Ni kosa gani alilolifanya Aboud Jumbe kustahili 'kifungo cha maisha'?

Mdondoaji,

..hata Mzee Mwinyi naye kajibanza huku Tanganyika "analima" maembe.

..Sheikh Idiris Abdul Wakil Nombe naye alikuwa kajinafasi Ilala-Bungoni.

..Maalim Seif naye inasemekana alikuwa akiishi hotelini hapa DSM. sijui kama ni kweli.

..Hamad Rashid Mohamed naye anaishi Tanganyika akifanya biashara ya vyuma chakavu.

..Zanzibar itajengwa na nani kama watu kama hawa hawataki kwenda kuishi huko?

Mkuu,

Mzee Mwinyi anaishi pale Mikocheni ila kila baada ya wiki mbili anaenda zake zanzibar na ana nyumba zake kule anafikia .

Seif Sharif Hamad sijui,

Hamad Rashid ana biashara zake huku inaeleweka kwanini anapendelea kuishi huku.

Ila mkuu Mzee we Aboud Jumbe ni mzaliwa haswa wa zanzibar na hana biashara huku wala nini. Anakaa mahali nyumba ilikuwa katika hali mbaya sana kabla Mh. Mkapa kwa huruma akaenda kuokoa jahazi. Wanawe wengi wako hali mbaya sijui yule aliyekuwa akisome ukapteni wa ndege yuko wapi. Kuna siri inaendelea na pia kwanini yuko Dar wakati yeye alikuwa Rais wa Zanzibar.

Idriss Abdul Wakil sijui mkuu ila nadhani alikuwa anaishi Zanzibar na tumemzika Zanzibar ila hilo la Dar silijui.
 
Kama ni kweli huyu mzee hajatendewa haki kabisa katika maisha yake na katika hilo Nyerere alikosea kabisa. Nadhani ni kutokana na zile kauli mbinu za wakati ule kwamba, fikira sahihi zilikuwa za Nyerere tu.
 
Mdondoaji,

..labda Mzee Jumbe yuko more comfortable na maisha yake hapo Mjimwema.

..siamini kama hana uhuru wa kurudi Zanzibar au hata kuongelea zahama za kisiasa alizokumbana nazo. kumbuka kwamba tayari ameshaandika hata na kitabu.

..binafsi nikisikia Mzee Mkapa ameamua kuweka makazi yake Nairobi, na huku Tanganyika anakuja kutembea tu, nitashangaa sana.
 
Mdondoaji,

..hata Mzee Mwinyi naye kajibanza huku Tanganyika "analima" maembe.

..Sheikh Idiris Abdul Wakil Nombe naye alikuwa kajinafasi Ilala-Bungoni.

..Maalim Seif naye inasemekana alikuwa akiishi hotelini hapa DSM. sijui kama ni kweli.

..Hamad Rashid Mohamed naye anaishi Tanganyika akifanya biashara ya vyuma chakavu.

..Zanzibar itajengwa na nani kama watu kama hawa hawataki kwenda kuishi huko?

Jamani kwani Jumbe na Mwinyi au Hamadi sio watanzania? hawana haki ya kuishi dar kama ilivyo kwa watanzania wengine wanaishi Dar lakini wamezalio maeneo kama Kilimanjaro, Arusha, Mwanza au kwingine? mbona hamuwashangai Akina Adamu Mwakanjuki, Askofu John Ramadhani, na mamia ya wabara wanaishi Visiwani? yaani Mzanzibari akiishi Bara nimakosa, lakini mbara akiishi Zenji ni haki sio?

Kwanza Mzee Jumbe na Mwinyi hawakuzaliwa Unguja bali asili yao ni huku huku Bara! sasa kuna ajabu gani wao kuishi huku?
Sasa nini maana ya Muungano kama tutakuwa tukinyoosheana vidole kuwa huyu ni wa kule na yule ni wa huku sijui Tunaelekea wapi!!!
 
Mbaya wa Aboud Jumbe si Nyerere, bali ni muungano wa wazenji kadhaa ambao hawakukubaliana na mwenendo wa Jumbe wa kujiweka mbali na muungano baada ya kuona kuwa umuhimu wa nafasi ya makamu wa rais ulikuwa unamweza na nafasi ya waziri mkuu wakati huo, yaani Sokoine.

