ERoni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2013
- 44,309
- 92,259
Kwenye underground wengi sana wanafanya makosa, hasa kwa vile wanatumia mbinu kama zako, kuchukua fundi abunibuni tu mchoro then vipimo vinaanza. Underground inahitaji planning nzuri ili interaction kati ya juu na chini iwe nzuri, wengine wanazitenganisha, yaani unakuta ili utoke underground uingie nyumba ya juu ni lazima utoke nje ndio uende ndani, while unaweza kuidizain vizuri ukapata kigorofa cha kishkaji.NINA MAKOSA KADHAA NGOJA NIYAWEKE.
Kosa la kwanza!
Kiwanja sikununua nilipewa na Bi. Mkubwa(Mama mzazi) na tayari nilishakuwa na Milioni saba ninazo za kuanzia ujenzi hivyo nikamwita fundi mchundo nikampeleka site aanze ujenzi. Kosa ni kwamba sikumtafuta mchora ramani wala Engineer niliona ni kupoteza pesa tu.
Fundi mchundo kufika site akachukua karatasi na peni akachora ramani ya harakaharaka na akapima uwanja kesho ujenzi ukaanza.
Kile kiwanja kilikuwa cha muinuko na lazima ili usingi ukae sawa utoe underground ya chumba kimoja au viwili kwa ufanisi zaidi. Fundi akashauri eti tutaweka vifusi kujazia zile underground na sio tuweke vyumba. Kasheshe msingi ulipokaa sawa kila akipiga hesabu ya kuweka kifusi anaona kabisa haiwezekani kwa maana nafasi ya ground ni kubwa kifusi lazima kitavunja ukuta.
Nikapata hasara ya kujenga underground, ambayo kama ningechorewa ramani ningejiandaa toka mwanzo. Nikalazimika kutoa underground ya chumba kimoja kile cha pili kwa vile kilijua juu kidogo kuogopa gharama nikajazia kifusi. Bajeti ya msingi iliongozeka kwa zaidi ya milioni 1.5 kwa kuweka underground.
Kumbuka underground lazima umwage zege na nondo kama unajenga ghorofa.
KOSA LA PILI
Kwenye hatua ya kusimamisha Boma nikahamishwa kikazi mkoa mwingine hivyo nikawa najenga kupitia simu yaani Fundi ananiambia kinachohitajika nami namtumia pesa, halafu tukakubaliana Boma litaisha kwa siku tano na pesa nimlipe ya siku (daily pay) aisee ile kazi ilikuja kuisha kwa wiki mbili maana Fundi alikuwa anafanya kazi ikifika saa nane anaondoka sababu kibao. Na nilipigwa kwenye malighafi maana nilikuwa natuma pesa tu kwake.
Hapa nilijifunza kama unataka kumlipa Fundi kwa kila siku itakulazimu ushinde site au umtafute msimamizi.
KOSA LA TATU
Ramani ya nyumba niliochelewa na Fundi mchundo ina vyumba viwili tu vya kulala labda ukiongeza na ile underground ndio inakuwa vyumba vitatu. Na sio kama eneo halitoshi ila nadhanj kwa vile sio fani yake maana kaacha eneo kubwa tu la kutoa chumba kizima.
Sasa huwa nikipata nafasi nakwenda site na wanangu, wawili wa kike na mmoja wa kiume ambae ndio mkubwa wao. Sasa mwanzoni nilipanga yule wa kiume ndio atakuwa analala kwenye hiyo underground lakini ameniambia baba fanya ufanyavyo ila mimi sitalala huku bondeni kwenye banda la kuku akimaanisha ile underground.
Maana kile chumba kimejitenga kabisa na vyumba vya ndani, na siwezi kuweka watoto wa kike kule nitakuwa nimewatoa sadaka kwa vijana wa kiume watachangamkia fursa.
Nimepanga na mama watoto ile underground tuifanye stoo hakuna namna, mpaka sasa kichwa kinaniuma mwanangu wa kiume atalala wapi? Kuna muda wife ananitania eti tugawane vyumba yeye alale na watoto wa kike na mimi nilale na mwanangu wa kiume ili vyumba vitoshe.
Hiyo nyumba ramani yake pia ina jiko, dining, sebule, choo cha master na choo cha public.
Na siwezi kuua dining au jiko nifanye chumba kwa kuwa ni nafasi ndogo haitatosha kabisa.
Haya ndio makosa nilioyafanya kwenye ujenzi wa nyumba yangu ila nimejifunza vitu vingi sana kwenye ujenzi ambapo kama nitabahatika kujenga nyumba nyingine makosa haya hayatatokea tena.