Hapana,
Mara baada ya Mzee Karume kuuwawa, nafasi yake ingechukulkiw na Mzee Thabiti Kombo kama ilikuwa ni swala la seniority, ila Mzee Kombo alikuwa na imani sana na utaifa ya Jamhuri ya Muungani na alijua kuwa nafasi ile ilitakiwa mtu aliyesoma kukaribiana na Nyerere kuliko yeye. Kwa hiyo akashauri nafasi hiyo apewe Jumbe, na kweli Jumbe aliifanya vizuri sana akiwa analenga kwenye utaifa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania badala ya Zanzibar. Kama ulisikia ile hotuba ya Jumbe ya mwaka 1975 wakati wa uteuzi wa mgombea wa uraisi wa Tanzania wakati huo utakubaliana nami kuwa alikuwa na utaifa zaidi ya uzanzibari wakati huo. Jumbe aliipenda na aliifanya kazi yake ua umakamu wa Rais kwa ufanisi sana huenda kuliko makamu mweingine yeyote wa Rais katika historia ya Taifa hili. Wakati wa vita Uganda, Jumbe aliidhinisha hela kutoka akiba ya serikali ya mapinduzi ya zanzibar, kwa ajili ya kununulia BM40 ambazo hatukuwa nazo wakati ule na Nyerere hakuwa na hela za kupata silaha hizo mara moja katika muda mfupi ule. Maamuzi yote yaliyokuwa yakifanyika na kuigusa Zanzibar wakati huo, yalikuwa hayatimii bila ridhaa ya Mzee Jumbe na Mzee Kombo. Mzee Jumbe alighafilika kidogo tu kutokana na kuchukia popularity ya Sokoine kufuatia vita ya uhujumu uchumi ya mwaka 1983, na ikawa ndiyo mporomoko wake wa moja kwa moja kisiasa.
Mzee Jumbe hayupo kizuizini, anapata huduma zote kama kiongozi mstaafu wa nchi kwa nafasi aliyokuwa nayo. Ana ulinzi wa serikali, huduma za usafiri na mabo mengine. Kwa sasa huyu mzee umri umekwenda na hawezi kuhudhuria shughuli yenye usumbufu wa aina yeyote anahitaji muda mwingi wa kupunzika na kuangaliwa. Mimi nadhani wakati mwingine kabla ya kuanza kulalamikia jambo ni heri ungeuliza ili wenye taarifa waweze kukujulisha.
Mdondoaji,Amekuja kuonekana in Public siku aliyofariki mwanae ndio mara mwisho zifa zote za kitaifa haalikwi muulize mbona kuna makada wa CCM kama akina Kingunge juu ya utu uzima wao wanaalikwa.
Sidhani kama Mzee A.Jumbe yuko kifungoni! yuko huru kabisa na hata juzi juzi alipelekwa India kwa matibabu na mtoto wake mmoja kufariki huko akiwa anamtibu Baba yake!
Mzee Jumbe kwa sasa ni Mzee sana na afya yake imedhoofika sana tokana na umri! kwa umri ni mkubwa hata kuliko Mzee Nelson Mandela! na kwa sasa hata akialikwa ktk hafla za kitaifa itakuwa vigumu sana kuhudhuria!
daa aiseee mie simooo
What is excatly the title of that book? and where can I possibly find?
Ebu fafanua hapo kwenye Nyekundu, mwaka gani hiyo Historia, Maana tokea hii mipaka ya Africa iwekwe haijawai kubadilishwa au una-undugu na Museveni wa Uganda anaye dai kisiwa cha Kenya kuwa chake.
Hivi sasa ni karibu miaka 25 tangu Abdu Jumbe awekwe kwenye kifungo cha nyumbani kutokana na kile kilichohitwa kuchafua hewa ya siasa huko visiwani. Katika kipindi hicho baadhi ya wale walikuwa katika mstali wa mbele katia kumchongea Jumbe kwa Nyerere, ikiwemo Shariff ahmad na Ahmad Rashid walikuja kutemwa katika CCM na kuwekwa lupango kwa miaka kadhaa. Hivi sasa baada yakushikishwa adabu wajisalimisha kwa CCM. Hata hivyo ukiwasikiliza kwa mbali, wanataka katiba ya sasa ya serikali ya muungano ifanyiwe marekebisho ili tuwe na mfumo wa shirikisho. Hoja hiyo ndiyo iliyomuweka Jumbe korokoroni. Sasa, iwapo hoja hiyo hivi sasa inazungumzika kwanini mzee wetu huyo hasiachiwe huru na kurejeshewa haki zake zote kama rais wa Zanzibar na makamu wa rais wa Tanzania?
What is excatly the title of that book? and where can I possibly find?
Kichuguu,
Uliyazungumza mengi ni ukweli ila kuna tatizo moja umelisahau kulizungumza au kulisema. Nyerere alikuwa na influence na power mpaka visiwani na aliyekuwa na uwezo wa kupambana nae alikuwa ni Marehemu Karume peke yake. Alipofariki ndipo Nyerere alikuja akabadilisha baadhi ya vipengele wakati wa kuandika constitution ya Tanzania kuimeza Zanzibar. Haya yamezungumzwa na wanahistoria wengi nchini na nje ya nchi. Sasa unafikiri Thabit Kombo au Mzee Aboud Jumbe walikuwa na uwezo wa kumpinga maamuzi yake. Pesa za vita zilitoka lakini kwa shingo upande kwani zilikuwa ziende kufinance shughuli za maendeleo visiwani badala yake zikaenda kununua vifaa vya kijeshi. Hili liliwakera wengi ndio sababu ya rebellion by mzee Jumbe kutaka Zanzibar iwe inatambulika kama nchi ili iwe na uhuru wa kufanya maamuzi yake yenyewe pasina kuingiliwa au kulazimishwa na serikali ya muungano.
Mzee Jumbe hayupo kizuizini, anapata huduma zote kama kiongozi mstaafu wa nchi kwa nafasi aliyokuwa nayo. Ana ulinzi wa serikali, huduma za usafiri na mabo mengine. Kwa sasa huyu mzee umri umekwenda na hawezi kuhudhuria shughuli yenye usumbufu wa aina yeyote anahitaji muda mwingi wa kupunzika na kuangaliwa. Mimi nadhani wakati mwingine kabla ya kuanza kulalamikia jambo ni heri ungeuliza ili wenye taarifa waweze kukujulisha.
Mainland kutamu. Mwinyi yuko mainland haendi Zanzibar ila tu kwa shughuli. Salim yuko mainland haendi Zanzibar ila tu kwa shughuli.
Mainland kutamu!
Abdu Jumbe yupo hai kwa wale serengeti boys anaishi dar ila ni mzee sana