Kwa muda mrefu tangu mwaka 1974 nafasi ya Makamu wa Rais ilikuwa na umuhimu sana ambapo Jumbe alimwakilisha Nyerere katika shughuli mbalimbali za kitaifa na za kimataifa, na vile vile alitoa maamuzi mbalimbali kwa niaba ya Rais. Baada ya Sokoine kung'ara sana katika siasa za Tanzania, nafasi hiyo ya Makamu wa Rais ikawa kama imemezwa na nafasi ya Waziri mkuu, ndipo Jumbe alipojisikia vibaya na kutaka kuondoa Zanzibar kwenye Muungano, na kusababisha machafuko ya kisiasa ya 1983. Hatua hiyo ilipingwa na wazenji kadhaa wakiwemo akina Sharif Hamad, Mzee Thabit Kombo, Brigedia Natepe, na wengineo.

Baada ya nafasi yaje kuchukuliwa na Rais Mwinyi, Mzee yule aliendelea kupewa heshima zote kama rais mstaafu, na nadhani ndiye mtu pekee aliyelipwa na kuhudumiwa sana na watanzania bila kufanya kazi yoyote, kwani tangu mwaka 1983 hadi leo hii ni karibu miaka 30 na bado analipwa na kuhudumiwa kama Rais mstaafu. Sidhani kama kuna kiongozi mweingie aliyewahi kuhudumiwa namna hiyo.

Nadhani kuwa alikuwa kakurupuka sana kwa vile kama angekuwa msikivu kidogo, huenda baada ya Sokine kufariki mwaka 1984, yeye ndiye ambaye angeweza kuchukua nafasi hiyo ya urais baada ya Nyerere kustaafu mwaka 1985; nafasi ambayo baadaye ilichukuliwa na Mwinyi aliyekuwa amemrithi umakamu wa Rais.
 
... halafu inashangaza sana hawa hawa jamaa (wanasiasa) si wa chama tawala wala wa upinzani ndio wa kwanza kuwachochea wafuasi wao chuki na matusi dhidi ya Muungano. Kumbe wote wana makazi na biashara za kudumu upande wa pili wa Muungano (Tanganyika)! Na hata wengine makaburi yao yako Tanganyika (pale Kisutu, n.k) badala ya kwetu visiwani.
 
nyumba ya huyu mh. iliwekwa kwa mazingira ya kizuizini,enzi hizo kigamboni ilikuwa kama kisiwa,na ikumbukwe ilikuwa na wanajeshi,alipewa usalama kwa hadhi ya cheo chake,ila ukweli ni kuwa alikuwa anachungwa mawasiliano yake,nyendo zake kila kitu kilikuwa kinaripotiwa,hakuwa na ujanja.
ila mungu wa ajabu,amemlinda na kumpa uhai mrefu kuona waliomtenda wakifa na kupoteza mvuto.its not over until its over.
 
Mkuu,

Mzee Mwinyi anaishi pale Mikocheni ila kila baada ya wiki mbili anaenda zake zanzibar na ana nyumba zake kule anafikia .

Seif Sharif Hamad sijui,

Hamad Rashid ana biashara zake huku inaeleweka kwanini anapendelea kuishi huku.

Ila mkuu Mzee we Aboud Jumbe ni mzaliwa haswa wa zanzibar na hana biashara huku wala nini. Anakaa mahali nyumba ilikuwa katika hali mbaya sana kabla Mh. Mkapa kwa huruma akaenda kuokoa jahazi. Wanawe wengi wako hali mbaya sijui yule aliyekuwa akisome ukapteni wa ndege yuko wapi. Kuna siri inaendelea na pia kwanini yuko Dar wakati yeye alikuwa Rais wa Zanzibar.


Idriss Abdul Wakil sijui mkuu ila nadhani alikuwa anaishi Zanzibar na tumemzika Zanzibar ila hilo la Dar silijui.
kwanini wasirudi basi Zanzibar? maana thread zako zoote zinahimiza Uzanzibari! au huoni role model wako hawana muda na huo unazi unaohimiza?
 
Jamani basi hata kabla ya kutoa tuhuma muwe na uhakika wa historia basi... ati Jumbe yuko kifungo cha maisha!

