuna hatua za kisheria zinazoendelea? Angeulizwa huyo Katibu.

Kuna bifu gani ya kidiplomasia iliyofanya tufunge mahusiano ya kibalozi? Hakuna mwandishi aliyeona ni muhimu kumuuliza Katibu Mkuu hizi details? Vyombo vyetu vya habari ni uhoro mtupu. Hakuna professional community bovu Tanzania kama ya waandishi wa habari.


Mimi NSSF yangu tuu inazidi hicho kiwango. Unazungumzia Serikali ya familia yako au ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania?
 
Mimi NSSF yangu tuu inazidi hicho kiwango. Unazungumzia Serikali ya familia yako au ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania?

Labda unamaanisha milioni 13.4020812. NSSF yako haiwezi kuwa na milioni 13, 402,081.20 kamwe.
 
Hatua mojawapo iliyochukuliwa ni kupunguza idadi ya watu wanaoambatana na Mhe. Rais kwenye ziara zake nje ya nchi , hili yeye mwenyewe kaliona na ameshatoa maelekezo kwa wizara ya mambo ya nnje kwa utekelezaji. kwa kuzingatia freq. ya safarari hizi ni kubwa pesa za kuhudumia balozi zetu zitapatikana

Ufumbuzi wa tatizo la kupunguza matumizi ya serikali ili kuokoa fedha lliwe ndio mwongozo wa kudumu, haitoshelezi eti kupunguza idadi ya wapambe wanaongozana na mkweree kwenye safari zake bali safari zenyewe zifanywe pale wananchi watakapopata faida ya safari hizo badala ya kwenda kubembea!!
 
Sioni faida ya hizo balozi. Nyingi zimejaa watoto wa viongozi ambao majina yao tunayasikia tangu tulipozaliwa. Sidhani kama hao huwa wanaishiwa kwa maana ya neno hilo. Bora balozi zote zifungwe maana hazina maana yoyote. Wengi wa mabalozi wamepewa kishkaji hawana cha maana wanachofanya.
 
Tutasema yote lakini tuangalie rasilimali za nchi hii na kisha tukumbuke ya kwamba ni matokeo ya kuendelea kushabikia CCM- magamba.hivyo basi mtatumia formula zote nyinyi wachumi lakini kwa TZ zita-prove fairule tu,foemula ya kweli kwa TZ ni kuing'oa CCM madarakani.hii ndio formula sahihi ya kuinua uchumi wa TZ,hizi zenu za kichumi kamwe hatuwezi kujinasua na hili janga.najua wengine watahoji je huko Ugiriki kuna CCM?jibu ni hapana,tusipende kulinganisha ki urahisi hivyo matatizo ya nchi yetu na kwingine bila kujua hasa chanzo cha matatizo yetu ni sawa na ya wengine?mfano matumizi mabaya ya rasilimali za TZ ni sawa na za Ugiriki?je Ufisadi uliopo hapa kwetu TZ ni sawa na ulioko Greece?je madini,mito,Ardhi,maziwa,bahari,mafuta na vingine vyote tulivyonavyo Ugiriki pia vipo?anyway kwangu mimi ninavyoona tukiwa na chama tawala hiki cha Magamba kamwe hata angelikuja mtaalamu wa uchumi kuliko wote dunia akatushauri kwa TZ hakuna kitakachobadilika,kwanza sioni ni nani wa kupokea na kuufuta ushauri huo,nani ataacha kukwapua mali za nchi kwa walioko madarakani,nani ataacha kupanga safu ya kufanya nao ufisadi kama chama ndo hiki cha CCM,ndio maana nasema formula pekee na ya kwanza kui-apply ni kuachana kabisa na CCM-magamba,kufuta kabisa katika historia ya kisiasa nchi hii.
Mtizamo wangu wakuu
 
Wadau, Nchi yetu inazidi kuelekea ktk aibu hadi kimataifa. Taarifa ya hali halisi ilivyo mbaya kama alivyokiri katibu mkuu, Mambo ya Nje ndg John Haule ni kuwa hali ni mbaya mno hadi balozi zinashinwa kuwalipa wafanyakazi wake mishahara, sembuse kulipia kodi za mapangnapango waliyokodi. Source;VOA news. My take: Hii ni ishara nyingine ya taifa kukosa dira na utawala. Fedha za madini, utalii, kodi zetu nk havijaweza kutusaidia lolote ktk huduma za ndani, wanazipeleka wapi viongozi wetu? Na bugeti za kila mwaka kwa wizara hii zinaliwa au wanapeleka wapi? Nawaomba hoja wadau tujadili!
 
Jamani mnataka mpaka mpigiwe filimbi ndo muelewe nchi imefilisika?
M.a.gamba wenyewe wamekili hilo!
 
''shilingi milioni 13, 402,081.20'' !!

Bajeti nzima ya serikali haijafikia shilingi ''milioni 13, 402,081.20,'' hata ungejumlisha zote toka uhuru! Sasa huyo mtu kaibaje ''milioni 13, 402,081.20'' ??!! Magazeti yetu feki, waandishi feki, wahariri vilaza wakubwa.


Kwa hiyo hela zikipotea unadaiwa tu na kazini unapeta, hakuna hatua za kisheria zinazoendelea? Angeulizwa huyo Katibu.

Kuna bifu gani ya kidiplomasia iliyofanya tufunge mahusiano ya kibalozi? Hakuna mwandishi aliyeona ni muhimu kumuuliza Katibu Mkuu hizi details? Vyombo vyetu vya habari ni uhoro mtupu. Hakuna professional community bovu Tanzania kama ya waandishi wa habari.


Acha ushamba wewee! Hivyo ndivyo inavyoandikwa...jitahidi uwe unasoma hotuba za bajeti..uandishi wa kiasi cha fedha za bajeti ni tofauti na jinsi ulivyofundishwa darasa la nne.

Katika bajeti tukisema kuwa kiasi kilichotengwa ni shilingi milioni kumi na tatu laki nne elfu mbili na themanini na moja na senti ishirini (13,402,081.20); basi kwenye uandishi wa kibajeti huandikwa "kiasi kilichotengwa ni shilingi milioni 13,402,081.20" na hii husomeka sh 13,402,081.20.

Neno milioni halimaanishi kuwa hizo pesa ni 1,000,000 x 13,402,081.20 bali hutangulia kumuelekeza msomaji atambue kuwa hiyo pesa iko katika kiwango cha milioni bila kuhesabu idadi ya sifuri au commas.

Jaribuni kufuatilia habari za bajeti za serikali kujua jinsi gani taarifa za bajeti zinavyoandikwa badala ya kuwaita waandishi ni VILAZA wakati WEWE ndiye kilaza usiyejitambua.
 
ni kweli govt imefilisika!mkulo,ngeleja ni mzigo mzito kwa jk!

Hapo kwenye red! Kama ni mizigo kwanini haituwi? Kama mtu ni mzigo na JK haoni hilo basi naye ni mzigo!! To me Jakaya Kikwete ndio mzigo tena mzito kwa taifa hili!!
 
Back
Top Bottom