Watanazania bwana. Takwimu zinaonyesha alikopa na ripoti ya BOT inaonyesha alikopa ila wewe unabisha eti hakukopa mabeberu walikuwa hawampendi! Hakuwa tishio kwao kihivyo na wala hakuwa amefikia kiwango cha kumnyima mikopo mengine yalikuwa propaganda tu.Hilo la kusema alikuwa anakopa silikubali! Alikuwa hapendwi na mabeberu! Watamkopeshaje? Upanuzi wa njia ya kimara hadi kibaha alienda kukopa wakamkatalia na kumwekea masharti makali ya barabara 4 yaani 2/2. Akasema atajenga kwa hela yake na akajeng kweli njia 12. 6(3/3) + 2 mwendokasi + 4 service road. Miradi ya Bwawa la Nyerere na SGR mabeberu yasingemkopesha kwasasa waliipinga! Sasa hela aliitoa wapi? Jamaa alikuwa mwamba kwelikweli!
Nakubaliana na mleta mada alikuwa na mazuri yake na mabaya yake. Kuna mazuri yake mengi tu hata mimi nimeyatambua baada ya kufa maana wakati yu hai nilikuwa naona mabaya yake tu.