Mkuu kama uliwahi kwenda kwa mzee huyu wakati wa nyerere ulikuwa huwezi kukatiza kama usabahiwa na askari wa JWTZ na mazingira ya hiyo nyumba ilikuwa kama yupo kizuizini kule. Tatizo vijana wa siku hizi wanasahau au hawafahamu alipokuja Mkapa ndio ikawa nafuu kwa huyu mzee ila sio tatizo pengine waliozaliwa miaka ya 80 ndio hawafahamu kitu kinachoendelea ila wengine waliozaliwa kabla wanajua kilichokuwa kinaendelea.
 
..kwanini haendi kupumzikia Zanzibar?

..Nyerere kaondoka madarakani muda mrefu sana, lakini Mzee Jumbe kajichimbia hapohapo Mjimwema hataki kurudi kwao.
Mainland kutamu. Mwinyi yuko mainland haendi Zanzibar ila tu kwa shughuli. Salim yuko mainland haendi Zanzibar ila tu kwa shughuli.
Mainland kutamu!
 
Mbaya wa Aboud Jumbe si Nyerere, bali ni muungano wa wazenji kadhaa ambao hawakukubaliana na mwenendo wa Jumbe wa kujiweka mbali na muungano baada ya kuona kuwa umuhimu wa nafasi ya makamu wa rais ulikuwa unamweza na nafasi ya waziri mkuu wakati huo, yaani Sokoine. Kwa muda mrefu tangu mwaka 1974 nafasi ya Makamu wa Rais ilikuwa na umuhimu sana ambapo Jumbe alimwakilisha Nyerere katika shughuli mbalimbali za kitaifa na za kimataifa, na vile vile alitoa maamuzi mbalimbali kwa niaba ya Rais. Baada ya Sokoine kung'ara sana katika siasa za Tanzania, nafasi hiyo ya Makamu wa Rais ikawa kama imemezwa na nafasi ya Waziri mkuu, ndipo Jumbe alipojisikia vibaya na kutaka kuondoa Zanzibar kwenye Muungano, na kusababisha machafuko ya kisiasa ya 1983. Hatua hiyo ilipingwa na wazenji kadhaa wakiwemo akina Sharif Hamad, Mzee Thabit Kombo, Brigedia Natepe, na wengineo.

Baada ya nafasi yaje kuchukuliwa na Rais Mwinyi, Mzee yule aliendelea kupewa heshima zote kama rais mstaafu, na nadhani ndiye mtu pekee aliyelipwa na kuhudumiwa sana na watanzania bila kufanya kazi yoyote, kwani tangu mwaka 1983 hadi leo hii ni karibu miaka 30 na bado analipwa na kuhudumiwa kama Rais mstaafu. Sidhani kama kuna kiongozi mweingie aliyewahi kuhudumiwa namna hiyo.

Nadhani kuwa alikuwa kakurupuka sana kwa vile kama angekuwa msikivu kidogo, huenda baada ya Sokine kufariki mwaka 1984, yeye ndiye ambaye angeweza kuchukua nafasi hiyo ya urais baada ya Nyerere kustaafu mwaka 1985; nafasi ambayo baadaye ilichukuliwa na Mwinyi aliyekuwa amemrithi umakamu wa Rais.

Kuna mengi yaliendelea achilia nafasi ya umakamu Rais, kuna pesa za karafuu zilizomezwa na muungano na huyu mzee hilo lilimuuma na kuhoji kwanini imekuwa hivyo. Pia kuna swala za Zanzibar kuwa nchi alilisimamia kwani alitaka kuwapo na serikali tatu na hilo likawa mwiba mkali kwa Nyerere akaona jamaa ni msaliti akishirikiana na kina Seif Sharif Hamad. Pia alihoji uhusiano wa Vatican na Tanzania na hilo halikumpendeza Nyerere akaona atamuharibia uongozi pengine (Soma katika kitabu chake).
 
kwanini wasirudi basi Zanzibar? maana thread zako zoote zinahimiza Uzanzibari! au huoni role model wako hawana muda na huo unazi unaohimiza?

Kwanza naomba tuheshimiane,

Mie ni mtanganyika pure born and bred huwezi kunitoa Tanganyika maana nimezaliwa tanganyika wazazi wangu watangayika huna vya kunibadilisha. Kama nilivyosema katika post zangu wazanzibar nimekaa nao na kwakweli nawasupport wanalolifanya kwani ukoloni mamboleo uliofanywa na Tanganyika mnajifanya hamuufahamu ni bora mkaufahamu vizuri sana. Labda nikuulize wewe je wazanzibari sio watanzania?
 
Enyi "great thinker who cannot think" hivi ni nani aliyewaloga na kuwafanya mdhanie kwamba Jumbe na Mwinyi wamezaliwa Zanzibar? Jumbe na Mwinyi wote ni wazaramo, tena ni wazaramo waliozaliwa katikati ya uzaramo. That is your answer.
 
Mkuu kama uliwahi kwenda kwa mzee huyu wakati wa nyerere ulikuwa huwezi kukatiza kama usabahiwa na askari wa JWTZ na mazingira ya hiyo nyumba ilikuwa kama yupo kizuizini kule. Tatizo vijana wa siku hizi wanasahau au hawafahamu alipokuja Mkapa ndio ikawa nafuu kwa huyu mzee ila sio tatizo pengine waliozaliwa miaka ya 80 ndio hawafahamu kitu kinachoendelea ila wengine waliozaliwa kabla wanajua kilichokuwa kinaendelea.

Hebu tuelezee maana yake unaonyesha kulishupalia hili, ulinzi wa kiongozi maana yake nini kama utawakuta walinzi halafu upite tu bila kuhojiwa.
 
Kuna mengi yaliendelea achilia nafasi ya umakamu Rais, kuna pesa za karafuu zilizomezwa na muungano na huyu mzee hilo lilimuuma na kuhoji kwanini imekuwa hivyo. Pia kuna swala za Zanzibar kuwa nchi alilisimamia kwani alitaka kuwapo na serikali tatu na hilo likawa mwiba mkali kwa Nyerere akaona jamaa ni msaliti akishirikiana na kina Seif Sharif Hamad. Pia alihoji uhusiano wa Vatican na Tanzania na hilo halikumpendeza Nyerere akaona atamuharibia uongozi pengine (Soma katika kitabu chake).

What is excatly the title of that book? and where can I possibly find?
 
Mkuu kama uliwahi kwenda kwa mzee huyu wakati wa nyerere ulikuwa huwezi kukatiza kama usabahiwa na askari wa JWTZ na mazingira ya hiyo nyumba ilikuwa kama yupo kizuizini kule. Tatizo vijana wa siku hizi wanasahau au hawafahamu alipokuja Mkapa ndio ikawa nafuu kwa huyu mzee ila sio tatizo pengine waliozaliwa miaka ya 80 ndio hawafahamu kitu kinachoendelea ila wengine waliozaliwa kabla wanajua kilichokuwa kinaendelea.

Niambie ni kwa kiongozi gani mstaafu unakoweza kwenda na kuingia bila kuhojiwa; unaweza kwenda kwa Warioba au kwa Mwinyi hivi hivi tu? Au na wao wako vizuizini?
 
Kuna mengi yaliendelea achilia nafasi ya umakamu Rais, kuna pesa za karafuu zilizomezwa na muungano na huyu mzee hilo lilimuuma na kuhoji kwanini imekuwa hivyo. Pia kuna swala za Zanzibar kuwa nchi alilisimamia kwani alitaka kuwapo na serikali tatu na hilo likawa mwiba mkali kwa Nyerere akaona jamaa ni msaliti akishirikiana na kina Seif Sharif Hamad. Pia alihoji uhusiano wa Vatican na Tanzania na hilo halikumpendeza Nyerere akaona atamuharibia uongozi pengine (Soma katika kitabu chake).

Tuwekee hicho kitabu hapa kama una soft copy, maana inawezekana maneno mengine umetunga, hasa kuhusu Vatican, Zanzibar kuwa nchi na karafuu!
 
Enyi "great thinker who cannot think" hivi ni nani aliyewaloga na kuwafanya mdhanie kwamba Jumbe na Mwinyi wamezaliwa Zanzibar? Jumbe na Mwinyi wote ni wazaramo, tena ni wazaramo waliozaliwa katikati ya uzaramo. That is your answer.

Tuwekee Birth Certificate zao hapa, otherwise tutaamini kuwa wewe ndiye uliyelogwa!
 
Back
Top Bottom